Sunday, November 2, 2014

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA LA VERNE WAPEWA SOMO KUHUSU USHIRIKI WA TANZANIA KATIKA UMOJA WA MATAIFA

Bw. Noel Kaganda, Afisa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York; na Bw. Suleiman Saleh, Afisa katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Washington D.C wakiwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha La Verne cha California waliotembelea Ubalozi wa Tanzania Washington D.C. kujifunza namna Tanzania inavyoshiriki katika Umoja wa Mataifa. Wanafunzi hao walipeperusha bendera ya Tanzania katika National Model United Nations (NMUN), iliyofanyika kuanzia tarehe 31 Oktoba hadi 2 Novemba 2014, huko Washington D.C.

Bw. Kaganda, akiwasilisha mada kuhusu ushiriki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, ikiwa ni pamoja na vipaumbele vya nchi katika vyombo, kamati, kamisheni, bodi na mikutano ya nchi wanachama wa mikataba mbalimbali ya Umoja wa Mataifa. Programu ya NMUN inatoa fursa kwa wanafunzi wa vyuo zaidi ya 5000 kutoka pembe zote za dunia kuvaa kofia za Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili dunia, ikiwemo migogoro, mabadiliko ya tabianchi, maafa, janga la umaskini, magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza na usawa na uwiano sawa wa kijinsia. Mafunzo haya kwa vitendo yanawajengea uelewa wa shughuli za Umoja wa Mataifa na  kuwapatia kionjo cha shughuli za kidiplomasia.

Washiriki wakifuatilia kwa makini mada inayowasilishwa. Pamoja na taarifa za kiuwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wanafunzi hao walipata wasaa wa kufahamu misingi na mikakati ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania iliyojikita katika kuendeleza mahusiano ya kiuchumi na kibiashara na kukuza fursa za uwekezaji. Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa zinaendelea kupokea wanafunzi kutoka shule na vyuo mbalimbali vya Marekani ambavyo vimeonesha kiu ya kupata uelewa wa shughuli za kidiplomasia na habari za vivutio vya kiutalii vilivyopo nchini.

Saturday, November 1, 2014

Makamu wa Rais wa Afrika Kusini awasili nchini kwa ziara ya siku moja


Makamu wa Rais wa  Afrika Kusini, Mhe. Matamela Cyril Ramaphosa akiteremka katika ndege mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius  Nyerere Jijini  Dar es Salaam.  Mhe. Ramaphosa yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja ambapo pamoja na mambo mengine atazungumza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,  Mahusiano , Mhe. Stephen Wasira kwa pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dkt.  Mahadhi Juma Maalim (Mb), na Bi. Zuhura Bundala, Kaimu Mkurugenzi   wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa mapokezi ya  Makamu wa Rais wa Afrika Kusini.  
Mhe. Ramaphosa akilakiwa na Mhe. Wasira mara baada ya kuwasili.
Mhe. Ramaphosa akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika mara baada ya kuwasili. 
Mhe. Ramaphosa akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Talha Mohammed 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu  Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa Matamela alipofika Ikulu kwa mazungumzo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Ramaphosa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikino wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) kwa pamoja na Mhe. Wasira wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Makamu wa Rais wa Afrika Kusini (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea. Kulia ni Mhe. Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini 

Picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mazungumzo.


Picha na Reginald Philip


Thursday, October 30, 2014

IOM yakabidhi vifaa vya Kompyuta Wizarani

Mkurugenzi wa Idara Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza na Mkurgenzi wa Shirika la Kimataifa Ia Uhamiaji (I.O.M), Bw. Damien Thuriaux ofisini kwake alipokuja kukabidhi vifaa vya kompyuta kwa ajili ya Wizara.
Mazungumzo yakiendelea kati ya Balozi Mushy na Damien Thuriaux, huku Bibi Naomi Zegezege, Afisa Mambo ya Nje akinukuu.
Balozi Celestine Mushy akipokea moja ya vifaa hivyo.

Wataalam wa Masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Wizara wakishuhudia makabidhiano hayo
Picha ya pamoja.


Wednesday, October 29, 2014

PRESS RELEASE

H.E. Dilma Rousseff, President of Brazil


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to Her Excellency Dilma Rousseff on the occasion of her re-election as President of the Federative Republic of Brazil.

The message reads as follows.

“Her Excellency Dilma Rousseff
  The President of the Federative Republic of Brazil,
  Brasilia,

  BRAZIL.

I have received with great pleasure the news of your re-election to the highest office of your country. On behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, I wish to convey my sincere and warmest congratulations to You and through you to the Government and the people of the Federative Republic of Brazil for your election to the Presidency of Brazil.

Your re-election is a sign of the trust and confidence that the people of Brazil have in your leadership qualities. As you continue discharging the noble duties bestowed upon you, I would like to assure Your Excellency of my continued co-operation in further strengthening the bilateral relations that so happily exist between our two countries.

Please accept, Your Excellency, my personal regards and best wishes for your continued good health and success”.


ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

29TH OCTOBER, 2014

PRESS RELEASE

H.E. Recep Tayyip Erdogan, President of Turkey


PRESS RELEASE

H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E Recep Tayyip Erdogan, President of the Republic of Turkey on the occasion of the National Day of Turkey.

The message reads as follows.

“His Excellency Recep Tayyip Erdogan,
The President of the Republic of Turkey,
Istanbul,
TURKEY.

Your Excellency,

It gives me great pleasure, on behalf of the people and Government of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, to extend cordial congratulations to You, and through you to the Government and the people of the Republic of the Turkey on the occasion of the 91st Anniversary of the Proclamation of the Republic of Turkey.

Our historic bilateral relations are multifaceted and cooperate in many areas such as education, agriculture, trade, tourism and transportation.
 
On this special occasion, I wish to cherish and celebrate these bilateral relations that exist between our two countries. Let me also take this opportunity to assure you that the Government of Tanzania remains committed to maintain and consolidating these relations for the mutual benefit of the people of our two countries.

Please accept, Your Excellency, my personal regards and best wishes for your continued good health and success”.


ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

29TH OCTOBER, 2014

Tuesday, October 28, 2014

TANZANIA YAKATAA RASMI NDOA ZA JINSIA MOJA KWENYE AGENDA ZA MAENDELEO YA MILENIA

Mkurugenzi wa Idara Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza kwenye warsha ya siku moja kuhusu Malengo ya Milenia kwa washiriki mbalimbali na kwa kiasi ngani Tanzania imeweza kufikia malengo hayo.
“Watanzania na Afrika kwa ujumla inataka malengo ya millennia na haki za binadamu zizifike mahali kuwadharirisha watu kutoka bara hili kwa kuruhusu mambo yanayokwenda kinyume na historia yao, mila na desturi za mwafrika,”aliongeza.
Kwa upande wake, Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Osward Mashindano amesema kwamba malengo ya milenia kwa kiasi kikubwa yamefikiwa na Tanzania hasa katika upande wa elimu na kupunguza vifo vya wakinamama na watoto wakati wa kujifungua.
“leo tumekutana hapa kuzungumza ni kwa kiasi ngani nchi yetu ya Tanzania imefikia malengo ya milenia na changamoto ni zipi katika malengo mapya ambayo ni 17 badala ya 8 ya awali,” aliongeza
Dkt Mashindano alifafanua kwamba ni lazima sasa serikali kutazama katika Nyanja za ubora katika huduma hizi muhimu kwa jamii baada ya kufikia lengo la kuandikisha watoto wenye umri wa kwenda shule kwa asilimia 85.
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Wanawake, Anna Collins akitoa hotuba yake wakati akifungua warsha ya siku moja kuhusu Malengo ya Milenia kwa washiriki mbalimbali na kwa kiasi ngani Tanzania imeweza kufikia malengo hayo.iliofanyika Makao Makuu ya Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF) Oktoba 27, 2014 jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi wetu
SERIKALI ya Tanzania imekataa rasmi kutambua ndoa za jinsia moja (ushoga) kama moja ya agenda za maendeleo katika malengo ya milenia 2015 mpaka 2030 katika mkutano wa Umoja wa Mataifa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye mkutano wa majadiliano ya malengo ya milenia yanayotazamiwa kumalizika mwakani na kuanza malengo mapya, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy amesema serikali ya Tanzania imekataa kutambua ushoga kama moja ya agenda za maendeleo.
“tunatambua haki za binadamu, usawa wa kijinsia kati ya wanaume na wanawake na hata katiba yetu pendekezwa imetoa haki za sawa kati ya wanaume na wanawake lakini katika swala la kutambua ndoa za jinsia moja hilo tumekataa,” amesema Balozi Mushy
Amesema kwamba tumewaambia nchi zilizoendelea na wahisani wa maendeleo katika Umoja wa Mataifa kwamba swala la ndoa za jinsia moja (ushoga) si agenda ya watanzania na si agenda ya maendeleo.
Wadau mbalimbali walioudhuria wakifuatilia mada mbalimbali.

Mhadhiri wa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Osward Mashindano akifafanua umuhimu wa kuwashirikisha wananchi wa ngazi ya chini kuhusu maswala ya malengo ya milenia ili yaweze kufikiwa kwa urahisi zaidi.
Aliongeza kwamba Tanzania na dunia kwa ujumla wameona ni muhimu kuweka agenda ya ubora katika kila agenda za malengo ya milenia kwa nchi zote ambao ni wanachama wa Umoja wa Mataifa.
Dkt Tausi Kida, Mkurugenzi wa Programu wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii, amesema kwamba malengo haya ya milenia ni lazima yaguse maisha ya watu katika ngazi ya chini ili matokeo chanya yaweze kuonekana kwenye jamii
Amesema kwamba ni lazima nchi zilizoendelea ziweke mkazo katika kuhakikisha kwamba nchini zinazoendelea zinajengewa uwezo wa kutafuta fedha za kutimiza malengo ya milenia.