Monday, November 15, 2021

BALOZI MULAMULA AMPOKEA MJUMBE MAALUM WA WAZIRI MKUU WA UINGEREZA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimueleza jambo Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya biashara Tanzania Bw. Lord Walney walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya biashara Tanzania Bw. Lord Walney akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula wakati wa mazungumzo yao katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Ujumbe wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) katika kikao na Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya biashara Tanzania Bw. Lord Walney kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya biashara Tanzania Bw. Lord Walney, katika picha ya pamoja na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. David Concar (mwenye suti ya bluu), kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amempokea na kufanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya biashara Tanzania Bw. Lord Walney katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.


Bw. Walney yupo nchini kwa ziara maalum yenye lengo la kujitambulisha rasmi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kushiriki Kongamano la Biashara baina ya Tanzania na Uingereza litakalofanyika Jijini Dar es Salaam Tarehe 16 Novemba 2021.


Viongozi hao wamejadili fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na namna ya kuangalia njia za kuvutia wawekezaji kutoka Uingereza kuja kuwekeza nchini na wafanyabiashara wa Tanzania kuuza bidhaa zao nchini Uingereza.


Akiongelea ujio wa Bw. Walney nchini, Waziri Mulamula amesema kuwa pamoja na kwamba Tanzania na Uingereza zimekuwa na mahusiano ya muda mrefu katika eneo la biashara lakini biashara ambapo wafanyabiashara wa Uingereza wamekuwa wakiuza zaidi kuliko watanzania na kuongeza kuwa, kongamano hilo litawakutanisha wafanyabiashara wa Uingereza na Tanzania kwa lengo la kuhamasisha Waingereza kuja kuwekeza zaidi nchini na wafanyabiashara wa Tanzania kuuza bidhaa zao zaidi Uingereza.

 
“Kongamano hilo litawakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na Uingereza kwa lengo la kuhamasisha Waingereza kuja kuwekeza zaidi nchini na wafanyabiashara wa Tanzania kuuza bidhaa zao Uingereza,” amesema Balozi Mulamula.


Waziri Mulamula ameongeza kuwa Kongamano la wafanyabiashara wa Tanzania na Uingereza litafunguliwa rasmi na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa jijini Dar es Salaam.


Kwa upande wake, Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya biashara Tanzania Bw. Lord Walney amesema kongamano hilo litatoa fursa kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili kukutana na kujadiliana juu ya fursa zilizopo katika nchini hizi na namna ya kuzitumia kwa maslahi ya pande zote mbili.
“Naamini kuwa kongamano hilo litakuwa nafasi muafaka kwa wafanyabiashara wa Uingereza na Tanzania kukutana na kujadili fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zinazopatika kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi zetu,” amesema Bw. Walney.


Kongamano hilo pia linatarajiwa kuhusisha wafanyabiashara na wawekezaji zaidi ya 300 kutoka Tanzania na Uingereza.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.