Tuesday, May 30, 2017

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga amewasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2017/2018 mbele ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Waziri Mahiga katika hotuba yake aliliomba Bunge kupitisha kiasi cha shilingi150,845,419,000 ambapo katika kiasi hiki cha fedha shilingi142,845,419,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi 8,000,000,000 imetengwa kwa ajili ya bajeti ya maendeleo.

Bajeti hii ya mwaka 2017/2018 pamoja na mambo mengine imepanga kutekeleza malengo makuu muhimu kulingana na majukumu ya Wizara kama ifuatavyo;
  • Kutangaza mazingira mazuri ya nchi yetu kwa ajili ya uwekezaji kutokana na historia yake ya miaka mingi ya amani, umoja, utulivu na mshikamano wa kitaifa;
  • Kuendelea kufuatilia utekelezaji wa ahadi mbalimbali zilizotolewa kwa nchi yetu na nchi wahisani, mashirika ya kikanda na ya kimataifa katika kusaidia utekelezaji wa mipango yetu ya maendeleo;
  •  Kuendelea kuratibu Wizara, Idara na Taasisi nyingine za Serikali katika kuvutia wawekezaji na watalii, kutafuta nafasi za masomo, ajira na nafasi za kubadilishana uzoefu na kutafuta masoko; 
  • Kusimamia, kufuatilia na kuratibu utekelezaji wa mikataba mbalimbali iliyosainiwa kati ya nchi yetu na nchi nyingine na ile ya mashirika ya kikanda na kimataifa;
  • Kufuatilia utekelezaji wa maelekezo ya viongozi mbalimbali wa kitaifa;
  • Kuendelea kusimamia balozi zetu katika kutekeleza majukumu ya uratibu hasa kutafuta wawekezaji, fursa za ajira, nafasi za masomo na masoko kwa bidhaa zetu;

