Monday, November 10, 2014

Naibu Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Marekani Eneo la Maziwa Makuu


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb)  na Mjumbe Maalum wa Marekani kwenye Ukanda wa Maziwa Makuu, Bw. Russel D. Feingold alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo. Katika mazungumzo yao waligusia mchango wa Tanzania katika suala la amani Mashariki mwa  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 
Mkurugenzi wa Idara  ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Sokoine akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bw. Innocent Shiyo  wakifuatilia mazungumzo kati ya Naibu Katibu Mkuu na Bw. Russel (hawapo pichani).

Sehemu ya ujumbe uliofutatana na Bw. Russel wakifuatailia mazungumzo.
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa mazungumzo kati ya Balozi Gamaha na Bw. Russel (hawapo pichani)

Picha na Reuben Mchome

Friday, November 7, 2014

Mhe. Rais awaapisha Balozi Zoka na Balozi Shelukindo


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha na kumkabidhi vitendea kazi Mhe. Jack Mugendi Zoka kuwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo Novemba 6, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi vitendea kazi Mhe Jack Mugendi Zoka
 Mhe. Rais Kikwete akimuapisha Bw. Samwel William Shelukindo kuwa Balozi na Mshauri wa Rais masuala ya Diplomasia  Ikulu Jijini Dar es salaam. Kabla ya uteuzi huu, Balozi Shelukindo alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi vitendea kazi Balozi Samwel William Shelukindo.
Picha ya pamoja ya Mhe. Rais na Balozi Shelukindo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sfue pamoja na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Joseph Sokoine. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki na anayefuata ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akizungumza jambo na Balozi  Shelukindo baada ya kuapishwa.
Balozi Shelukindo (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wenzake kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Picha na Reginald Philip

Thursday, November 6, 2014

Naibu Waziri afanya ziara ya kikazi nchini Ufaransa


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungungumza na Mkurugenzi anayeshughulikia masuala ya Afrika kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa, Bw. Jean Christophe Belliard wakati wa ziara yake ya kikazi nchini humo.
Mhe. Dkt. Maalim (katikati)  akiwa na Mhe. Begum Taj (kulia), Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa wakati wa mkutano wao na Bw. Arnaud de Lamotte, Makamu wa Rais wa Kituo cha Biashara cha Kimataifa na Huduma za Serikali wa Ufaransa wakati wa ziara yake ya kikazi nchini humo.
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa MEDEF-International, Bw. Phillippe Gautier Taasisi ambayo imeandaa Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Ufaransa litakalofanyika Paris, Ufaransa mwezi Desemba, 2014.  
Mhe. Dkt. Maalim katika picha ya pamoja na Balozi Taj (wa pili kulia) na Bw. Chiristophe Gallean, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Starch of Tanzania. Mhe. Dkt. Maalim yupo nchini Ufaransa kwa ziara ya kikazi.
Mhe. Dkt. Maalim (mwenye tai nyekundu) na Mhe. Balozi Taj (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Maafisa wa Ubalozi mbele ya jengo jipya la Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa.

36 African countries mull ICC withdrawal

Foreign Minister Bernard K. Membe (MP.)

THIRTY six African countries, including Tanzania, are contemplating to withdraw their membership from the International Criminal Court (ICC) by January, next year, the National Assembly was told on Wednesday.

The African Union (AU) summit, slated for January, next year, is expected to discuss the matter, among others, according to the Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Mr Bernard Membe.

The move by the African countries comes at a time the Hague-based court summoned Kenyan President Uhuru Kenyatta to appear before it in regard to the postelection violence that rocked that country in 2007.

Minister Membe made the remarks in response to a supplementary question by Chwaka MP Yahya Kassim Issa (CCM), who expressed concern over Kenyatta’s summon while heads of state in Africa had earlier opposed the move.
“It is at this meeting that Africa will make a decision on whether to remain or pull out of the international court,” Minister Membe told the House.

Responding to a basic question raised by the legislator earlier, Mr Membe said the government of Tanzania was satisfied with the status of cooperation among African countries in addressing challenges they face.

He explained that despite arrest warrant being issued by the ICC to arrest several African leaders, the leaders have continued to walk around in various countries without being arrested, thanks to good cooperation between the governments.

