Monday, July 23, 2018

SADCAS Job Vacancies Announcement.








The Southern African Development Community Accreditation Service (SADCAS), a multi economy Accreditation body based in Botswana was established to offer accreditation services throughout the SADC region in those Member States that do not have a national accreditation body namely: Angola, Botswana, Democratic Republic of Congo, Lesotho, Malawi, Mozambique, Namibia, Seychelles, Swaziland, Tanzania, Zambia and Zimbabwe.

The following TWO posts tenable in Gaborone are currently on offer:

(1) Program Coordinator for Calibration Laboratories Accreditation Scheme (ISO/IEC 17025) and Inspection Bodies Accreditation Scheme (ISO/IEC 17020)


Main Purpose of the Job
To provide support to the Technical Manager to ensure co-ordination of the Calibration Laboratories and Inspection Bodies Accreditation Schemes are undertaken efficiently in order to achieve the organization strategic targets

Key Responsibilities
· Manage all applications received under the Calibration Laboratories and Inspection Bodies Accreditation Schemes;
· Check technical details and perform document reviews for
new applications;
· Manage assessment teams;
· Confirm all logistics pertaining to assessments that have been arranged by the Administrator timeously i.e. accommodation,
assessment packs, travel logistics, etc;
· Conduct minimum assessments as required by the schemes
· Confirm technical correctness of accreditation schedules
agreed during assessments;
· Contribute to assessment and financial planning with the
Technical Manager;
· Assist in mentoring/monitoring of assessors and trainees
assessors;
· Manage the generation and maintenance of appropriate
documents for assigned areas of responsibility;
· Contribute in the implementation and realization of the
schemes, objectives and deadlines;
· Interact with various stakeholders and provide good client

·
 
services; and
Maintain personal development plan.
           
Qualification and Experience
· Diploma/ Degree in Physics/Mathematics/ Engineering
· Understanding of accreditation requirements and systems
based on ISO/IEC 17025 and ISO/IEC 17020.
· A minimum of 5 years technical experience with at least 2
years at managerial level.

Required Skills and Competencies · Target driven;

· Attention to detail;
· Ability to work in a team;
· Good organizational and time management skills;
· Excellent writing and verbal skills;
· Computer literate with specific experience in Microsoft Office; and
· Candidates with high proficiency in two of the SADC official
languages (English/Portuguese/French) encouraged to apply.

(2) Quality Manager

Main Purpose of the Job

To manage the SADCAS Quality Management System (QMS) and ensure that it complies with the requirements of ISO/IEC 17011 and of AFRAC, SADCA, ILAC and IAF in order to achieve and main-tain the international recognition of SADCAS.
Key Responsibilities
· Manage Internal Audit process as per SADCAS procedure;
· Manage Management Reviews meetings as per SADCAS procedure;
· Manage the preparation, approval, control, review and publication of QMS documents (procedures, forms, and standard letters) as per the SADCAS procedure;
· Ensure that relevant personnel are trained on ISO/IEC 17011
and SADCAS QMS documents;
· Coordinate the SADCAS Customer feedback system including
complaints as per the SADCAS procedure;
· Ensure that the external customer satisfaction survey is conducted on an ongoing basis;
· Manage and coordinate all activities related to SADCAS Peer
Evaluation’
· Maintain updated records of all personnel involved in SADCAS
assessments/decisions on accreditations; and
· Compile reports on complaints, customer satisfaction feedback,
trends in internal audit/peer evaluation findings etc.

Qualification and Experience
· A degree in a technical discipline;
· Understanding of accreditation bodies requirements and systems based on ISO/IEC 17011;
· Qualified and registered Lead/Technical Assessor;
· A minimum of 5 years technical experience with at least 2 years
at managerial level; and
· Peer evaluator training will be an added advantage;

Required Skills and Competencies 

· Target driven;
  • Attention to detail;
  • Ability to work in a team;
  • Good organizational and time management skills;
  •  Excellent writing and verbal skills;
  • Computer literature with specific experience in Microsoft Office; and
  • Candidates with high proficiency in two of the SADC official languages (English/Portuguese/ French) encouraged to apply.


SUBMISSION
Interested and suitably qualified candidates who are up for the challenge are encouraged to email a motivational letter, CV (maximum 3 Pages) and certified copies of qualifications to info@sadcas.org


CLOSING DATE: 30 July 2018

CORRESPONDENCE WILL BE LIMITED TO SHORTLISTED CANDIDATES ONLY.

