Wednesday, December 9, 2015

Wizara ya Mambo ya Nje na Mfuko wa UTT/PID watiliana saini makubaliano ya kuendeleza viwanja vya Balozi za Tanzania nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) wakiweka saini Mkataba wa Hati ya Makubaliano (MoU) na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Umoja Unit Trust (UTT/PID),  Dkt. Gration Kamugisha,  Makubaliano hayo yatatoa fursa kwa Mfuko wa UTT/PID kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje katika kuendeleza viwanja na majengo mengine ya Ofisi za Balozi zilizopo nje ya nchi.  
Balozi Mulamula na Dkt. Kamugisha wakibadilisha Mkataba huo mara baada ya kuweka saini 
Viongozi mbalimbali wa Wizara ya Mambo ya Nje nao wakishuhudia zoezi hilo la uwekaji saini Kutoka kulia ni Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. James Lugaganya, Mkurugenzi wa Sera  na Mipango, Balozi Baraka Luvanda, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria na Bw. Gerald Mbwafu, Afisa Mambo ya Nje.
Ujumbe ulioambatana na Dkt. Kamugisha nao wakishuhudia tukio hilo
Balozi Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Dkt. Kamugisha
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula na Mtendaji Mkuu Dkt. Kamugisha wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi Luvanda (wa tatu kutoka kulia),  Bi. Kasiga (wa kwanza kulia), na Maafisa Mambo ya Nje, Bw. Mbwafu (wa pili kutoka kulia) na Bi. Happy Ruangisa (wa kwanza kushoto) 

Picha na Reginald Philip


========================

TAARIFA YA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUSAINIWA KWA HATI YA MAKUBALIANO KATI YA WIZARA NA MFUKO WA UTT/PID

Ndugu wanahabari nimewaita leo ili mshuhudie tukio muhimu la uwekaji saini wa Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mfuko wa Umoja Unit Trust (UTT/PID). 

Makubaliano haya yatatoa fursa kwa Mfuko wa UTT/PID kwa kushirikiana na Wizara yangu kuendeleza viwanja na majengo mengine ya Ofisi zetu za Balozi zilizopo nje ya nchi.

Kama mnavyofahamu, Serikali ina Balozi 35 katika nchi mbalimbali duniani. Tumefanikiwa kuwa na majengo yetu wenyewe kwa ajili ya ofisi na makazi ya maafisa wetu katika Ofisi za Balozi za baadhi ya nchi. Majengo hayo yamejengwa au kununuliwa kwa kutumia fedha za Bajeti ya Maendeleo za Serikali na imesaidia kupunguza mzigo mkubwa kwa Serikali wa kulipa gharama kubwa za kodi ya pango katika nchi hizo.

Ieleweke kwamba, nia ya Wizara ni kuendeleza viwanja na majengo yote yanayomilikiwa na Ofisi za Balozi nje ya nchi.  Hivyo, Wizara imebuni mkakati wa kushirikiana na wabia mbalimbali kuhakikisha kuwa viwanja au majengo yanayomilikiwa na Balozi nje ya nchi vinaendelezwa.

UTT/PID ni mmoja wa washirika aliyeitikia wito wa mkakati huo wa Wizara ambapo baada ya kusainiwa kwa Makubaliano haya, Wizara katika siku chache zijazo itakabidhi kwa UTT/PID ripoti ya viwanja na majengo mengine inayomiliki nje ya nchi ili waainishe maeneo watakayoanza kuyaendeleza kwa kuzingatia kigezo cha fursa za kiuchumi.

Lengo la Wizara kuviendeleza viwanja hivyo, sio tu kupata ofisi na makazi ya kudumu ya maafisa wa Ubalozi bali pia kwa ajili ya vitega uchumi ambapo ofisi za ziada zitapangishwa kwa ajili ya kuingizia mapato Serikali.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
08 Desemba, 2015

Friday, December 4, 2015

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje aongoza maadhimisho ya miaka 44 ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE)



Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya miaka 44 ya  Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) zilizofanyika kwenye Ubalozi wa UAE hapa nchini hivi karibuni. Katika hotuba yake Balozi Yahya alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na UAE ili kujiletea maendeleo.
Sehemu ya Mabalozi na Wageni waalikwa walioshiriki maadhimisho ya miaka 44 ya UAE
Balozi wa UAE hapa nchini, Mhe.Abdulla Ibrahim Alsuwaidi nae akitoa hotuba wakati wa maadhimisho hayo ambapo aliisifu Tanzania kuwa ni nchi inayoshirikiana kwa karibu na UAE katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Abdallah Kilima akiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara hiyo, Bi. Mindi Kasiga (katikati) pamoja na wageni wengine waalikwa wakifuatilia hotuba ya Balozi Alsuwaidi (hayupo pichani).
Balozi Yahya kwa pamoja na Balozi Alsuwaidi na Mabalozi wengine wakikata keki kuashiria maadhimisho ya miaka 44 ya UAE
Balozi Yahya na Balozi Alsuwaidi wakimkabidhi tiketi ya ndege ya shirika la Emirates Afisa kutoka Ubalozi wa Msumbiji alipojishindia tiketi hiyo katika droo iliyoendeshwa kusherekea miaka 44 ya uhuru wa UAE
Balozi Yahya nae akifurahia tiketi ya Ndege ya Shirika la ETIHAD baada ya kushinda bahati nasibu katika halfa hiyo. Shirika hilo kutoka UAE limezindua safari zake hapa nchini tarehe 01 Desemba, 2015
Kiongozi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa DRC, Mhe. Juma Halfan Mpango nae akifurahia zawadi aliyojishindia
Mtoto mdogo aliyeshiriki maadhimisho hayo ni mmoja kati ya wale waliojishindia tiketi ya Ndege ya Shirika la ETIHAD

Balozi Kilima akiwa na Bw. Seif Kamtunda, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia matukio
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Hangi Mgaka nae akifuatilia matukio wakati wa maadhimisho ya UAE.

.............Matukio mengine kwenye maadhimisho ya miaka 44 ya UAE


Balozi Abdulla Ibrihim Alsuwaidi akimpokea Balozi Yahya alipowasili Ubalozini hapo kabla ya kuanza maadhimisho ya miaka 44
Balozi Alsuwaidi akimpokea Balozi Abdallah
Balozi Alsuwaidi akimkaribisha Balozi wa Uganda hapa nchini
Balozi Alsuwaidi akimkaribisha Balozi wa Vatican hapa nchini
Bi. Mindi akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya miaka 44 ya UAE
Bw. Omar Mjenga (kushoto) kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nae akiwa kwenye maadhimisho hayo.
Wageni waalikwa
Bi. Ester Baruti (kulia), Mwakilishi wa Kampuni ya Dangote hapa nchini akishiriki maadhimisho ya UAE
=======================
Picha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Ujenzi wa Mahakama ya Kimataifa waanza jijini Arusha.



Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Baraka Luvanda (wa pili kulia), Msajili wa MICT Bw. John Hocking (wa pili kushoto) Afisa wa MICT Bw. Bw. Samwel Akorimo (wa kwanza kulia) na Afisa Mambo ya Nje Bw. Elisha Suku (wa kwanza kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja. 

Umoja wa Mataifa umeanzisha mradi wa ujenzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Masalia ya kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (Mechanism for International Criminal Tribunals (MICT) katika eneo la Lakilaki jijini Arusha.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Baraka Luvanda, kwa niaba ya Wizara hiyo ametembelea mradi huo tarehe 02/12/2015 ili kujionea maendeleo ya ujenzi huo.

Ujenzi huo unahusisha masijala ya nyaraka mbalimbali za Mahakama ya kimataifa ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) ambayo inahitimisha shughuli zake tarehe 31/12/2015.

Eneo hilo la Lakilaki limetengwa mahsusi kwaajili ya taasisi mbalimbali za kimataifa ambapo mpaka sasa taasisi kama United Nations for International Criminal Tribunal (UNMICT), African Union Advisory Board on Corruption (AUABC), African Institute of International Law (AIIL) na African Court on Human and Peoples' Rights (ACHPR) zinatarajiwa kuwa na ofisi katika jengo hilo.

Pamoja na ziara hiyo, Balozi Luvanda alipata fursa ya kushiriki kwenye uzinduzi wa mnara wa amani (The Arusha Peace Park Monument), tarehe 30/12/2015 mnara ambao  umejengwa  na ICTR kama kumbukumbu ya kudumu kufuatia kuhitimisha shughuli zake jijini Arusha.