  • Kuendelea kufuatilia kwa karibu mageuzi kwenye taasisi za Umoja wa Mataifa kama vile Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Baraza la Kiuchumi na Kijamii, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na utekelezaji wa Malengo Endelevu ya Maendeleo;
  • Kuongeza uwakilishi wetu nje kwa kufungua Balozi mpya na Konseli Kuu na kuendelea kununua, kujenga na kukarabati majengo kwa ajili ya makazi na ofisi za Balozi kwa kadri hali ya fedha itakavyoruhusu; 
  • Kujenga mahusiano ya kirafiki na ushirikiano wa kiuchumi kati yetu na vyombo mbalimbali vya Kikanda na Kimataifa, unaozingatia maslahi ya Taifa letu; 
  • Kuendelea kutetea na kusimamia maslahi ya nchi maskini kwenye mikutano yote mikubwa na hasa ile ya Umoja wa Mataifa na taasisi zake. Vilevile, tutaendelea kufanya mazungumzo na nchi tajiri duniani ili kuhakikisha zinatekeleza ahadi mbalimbali zilizotoa ili kuharakisha maendeleo ya nchi maskini. Kwa mfano, ahadi za G8 na ile ahadi ya kila nchi tajiri kutoa asilimia 0.7 ya pato lake la Taifa kwa nchi zinazoendelea na kutoa asilimia 0.2 ya pato lake kwa nchi maskini sana duniani kama msaada; 
  • Kuendelea kutambua jumuiya za watanzania wanaoishi ughaibuni na kuweka utaratibu utakaowawezesha kuchangia maendeleo ya taifa; 
  • Kuratibu maandalizi na kushiriki kwenye majadiliano katika mikutano ya Viongozi Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mabaraza ya Kisekta ya Mawaziri ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na mikutano ya Vikundi Kazi na Wataalam; 
  • Kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mabaraza ya Kisekta ya Mawaziri ya Afrika Mashariki, miradi na programu za Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  • Kuratibu utekelezaji wa Mpango Kazi wa miaka kumi wa Umoja wa Fedha katika kuelekea kwenye eneo la Sarafu Moja ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  • Kuratibu zoezi la mapitio ya Sheria za Tanzania ili kuwezesha Watanzania kunufaika na utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki;
  • Kuratibu majadiliano na kusimamia utekelezaji wa makubaliano ya kuanzisha Eneo Huru la Biashara baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na COMESA na SADC pamoja na Eneo Huru la Biashara la Afrika; 
  • Kuratibu majadiliano kuhusu maeneo ya ushirikiano katika uendelezaji wa miundombinu ya kiuchumi (reli, barabara, bandari, nishati, viwanja vya ndege na hali ya hewa) na kijamii (elimu, afya, mazingira, jinsia na watoto) katika Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  • Kuratibu uondoaji wa Vikwazo Visivyo vya Kiforodha katika biashara baina ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  • Kuratibu ushiriki wa Tanzania katika Mikutano ya Bunge la Afrika Mashariki;
  • Kuratibu na kushiriki katika maandalizi ya Rasimu ya Katiba ya Shirikisho la Kisiasa la Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuzingatia mfumo wa Confederation; 
  • Kuratibu na kushiriki katika majadiliano ya kuanzisha Baraza la Usalama la Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  • Kuratibu na kushiriki katika majadiliano ya Mkataba wa Ulinzi wa Pamoja wa Afrika Mashariki; 
  • Kuratibu na kushiriki katika majadiliano ya kuanzisha Itifaki ya Utawala Bora ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Itifaki ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  • Kutoa Elimu kwa Umma juu ya fursa zitokanazo na mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki; 
  •  Kuratibu mapitio, utafiti, ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki;
  • Kuratibu na kufanya uchambuzi wa utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Taasisi ya TradeMark East Africa Wizarani, Wizara nyingine, Idara, Taasisi za Serikali na sekta binafsi; na 
  • Kukamilisha kuandaa Sera Mpya ya Mambo ya Nje 
Hotuba ya makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/2018  mara baada ya kuwasiliswa ilijadiliwa na kuchangiwa na Wabunge mbalimbali na hatimaye kupitishwa na Bunge hilo.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Philip Mahiga  (Mb) akiwasilisha hotuba ya bajeti ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Bungeni mjini Dodoma


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba (Mb) akijibu hoja mbalimbali za Wabunge wakati wa Kikao cha Bunge baada ya kuwasilishwa kwa bajeti ya Wizara Mjini Dodoma.

Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi mbalimbali nchini wakifuatilia uwasilishwaji wa Hotuba ya Makadirio ya  Bajeti ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bungeni mjini Dodoma

Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga akifurahia jambo na Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Peter Msigwa mara baada ya kuwasilisha hotuba ya bajeti Bungeni mjini Dodoma

Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga, Naibu Waziri Dkt. Susan Kolimba, Katibu Mkuu  Balozi Dkt. Aziz Mlima na Waziri Kivuli wa Wizara Mhe. Msigwa wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi na baadhi ya Wabunge.

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga na Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima wakishirikishana jambo baada ya kuwasilisha hotuba ya Madirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2017/2018 katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma

Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga akijibu hoja za wa Bunge Bungeni.


Waziri Mhe.Dkt. Mahiga na Naibu Waziri Mhe.Dkt. Susan Kolimba wakiwa katika picha ya pamoja na Watendaji mbalimbali wa Wizara mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara Bungeni Mjini Dodoma

 HOTUBA YA MHESHIMIWA BALOZI DKT. AUGUSTINE PHILIP MAHIGA (MB), WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA BAJETI YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA
 FEDHA 2017/2018

Sunday, May 28, 2017

Intentanational Community Applauds Tanzania’s Leadership of SADC Organ

Ambassador Mahiga in conversation with the United States Ambassador to the Kingdom of Lesotho H.E. Matthew T. Harrington after launching SEOM at AVANI Hotel in Maseru Lesotho. 

