Friday, August 14, 2015

Naibu Waziri Mambo ya Nje aongoza ujumbe wa Tanzania Mkutano wa Baraza la Mawaziri SADC

Dkt. Stagomena Tax, Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC akitoa hotuba ya ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Mawaziri wa jumuiya hiyo.

Picha ya pamoja ya Mawaziri waliohudhuria Kikao cha Baraza la Mawazi wa Nchi wanachanama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC, Jijini Gaborone, Botswana tarehe 14-15 Agosti, 2015


Mhe. Mahadhi J. Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Mawaziri wa  Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) Jijini Gaborone, Botswana Ijumaa Agosti 14, 2015.

Ujumbe wa Tanzania kwenye Kikao cha Baraza la Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya SADC uliiongozwa na Mhe. Mahadhi J. Maalim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje (wa pili kulia), akifuatiwa na Balozi Simba Yahya, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje. Wengine mstari wa mbele ni Bw. Musa Uledi, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara (wa pili kushoto) na Dkt. Hamis Mwinyimvua, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha. 


Kongamano la Diaspora na Wajasiriamali likiendelea kwa siku ya pili jijini Dar es Salaam



Chukwu-Emeka Chikezie akiongoza moja ya mdahalo katika kongamano la Diaspora, Balozi wa Marekani nchini Mhe. Mark Childress kwa pamoja na Bw. Ali Mufuruki, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maafisa Watendaji Wakuu nchini, Bw. Richard Miles, Mwakilishi wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Marekani nchini na Dkt. Silencer Mapuranga, Mchumi kutoka ITC.
Balozi wa Marekani nchini, mhe. Childress akichangia mada kuhusu mabadiliko ya kiuchumi Tanzania wakati wa Kongamano la Diaspora.
Bw. Miles nae akichangia wakati wa mjadala kuhusu mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania na namna ya kuwashirikisha wafanyabiashara wadogo na wakati katika maendeleo ya nchi.
Balozi Mulamula akizungumza wakati wa mjadala huo 
Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing akiwasilisha mada kuhusu Mapinduzi ya Viwanda nchini na wajibu wa Diaspora katika ukuaji wa SME's
Balozi Lu akiwasilisha mada yake
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Modest Mero wakimsikiliza Balozi wa China nchini (hayupo pichani) wakati akiwasilisha mada
Washiriki wakifuatilia mada kutoka kwa Balozi wa China
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. Hemed Mgaza akiwa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Achiula wakisikiliza kwa makini uwasilishwaji wa mada wakati wa kongamano la Pili la Diaspora.
Mada zikitolewa
Maafisa Mambo ya Nje wakijadili jambo 
Timu ya Waandishi wa kumbukumbu za mkutano kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakinukuu taarifa mbalimbali wakati wa Kongamano la Diaspora ili kuweka kumbukumbu za tukio hilo sawasawa
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo akizungumza wakati wa kongamano hilo
Mada zikiendelea kutolewa wakati wa kongamano hilo 
Washiriki wa kongamano 


Picha na Reginald Philip

Rais Kikwete ashiriki hafla ya chakula cha jioni kuhitimisha Kongamano la Pili la Diaspora



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.
 Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Watanzania waishio Ughaibuni (Diaspora) hawapo pichani wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa ajili ya kuhitimisha Kongamano la Pili la Diaspora katika Hotel ya Serena Jijini Dar es Salaam
Mhe. Rais akisisitizia jambo kwa Watanzania waishio Nje 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Bi. Rosemary Jairo akimsikiliza Rais Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na Diaspora wakati wa hafla ya chakula cha jioni.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju (kulia) akiwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bi. Zuhura Bundala (kushoto).
Sehemu ya wageni waliohudhuria hafla hilo wakimsikiliza Mhe. Rais Kikwete (hayupo pichani).
 
Rais Kikwete akiendelea na hotuba yake
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula naye akizungumza wakati wa hafla hiyo ya chakula cha jioni.
Balozi Mulamula akiendelea kuzungumza

Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.
Wana Diaspora kutoka nchi mbalimbali na Tanzania  wakati wa hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa maalum kwa ajili ya kufunga Kongamano la pili la Diaspora. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mirisho Kikwete (kushoto) akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wa NHC kwenye masuala ya Diaspora Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Bwa. Nehemia Mchechu (Kulia)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mirisho Kikwete (kushoto) akimkabidhi cheti Mkurugenzi Mtendaji kutoka Kampuni ya Huawei nchini Bw. Sung

Balozi wa China nchini, Mhe. Lu akizungumza na mdau walipo hudhuria hafla ya chakula cha jioni kwa ajili ya kuhitimisha Kongamano la Pili la Diaspora nchini 
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mugendi Zoka akibadilishana mawazo na Watanzania waishio Nje waliohudhuria hafla ya chakula cha jioni
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza  na Mkurugenzi Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju (kulia), na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bi. Zuhura Bundala

Mkurugenzi Msaidizi, Bw. James Bwana (kulia),  akibadilishana Mawazo na Afisa Mambo ya Nje Bw. Hassan Mwamweta (kushoto).
Rais Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Bi. Rosemary Jairo (kushoto) na kulia ni Mtoto wa Bi. Rosemary Jairo 
Rais Kikwete (mwenye tai nyekundu) akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na Watanzania waishio Nje.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Kamati iliyoandaa Kongamano hilo.













Picha na Reginald Philip.

Waziri Membe atembelea mabanda ya maonesho wakati wa Kongamano la Diaspora

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (kushoto) akipata maelezo kuhusu na matumizi ya Gesi Asilia, Miradi na manufaa yake kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Bw. James Mataragio (kulia) alipotembelea banda la shirika hilo wakati wa Kongamano la Watanzania waishio Ughaibuni (Diaspora) 


Waziri Membe akionyeshwa na Bw. Mataragio eneo bomba la gesi asilia lilipopita kwenye Mchoro wa Ramani ya Tanzania uliopo mbele yao.
Waziri Wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika picha ya pamoja na Bibi Dorcas Membe (kushoto), Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Bw. James Mataragio (Kulia), Kaimu Mkurugenzi Idara ya Diaspora, Bi Rosemary Jairo (wa pili kutoka kulia) na Watumishi kutoka katika shirika hilo.
Waziri Membe na Mkewe Mama Dorcas wakipata maelezo juu ya matumizi ya radio calls kutoka kwa  Bw. Sunji wa Kampuni ya Huawei nchini alipotembelea banda la Kampuni ya hiyo wakati wa Kongamano la Diaspora.
Waziri Membe (wa kwanza kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) nchini, Bi. Matilda Nyallu. Kushoto kwa Mhe. Membe ni Balozi Mulamula, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Balozi Mulamula (katikati) akielezea jambo kwa Waziri Membe (kushoto).
Waziri Membe akisalimiana na mmoja wa  Washiriki wa Kongamano la Pili la Diaspora,Bw. William Malecela. Kulia ni Balozi Mulamula na katikati ni Bi. Suzani Mzee kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Bi. Rosemary Jairo (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Itifaki, Bw. James Bwana (wa pili kutoka kushoto)na Maafisa Mambo ya Nje Bw. Batholomeo Jungu ( kulia) na Bw. Amosi Tengu ( kushoto). 

Picha na Reginald Philip