Wednesday, December 2, 2015

MHE. BALOZI WILSON M. MASILINGI AKUTANA NA BI. CATHY BYRNE, MKURUGENZI MWANDAMIZI WA MASUALA YA AFRIKA, IKULU YA MAREKANI (WHITE HOUSE) TAREHE 30 NOVEMBA 2015

Mhe. Balozi Masilingi (kulia) ametembelea ofisi ya Bi. Cathy Byrne, Mkurugenzi Mwandamizi wa masuala ya Afrika katika Ikulu ya Marekani (White House). Katika maongezI yao, Bi. Cathy Byrne alimueleza Mhe. Balozi Masilingi jinsi Serikali ya Marekani inavyoridhishwa na mahusiano mazuri baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Marekani. Pia alieleza kuhusu serikali ya Marekani kuridhishwa na hatua za serikali ya Tanzania, katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.
 Mhe. Balozi Masilingi amemhakikishia mwenyeji wake kuwa ataendeleza mashirikiano mazuri sana yaliyopo kati ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Marekani kwa njia ya diplomasia ya uchumi yenye lengo la kuhamasisha biashara na uwekezaji nchini Tanzania.

==============================
Mhe. Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, akifuatana na Bw. Paul Mwafongo alihudhuria mkutano na Bw. Louis Rene Peter Larose, Mkurugenzi Mtendaji, Benki ya Dunia, Kundi la Nchi za Afrika. 

Wengine waliohudhuria ni pamoja na Bw. Andrew Ndaamunhu Bvumbe, Mkurugenzi Mtendaji Mbadala Benki ya Dunia, Kanda ya Afrika, na Bw. WilsonToninga Banda, Mshauri, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji.

Shabaha ya Mkutano ilikuwa ni kufuatilia mazungumzo yaliyofanyika Lima, Peru kuhusu kuimarisha ushirikiano kwa maslahi ya Afrika. 

Mhe. Balozi Masilingi alishukuru Benki ya Dunia kwa ushirikiano mzuri uliopo na kwa misaada na mikopo wanayotoa kuunga mkono juhudi za kujenga uchumi na kufanikisha mipango ya maendeleo kwa manufaa ya Watanzania wote. 

Aidha aliwahakikishia ushirikiano muda wote atakapokuwa katika kutekeleza wajibu wake wa kazi kwa maslahi ya Taifa. Mkurugenzi Mtendaji Benki ya Dunia, Kanda la Afrika, Bw. Louis Larose, alieleza kwa upande wake kuridhirishwa kwake na ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Benki ya Dunia. 

Aidha Bw. Larose aliipongeza Tanzania kwa kufanikisha Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba , 2015 kwamba ulikuwa huru na wa haki. Pia, alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John P. Magufuli kwa ushindi na kwa juhudi zake katika kuangalia udhibiti wa ukusanyaji wa mapato ya serikali na kuziba mianya ya uvujaji wa mapatao ili zipatikane fedha kwa ajili ya kusukuma maendeleo ya Watanzania. 

 Mkurugenzi Mtendaji aliahidi kwamba Benki ya Dunia iko tayari kutoa msaada wowote wa haraka utakaohitajika na kuombwa na Serikali ya Tanzania ili kufanikisha mpango wa kukusanya mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza program za maendeleo na huduma za serikali. 

 Bw. Larose, alimdokeza Mhe. Balozi kwamba Benki ya Dunia itaandaa siku maalumu mjini Washington, D.C. kwa ajili ya kuitangaza Tanzania na vivutio vyake nchini Marekani na kuomba kwamba Benki ya Dunia itamwalika Mhe. Balozi kuzindua siku hiyo. Akijibu hoja hiyo Mhe. Balozi alikubali mwaliko huo.

Tuesday, December 1, 2015

Balozi wa Afrika Kusini nchini amtembelea Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Afrika Kusini hapa nchini Mhe. Thamsanga Dennis Mseleku katika mazungumzo yaliyolenga kuboresha mahusiano mema na ya muda mrefu baina ya nchi hizo mbili.  
Balozi Thamsanga Dennis Mseleku, akisisitiza jambo kwa Katibu Mkuu Balozi Mulamula.
Mazungumzo yakiendelea huku Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), Bw. Merdard Ngaiza, Afisa Mambo ya Nje (katikati) pamoja na Afisa Habari wa Mambo ya Nje, Bw. Ally Kondo wakifuatilia mazungumzo hayo.
    
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akiagana na Balozi wa    Afrika Kusini hapa nchini Mhe. Thamsanga Dennis Mseleku,           baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Wizarani tarehe 01/12/2015.
                         =========================
                           Picha na Reuben Mchome.