Ambassador Mahiga flagged with SADC Secretariat together with members of SADC Organ with all SADC Elections Observation Mission in a group photo. SADC has deployed about 40 observers from 9 member states in this year's election. 
Head of SADC Elections Observation Mission in Lesotho and Chairperson of the Ministerial Committee of the Organ Amb. Dr. Augustine Mahiga, delivering his statement during the launch of the mission recently in Maseru Lesotho.


    PRESS RELEASE
INTERNATIONAL COMMUNITY APPLAUDS TANZANIA’s LEADERSHIP OF SADC ORGAN AND EFFORTS TO STABILIZE POLITICAL SITUATION IN LESOTHO
Tanzania’s President Dr. John Pombe Magufuli has been applauded by the international community for his impeccable leadership of the SADC organ on politics, defense and security cooperation at this juncture when the community is ushering Lesotho into yet another National Parliamentary Election, the third within five years. 
Representatives from international organizations operating within SADC region and Lesotho in particular including the United Nations and European Union have commended SADC urgent call to the incoming government for serious structural and constitutional reforms. 
During the recent launch of SADC Electoral Observation Mission (SEOM) in Lesotho held in Maseru, Hon. Dr. Augustine Mahiga, Tanzania’s foreign Minister, Chairperson of the Ministerial Committee of the Organ and mission head reiterated SADC ‘s earlier mandate to the current government to undertake reforms in order to stabilize its political system and avoid a repeat of previous political crises. 
While commending political parties for signing pledges to accept election results and Independent Electoral Commission of Lesotho (IEC) for its preparedness for the upcoming national elections, Ambassador Mahiga sends a strong message to Lesotho,
“After three elections within less than five years the fatigued voters deserve a different and durable outcome. SADC will definitely take these pledges and commitments seriously in supporting the reform process in the Kingdom of Lesotho by the next government” said Ambassador Mahiga
Briefing members of SADC Secretariat before the launch, Amb. Mahiga said that it is upon SADC that leaders of the next government of Lesotho be held accountable to carry out the reforms. 
“Presedent Magufuli, our Chair of the Organ has given me clear instructions that we must work hard, together, and to make sure that this time around we are successful. The people of Lesotho have great expectations on us as SADC, let us not disappoint them” he remarked. 
Similar message was shared at the launch with all stakeholders about the commitment of President Magufuli, to stabilize political situation in the Mountain Kingdom as well as in the SADC region. He said that the work of SADC mission in the country was mandated by President Magufuli and that several groups have been working tirelessly since April 2017 in Lesotho. Based on their observation and preliminary work, SADC is still of the view that major reforms are needed in the country and not just national elections.
“It is evident from our extended presence on the ground in the Kingdom of Lesotho that the resolution of the political and security problems is not entirely predicated upon the elections and its outcomes, Clearly, there has to be stronger and time-bound commitment to broader reforms in the political, security and public sectors in order to stabilize the country” he added. 
As Tanzania is about to finish its term as the head of this important organ of the community, Ambassador Mahiga said he is simply executing President Magufuli’s vision in Tanzania’s engagements in regional integration bodies. He said that Tanzania is of the view that SADC is stronger when there is integration and cooperation. But SADC cannot make full progress if one member is in political crisis. Three elections within five years do not just bring fatigue to voters, it disorient the badly-needed work force, preventing them to contribute effectively to daily economic activities but it also dwindle much-needed resources for the government. 
In his speech, Ambassador Mahiga reminded the audience that as the continent celebrates fifty plus years of the African Unity, it is mind-boggling for Lesotho to still be pre-occupied with the basics of forming a stable government. 
“Allow me to add that it is strange paradox indeed that on this 25th day of May, 2017 marking the historical occasion of the Commemoration of the founding of the Organisation of African Unity; when we should ordinarily be celebrating milestones in the advancement of our societies and the consolidation of our democratic institutions; we are still locked in protracted debates on the basic requirements of forming and stabilizing governments”.
Commenting on SADC engagement in Lesotho, United Nations Development Program Deputy Resident Representative in Lesotho Ms. Christy Ahenkora said SADC intervention and follow up was badly needed for Lesotho to carry out reforms which will stabilize its political set up focusing on how coalition government should operate. 
Similarly, the Head of the European Union Delegation in Lesotho noted with keen interest the strong message from Ambassador Mahiga during the lunch of the mission and commended the organization for playing its part in Lesotho. The delegation has not brought in observers this time around, but it will deploy EUPlus Diplomatic Watch of 42 officials. 
An applaud was also given to Tanzania and SADC Mission by the American Ambassador to the Kingdom of Lesotho immediately after Hon. Mahiga's statement saying that candid observation by SEOM and deliberate efforts by SADC in Lesotho will bring about well-built democratic institutions and organization in the region.