Source: Daily News (06 November 2014)


Tuesday, November 4, 2014

Waziri Membe amuaga Balozi wa Qatar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Mhe. Bernard  K. Membe (Mb.) akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa kwanza wa Qatar nchini Tanzania Mhe. Jassim M. Al-Darwish alipokwenda kumuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
Waziri Membe akizungumza jambo na Balozi Jassim M. Al-Darwish huku Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Simba Yahya (kushoto) akisikiliza.
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Batholomeo Jungu akisikiliza mazungumzo kati ya Waziri Membe na Balozi Al- Darwish ambao hawapo pichani

--------------Hafla ya kumuaga Balozi Al-Darwish


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) akitoa neno la shukrani kwa Balozi wa Quatar Mhe. Jassim M. Al-Darwish, kwenye Hafla ya Chakula cha Mchana iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje  kwa ajili ya kumuaga Balozi Al-Darwish ambaye amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
Sehemu ya Wajumbe kutoka Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Ubalozi wa Qatar wakati wa hafla ya kumuaga Balozi Al-Darwish
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga pamoja na wageni wengine waalikwa wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kumuaga Balozi Al-Darwish wa Qatar ambaye amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
Balozi Jassim M. Al-Darwish akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya kumuaga ambapo alitoa shukrani kwa Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano aliopata katika kipindi chote alichokuwepo hapa nchini na kuomba ushirikiano huo uendelee.
Sehemu ya Wageni waalikwa wakati wa hafla ya kumuaga Balozi wa Qatar akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Simba Yahya (wa pili kulia) wakimsikiliza Balozi huyo (hayupo pichani) alipowahutubia.

Waziri  Membe (Mb.) akimkabidhi zawadi ya picha yenye mchoro wa Tembo  Balozi wa Kwanza wa Quatar nchini Tanzania Mhe.  Al-Darwish wakati wa hafla fupi ya kumuaga Balozi huyo ambaye amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini. 
Picha ya Pamoja. 

Picha na Reginald Philip

Monday, November 3, 2014

Ujumbe wa wanajeshi wamtembelea Balozi wa Tanzania nchini Malawi

Balozi wa Tanzania, nchini Malawi Mhe. Patrick Tsere (watatu  kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa wanajeshi sita ukiongozwa na Brigedia Jenerali  Ernest Golinoma Mstaafu (wanne kutoka kulia) walipo mtembelea Ofisini kwake wakiwa na Tuzo walizopata baada ya kushiriki mashindano ya mchezo wa gofu yaliyofanyika mwishoni mwa juma, mjini Lilongwe. Ujumbe huo wa wanajeshi kutoka Tanzania ulikuwa umealikwa na Jeshi la Malawi kucheza gofu ikiwa ni maadhimisho ya kuwakumbuka Waafrika walioshiriki Vita vya Pili vya Dunia na kutimiza miaka mia baada ya vita vya kwanza.
 

Sunday, November 2, 2014

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA LA VERNE WAPEWA SOMO KUHUSU USHIRIKI WA TANZANIA KATIKA UMOJA WA MATAIFA

Bw. Noel Kaganda, Afisa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York; na Bw. Suleiman Saleh, Afisa katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Washington D.C wakiwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha La Verne cha California waliotembelea Ubalozi wa Tanzania Washington D.C. kujifunza namna Tanzania inavyoshiriki katika Umoja wa Mataifa. Wanafunzi hao walipeperusha bendera ya Tanzania katika National Model United Nations (NMUN), iliyofanyika kuanzia tarehe 31 Oktoba hadi 2 Novemba 2014, huko Washington D.C.

Bw. Kaganda, akiwasilisha mada kuhusu ushiriki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, ikiwa ni pamoja na vipaumbele vya nchi katika vyombo, kamati, kamisheni, bodi na mikutano ya nchi wanachama wa mikataba mbalimbali ya Umoja wa Mataifa. Programu ya NMUN inatoa fursa kwa wanafunzi wa vyuo zaidi ya 5000 kutoka pembe zote za dunia kuvaa kofia za Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili dunia, ikiwemo migogoro, mabadiliko ya tabianchi, maafa, janga la umaskini, magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza na usawa na uwiano sawa wa kijinsia. Mafunzo haya kwa vitendo yanawajengea uelewa wa shughuli za Umoja wa Mataifa na  kuwapatia kionjo cha shughuli za kidiplomasia.

Washiriki wakifuatilia kwa makini mada inayowasilishwa. Pamoja na taarifa za kiuwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wanafunzi hao walipata wasaa wa kufahamu misingi na mikakati ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania iliyojikita katika kuendeleza mahusiano ya kiuchumi na kibiashara na kukuza fursa za uwekezaji. Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa zinaendelea kupokea wanafunzi kutoka shule na vyuo mbalimbali vya Marekani ambavyo vimeonesha kiu ya kupata uelewa wa shughuli za kidiplomasia na habari za vivutio vya kiutalii vilivyopo nchini.