Friday, January 19, 2018

Rais Magufuli azungumza na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wa nne kutoka kushoto akiongea na wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam. Wengine katika picha kutoka kulia kwa Mhe. Rais ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga; Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba. Kutoka kushoto kwa Mhe. Rais ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Zanzibar, Mhe. Baloz Ali Karume; Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakisikiliza kwa makini maelekezo na maagizo ya Mhe. Rais Magufuli. Mhe. Rais aliagiza Wizara iongeze nguvu katika kuratibu masuala ya kimataifa kati yake na Wizara/taasisi za kisekta ili kusiwe na ucheleweshwaji wa utekelezaji wa masuala mbalimbali ikwemo uwekezaji, biashara, utalii na huduma za kijamii kama afya na elimu.

Watumishi wakiendelea kumsikiliza Mhe. Rais Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisisitiza jambo katika kikao hicho.
Mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bibi Helen Maduhu akichangia jambo katika kikao hicho. Mhe. Rais aliwataka watumishi wabainishe bila woga changamoto zote zinazowakabili ili kwa pamoja wajadili namna ya kuzipatia ufumbuzi.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akichangia hoja zitakazosaidia kuboresha utendaji wa Serikali ili malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano yaweze kufikiwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiagana na watumishi wa Wizara baada ya kikao kumalizika. Katika picha ni Katibu Mtendaji wa APRM Tanzania, Bibi Rehema Twalibu akiagana na Mhe. Rais Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akifurahi jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Afrika, Balozi Grace Mujuma.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akiagana na Mhe. Rais Magufuli.


Watumishi wakiendelea kuagana na Mhe. Rais, pichani ni Bw. Ally Kondo naye akishikana mikono na Mhe. Rais.

Thursday, January 18, 2018

Tanzania yawa mwenyeji wa Mkutano wa pili wa India - Afrika

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa hotuba ya ufunguzi katika Mkutano wa pili wa India - Afrika uliofanyika katika ofisi za ubalozi wa India nchini Jijini Dar es Salaa tarehe 18 Januari 2017.

Mkutano huo wa siku mbili unatarajiwa kumalizika tarehe 19 Januari 2018 ambapo umewakutanisha  wajumbe kutoka serikali ya India, wajumbe wa nchi wanachama wa Afrika Mashariki (EAC) na wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC) kwa lengo la kujadili masuala ya ushirikiano pamoja na kubuni maeneo mapya ya ushirikiano kwa manufaa ya wananchi wa India na wa jumuiya hizo 

Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya akihutubia ambapo alieleza pamoja na kujadili masuala ya ushirikiano Serikali ya India itatumia fursa ya Mkutano huo kukusanya maoni, taarifa na mapendekezo yatakayotolewa na wadau hususan katika masuala ya ulinzi, amani na maendeleo ili kila Taifa liweze kufikia malengo ya kitaifa na kuboresha maisha ya wananchi wake.

Waziri Mkuu Mstaafu, Dr. Salim Ahmed Salim akihutubia katika Mkutano huo ambapo alieleza kuwa India ni mfano wa Taifa kubwa linaloendeshwa kidemokrasia licha ya kuwa na idadi kubwa ya watu na hivyo akasisitiza ni muhimu kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na zile za Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika zikafata mfano huo ili ziweze kuruhusu shughuli za maendeleo kufanyika kwa amani na kuwaletea wananchi maendeleo.

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza linaloshughulikia masuala ya Ulimwengu nchini India, Bw. Nalin Surie akihutubia katika ufunguzi wa Mkutano huo ambapo alieleza India imejidhatiti katika kuhakikisha ushirikiano wake na mataifa ya Afrika unaimarika na kuwa wa manufaa kiuchumi huhusan kwa nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika.
Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Bernard Haule (wa pili toka kulia) pamoja na wajumbe wengine wakifuatilia Mkutano.


Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Stephen Mbundi na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Achiula wakifuatilia Mkutano. 

Sehemu ya wajumbe kutoka nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika wakifuatilia Mkutano.

Sehemu nyingine ya Wajumbe wakifuatilia Mkutano
Wajumbe wakishuhudia hafla ya ufunguzi wa Mkutano.

Waandishi wa Habari wakifanya mahojiano na Mhe. Waziri Mahiga mara baada ya hafla ya ufunguzi kumalizika.

Tanzania yashiriki maonesho ya utalii ya kimataifa nchini Uholanzi






Washiriki kutoka Tanzania wakiwa katika banda la Tanzania kwenye Maonesho maarufu ya Utalii ya Kimataifa (Vakantiebeurs 2018) yaliyofanyika hivi karibuni mjini Utrecht, Uholanzi.

Kutoka kushoto ni Bw. Willy Lyimo wa Bodi ya Utalii (TTB), Bibi Agnes Kiama Tengia, Afisa Ubalozi, Bw. Susuma Kusekwa wa Hifadhi za Taifa (TANAPA), Bw. John Sung’are wa African Wildcats Expeditions Ltd. (Arusha), Bibi Naomi Z. Mpemba, Kaimu Balozi wa Ubalozi wa Tanzania The Hague Uholanzi na Bw. Mushtaqali Abdalla wa Bobby Tours and Safaris (Arusha).

Kaimu Balozi Bibi Naomi Z. Mpemba akimsikiliza mteja aliyefika kwenye banda la Tanzania.

Bw. Iddi Mavura wa NCAA na Bw. Susuma Kusekwa wa TANAPA wakiwasiliza wateja waliofika kwenye banda la Tanzania katika Maonesho ya Utalii ya Kimataifa ya Vakantiebeurs 2018.

Bi. Sophia Tumsifu, Mtumishi wa Ubalozi akiwapa maelezo wateja waliofika katika banda la Tanzania ambapo pamoja na kupata taarifa kuhusu vivutio vya Tanzania, walipata pia ladha ya vyakula vya Tanzania.

Bibi Mwajuma Kitano, Mwanamuziki Mtanzania anayeishi Uholanzi, akiwa pamoja na wanafunzi wake ambao ni raia wa Uholanzi, kwa pamoja wakitumbuiza katika banda la Tanzania katika Maonesho ya Utalii ya Kimataifa ya Vakantiebeurs 2018.