ENDS

Issued by:
Government Communication Unit, 
Ministry of Foreign Affairs and East African Community, Maseru, Lesotho, 
May 28, 2017















Waziri Mahiga aongoza kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga leo ameongoza kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti ya Wizara. Hotuba hiyo inatarajiwa kuwasilishwa Bungeni hapo kesho tarehe 29 Mei, 2017.

Kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma katika ukumbi mikutano wa jengo la Hazina pia kimehudhuriwa  na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Susan Kolimba, Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz Mlima Wakurugenzi ,Wakuu wa Vitengo na baadhi ya Maafisa wa Wizara.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Naibu Mhe. Dkt. Susan Kolimba wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu Balozi Dkt.Aziz Mlima.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na  Naibu Waziri Mhe.Dkt.Susan Kolimba wakishirikishana jambo wakati wa Kikao cha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti ya Wizara.

Mhasibu Mkuu wa Wizara Bw. Paul Kabale akichangia jambo wakati wa kikao

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akichangia jambo wakati wa kikao

Kaimu Mkurugenzi  wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Bernard Haule (kulia) akichangia jambo wakati wa kikao

Wajumbe wakiwa katika kikao

Friday, May 26, 2017

Waziri Mahiga Azindua Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi ya SADC na Ujumbe Mzito Lesotho




Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), imesisitiza kuwa wapiga kura wa Lesotho wanatarajia kuwa Serikali itakayochaguliwa na wananchi kwenye Uchaguzi Mkuu wa Wabunge wa mwaka 2017 itasimamia na kutekeleza mageuzi yanayohitajika nchini humo. 

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi ya SADC, Kiongozi wa Timu hiyo Balozi Dkt. Augustine Mahiga alisema japo mazingira ya upigaji kura yameandaliwa na kukamilika, lakini huu ni uchaguzi wa tatu ndani ya miaka mitano na wapiga kura wamechoka. Ni matumaini ya SADC na ya wananchi wa Lesotho kuwa Serikali ijayo itajipanga vizuri na kusimamia kikamilifu mageuzi ya kikatiba na kimfumo ambayo yataleta uimara wa kisiasa na unaotabirika nchini humo.



"Jumuiya yetu imejiwekea misingi imara ya kidemokrasia ambayo ikijumuishwa na ile ya nchi, na kimataifa kama Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa tunapata vigezo tisa ambavyo timu yetu itaviangalia wakati huu wa uchaguzi" alisema Balozi Mahiga.



Baadhi ya vigezo vitakavyoangaliwa kwenye uchaguzi huo ni ushiriki wa wananchi kwenye michakato ya siasa, fursa sawa kwa vyama vyote vya siasa, uhuru wa taasisi zinazosimamia uchaguzi, elimu ya mpiga kura na wajibu wa wagombea na vyama vya siasa kukubaliana na matokeo kama yatakavyotangazwa na tume huru ya uchaguzi kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za nchi husika.



Wadau mbali mbali waliohudhuria hafla hiyo wakiwemo Viongozi wa vyama vya Siasa na Jumuiya ya Diplomasia nchini Lesotho, walielezwa kuwa SADC imepongeza hatua ya vyama vya siasa kuweka makubaliano yaliyosainiwa na Viongozi wa vyama kukubali matokeo ya uchuguzi iliyoratibiwa na Umoja wa Makanisa Lesotho.



Uchaguzi Mkuu wa Wabunge nchini Lesotho unatarajiwa kufanyika tarehe 3 Juni 2017 ambapo Chama au Muungano wa Vyama vyenye ushindi mkubwa wa viti vya ubunge, wataunda Serikali ambayo itaingozwa na Waziri Mkuu.


-Mwisho-



Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Maseru, Lesotho 26 Mei, 2017





Wizara ya Mambo ya Nje yawazawadia watumishi walionyesha utendaji bora

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima (wa kwanza kulia), akimkabidhi zawadi Afisa Mambo ya Nje, Bi. Eva Ng'itu kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa. Bi. Ng'itu amekuwa Mfakazi Hodari wa wa Wizara ya Mambo ya Nje kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
Dkt. Mlima aliwapongeza na kuwasihi wafanyakazi waliofanya vizuri kuwa zawadi walizokabidhiwa iwe chachu ya kuongeza juhudi na ufanisi katika utumishi wao.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akimpongeza  Bi. Ng'itu kwa kuwa mfanyakazi Hodari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Bw. Mohammed Kheri kutoka Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar akipokea zawadi yake kwa kuwa mfanyakazi bora wa Idara hiyo.
 Bw.Joseph Mlingi akipokea zawadi kwa kuwa mfanyakazi bora kwa upande wa madereva wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Bw. Emannuel Luangisa akipokea zawadi yake ya kuwa mfanyakazi bora wa Idara ya Asia na Australasia.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora na Mratibu wa Mafunzo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Tagie Daisy Mwakawago naye akipokea zawadi ya ufanyakazi bora wa Idara ya Diaspora
Bi Eva Kaluwa kutoka Idara ya Sera na Mipango akipokea zawadi yake kutoka kwa Dkt. Mlima.
Bi. Kisa Mwaseba akipokea zawadi ya Mfanyakazi bora wa Idara ya Mashariki ya Kati.
Bi. Upendo Mwasha akipokea zawadi ya mfanyakazi bora wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda.
Bi. Nelusigwe kutoka Kitengo cha Ununuzi na Ugavi akipokea zawadi baada ya kuibuka mfanyajkazi bora wa Kitengo hicho.
Bw. Erick Ngilangwa kutoka Idara ya Afrika akipokea zawadi ya mfanyakazi bora wa Idara hiyo
Afisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Rose Mbilinyi akipokea zawadi yake kutoka kwa Dkt. Mlima.
Katibu Mkuu Dkt. Mlima akizungumza katika kikao cha  baraza la wafanyakazi la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Mambo ya Nje, Zanzibar akichangia jambo katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza kwa makini Katibu mkuu alipo kuwa akizungumza nao
Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu, Dkt. Mlima na wafanyakazi bora kutoka kwenye Idara na Vitengo vya Wizara. Mwanamke pekee aliyeketi ni Bi. Eva Ng'itu ambaye ameibuka mfanyakazi hodari wa Wizara nzima kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Thursday, May 25, 2017

Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Mfalme Letsie wa III wa Lesotho


 Mkuu wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akisalimiana na Mfalme Letsie wa III wa Falme ya Lesotho, alipo kutana nae na kufanya mazungumzo.  


Waziri Mahiga akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na Mfalme Letsie wa III, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Balozi Innocent Shiyo.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Waziri Mahiga afanya mazungumzo na Mfalme Letsie wa III kuelekea Uchaguzi wa Mkuu wa Lesotho



Mkuu wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Mhe. Dkt. Augustine Mahiga amemhakikishia Mfalme Letsie wa III wa Lesotho kuwa Asasi ya Ushirikiano ya SADC ya Siasa, Ulinzi na Usalama imethibitisha pasipo mashaka utayari wa wapiga kura wa nchi hiyo kupiga kura siku ya Jumamosi tarehe 3 Juni 2017.



Hayo yamesemwa kwenye mazungumzo ya viongozi hao ambapo Mhe. Dkt. Mahiga alimuelezea Mtukufu Mfalme Letsie wa III, hatua mbalimbali za uangalizi wa uchaguzi zilizochukuliwa na Jumuiya ya SADC tangu alipofika nchini Lesotho. Jumuiya hiyo mbali na kupeleka waangalizi 41 wa uchaguzi kutoka kwenye nchi tisa wanachama, pia ina wajumbe wawili wa Baraza la Ushauri wa Masuala ya Uchaguzi ambapo mmoja wa wajumbe hao ni Jaji Mstaafu John Tendwa wa Tanzania.



Mhe. Mahiga pia alisifu jitihada za Serikali na Tume Huru ya Uchaguzi ya Lesotho ambao kwa pamoja wamehakikisha kuwa mazingira mazuri yameandaliwa yatakayoruhusu uchaguzi mkuu wa mwaka huu kufanyika kama ilivyopangwa.



Kwenye mazungumzo yao, Mhe. Mahiga alitumia pia nafasi hiyo kumpelekea Mfalme Letsie salaam za heshima kutoka kwa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano ya SADC ya Siasa, Ulinzi na Usalama ambayo inaundwa na nchi za Tanzania, Msumbiji na Angola kwa sasa.



Kwa upande wake, Mtukufu Mfalme Letsie wa III wa Falme ya Lesotho alimshukuru Mhe. Rais Magufuli  kama kiongozi wa asasi hiyo muhimu ya Jumuiya ya SADC na kuongeza kuwa ni matarajio yake kuwa chini ya uongozi wake makini na mahiri, nchi wanachama wa Jumuiya watatekeleza kwa ufanisi majukumu yao muhimu ya kuendeleza jumuiya.



Mfalme huyo mrithi wa baba yake Mfalme Moshoeshoe wa II anayetawala Lesotho tangu mwaka 1996 kama Falme ya Kikatiba, alisema anaiheshimu sana Tanzania kwa mchango mkubwa kwa nchi hiyo hususan kwenye kuendeleza taaluma mbalimbali nchini humo. Alisema kwa miaka mingi sasa wataalamu wa masuala ya afya na elimu kutoka Tanzania wameendelea kufanya kazi Lesotho na kuongeza kuwa hata yeye binafsi alifundishwa Chuo Kikuu cha Lesotho na Mtanzania masomo ya Sheria na Sayansi ya Siasa.

Mtukufu Mfalme Letsie alimaliza kwa kuahidi kuendeleza ushirikiano wa karibu uliopo baina ya Lesotho na Tanzania ambapo chimbuko lake ni kuwa nchi zote mbili ni wanachama waanzilishi wa Jumuiya ya SADC. Aidha alionesha nia kubwa ya kuzuru Tanzania siku za usoni, na kumuomba Mhe. Dkt. Mahiga, kufikisha salamu za heshima na ushirikiano kwa Rais na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 



 -Mwisho-



Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Maseru, Lesotho 25 Mei, 2017


Wednesday, May 24, 2017

Waziri Mahiga Aongoza Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa SADC nchini Lesotho

Dr. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrioka Mashariki na Mkuu wa Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa SADC akizungumza na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi ya Lesotho, Mhe. Jaji Mstaafu Lesao Lehohla   (wa pili kutoka kulia) alipotembelea tume hiyo mjini Maseru Lesotho kabla ya kuzindua rasmi Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi ya SADC.
Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Mkuu wa Umoja wa Makanisa wa Lesotho Archbishopp Gerald Tlali Lerotholi na ujumbe wake alipotembelea ujumbe huo kusikiliza maoni yao kuhusu uchaguzi mkuu nchini humo unaotarajiwa kufanyika tarehe 3 Juni 2017.
Dkt. Mahiga na ujumbe wake wakikamilisha majumuisho ya mikutano mbalimbali waliyoifanyana na wadau .
5: Dkt Mahiga akiagana na wenyeji wake nje ya Tume Huru ya Uchaguzi.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri Mahiga Aongoza Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa SADC nchini Lesotho



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, amezihimiza taasisi za Serikali na za dini nchini Lesotho kudumisha amani na usalama kwenye kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi mkuu nchini hapa ili kuwezesha Serikali itakayoingia madarakani kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kwa ajili ya wananchi wa Lesotho.



Uchaguzi huo mkuu wa wabunge ambao ni wa tatu kufanyika ndani ya kipindi cha miaka mitano, unatarajiwa kufanyika tarehe 3 Juni 2017 ambapo vyama 26 kati ya 30 vilivyojiandikisha, vitashiriki kwenye kinyang’anyiro hicho cha kuchagua wawakilishi Bungeni.



Kwa mujibu wa Katiba ya Falme ya Lesotho, kiongozi wa chama kitakachoshinda viti vingi zaidi vya ubunge kwenye uchaguzi huo ndiye  atakayeapishwa kuwa Waziri Mkuu na Kiongozi wa Serikali, ambapo mkuu wa nchi na mtawala mkuu anaendelea kuwa Mfalme Letsie III.



“Wakati umefika sasa kwa Jumuiya yetu ya SADC kushiriki kwenye uangalizi wa uchaguzi huu tukiwa na habari njema ya kurejesha matumaini kwa wananchi kuhusu mustakabali wa uongozi. Lakini pia tuwe na ujumbe mzito kwa Serikali ijayo ili iweze kufanya mageuzi ya kweli kwenye nyanja mbalimbali kwa manufaa ya wananchi” Mhe. Mahiga amehimiza kwa wajumbe wa timu ya waangalizi wa uchaguzi.



Tangu alipowasili nchini hapa tarehe 22 Mei 2017, Dkt. Mahiga na ujumbe wake wamekutana na wadau mbalimbali wakiwemo Tume Huru ya Uchaguzi ya Lesotho na Umoja ya Makanisa wa Lesotho kwa lengo la kupata maoni ya kina kabla ya kuzindua Timu ya Uangalizi ya SADC (SADC Elections Observersion Mission - SEOM) tarehe 25 Mei 2017.



Mhe. Dkt. Mahiga anaongoza timu hii ya waangalizi wa uchaguzi ya SADC kwasababu kwa sasa Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Organ).



Akiongoza mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa Lesotho Mhe. Mampono Khaketla, Mhe. Mahiga alipongeza jitihada za Serikali kuhakikisha kuwa usalama wa raia  na amani vinatawala nchini humo wakati wa uchaguzi. Hata hivyo aliongeza kuwa yeye na ujumbe mzima wa asasi hiyo muhimu ya maamuzi ya SADC ipo Lesotho kwa mara ya tatu, kama waangalizi wa uchaguzi ambapo mara ya kwanza na ya pili ilikuwa uchaguzi wa mwaka 2012 na 2015.



Alisema ni matarajio yake na ujumbe mzima kuwa uchaguzi wa mwaka huu utazaa matunda yatakayoleta matumaini kwa wananchi ya kuwa na Serikali imara itakoyoongoza na kusimamia mageuzi ya kweli. “Haya ni matumaini ya wananchi wa nchi hii, na mimi kama  kiongozi wa SEOM nimekuja kuwahakikishia ndugu zangu, tutasimama pamoja nanyi, tutawasindikiza kwenye uchaguzi huu, kama misingi ya Jumuiya yetu inavyoelekeza lakini pia wananchi wanatarajia hayo”



Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi ya SADC imewasili nchini Lesotho tarehe 18 Mei, 2017 na inaundwa na nchi tisa ambazo ni wananchama wa Jumuiya hiyo. Wajumbe wapatao 41 watasambaa kwenye majimbo yote ya uchaguzi kama waangalizi na kutoa taarifa ya kina siku chache baada ya uchaguzi huo, kuhusu mwelekeo na mwenendo wa uchaguzi huo.



 -Mwisho-



Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Maseru, Lesotho 23 Mei, 2017