Tanzania na Korea zakubaliana kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kibiashara

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania imeiomba Jamhuri ya Korea iendelee kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo Serikali ya awamu ya tano imeifanya kuwa ya kipaumbele katika kufikia azma ya uchumi wa viwanda.

Kauli hiyo ilitolewa leo Ikulu jijini Dar Es Salaam na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) mbele ya waandishi wa habari akiwa na mgeni wake, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea, Mhe. Lee Nak-yon.

Miradi ambayo Mhe. Waziri Mkuu aliitaja ni pamoja na ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi mkoani Mwanza lenye urefu wa mita 3200, barabara ya Chaya mkoani Tabora yenye urefu wa kilomita 42 na ujenzi wa barabara ya juu ya bahari kutoka ufukwe wa Coco, Osterbay hadi Aga Khan, Upanga jijini Dar Es Salaam yenye urefu wa kilomita zaidi ya sita. Miradi mingine ni ujenzi wa hospitali tano za rufaa katika kanda mbalimbali nchini na ujenzi wa reli ya kisasa ya kiwango cha kimataifa utakaotekelezwa kwa awamu tano ambapo awamu ya kwanza na ya pili kutoka Dar Es Salaam - Morogoro hadi Dodoma umeshaanza kwa kutumia Fedha za ndani.

Mhe. Majaliwa kabla ya kuzungumza na wana habari alikuwa na mazungumzo rasmi na mwenyeji wake na baadaye viongozi hao walishuhudia uwekaji saini wa Mkataba wa kuondoa hitaji la viza kwa wenye hati za kusafiria za kidiplomasia na utumishi baina ya Tanzania na Korea.

Mkataba huo kwa upande wa Tanzania ulisainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga na kwa upande wa Korea, Makamu wa Kwanza wa Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Lim Sung- Nam aliweka saini kwa niaba ya Serikali yake.

Katika ziara hiyo, Mhe. Lee pamoja na mambo mengine alitembelea Kituo cha Kutunzia kumbukumbu cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ambacho ujenzi wake ulitokana na mkopo wa masharti nafuu wa benki ya Exim ya Korea. Aidha, alitembelea hospitali ya Mnazi mmoja na kutoa msaada wa gari mbili za kubebea wagonjwa.

Wakati wa mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Mhe. Majaliwa alitumia fursa hiyo kuwakarabisha wafanyabiashara wa Korea kuja kuwekeza nchini katika sekta mbalimbali ikiwemo utalii.

Kuhusu utalii, Waziri Mkuu Majaliwa alieleza kuwa Korea imekubali kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kuhamasisha watalii wengi kutoka nchi hiyo kuvitembelea na kubainisha kuwa michoro ya tingatinga ambayo asili yake ni Tanzania inapendwa sana nchini humo.

Katika ziara hiyo, Mhe. Lee amefuatana na wafanyabiashara wakubwa ambao watafanya mkutano na wafanyabiashara wa Tanzania siku ya Jumatatu tarehe 23 Julai 2018 unaolenga kuangalia namna watakavyoweza kushirikiana katika uwekezaji kwenye sekta mbalimbali hapa nchini.

Mhe. Majaliwa alieleza kuwa Serikali ya Tanzania inasifu na kuunga mkono jitihada zinazofanywa kati ya Korea Kusini na Korea Kaskazini za kumaliza tofauti zao kupitia mazungumzo ya amani.

Alihitimisha kwa kuwahakikishia wananchi kuwa Korea inaridhishwa na jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano za kuinua uchumi wa Tanzania na kwamba nchi hiyo itaendelea kuunga mkono jitihada hizo. Aidha, Korea inasifu uwepo wa amani nchini na kuwasihi Watanzania waendelee kuitunza kwa kuwa ndio msingi wa maendeleo duniani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
22 Julai 2018


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Mgeni wake, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea, Mhe. Lee Nak-yon walipokutana kwa ajili ya kufanya mazungumzo jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga (kulia) na Makamu wa Kwanza wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Korea, Mhe. Lim Sung- Nam wakiweka saini Mkataba wa kuondoa hitaji la viza kwa wenye hati za kusafiria za kidiplomasia na utumishi wanaposafiri baina ya nchi hizo mbili. 

Sunday, July 22, 2018

Waziri Mkuu wa Korea atembelea NIDA na Hospitali ya Mnazi Mmoja

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola (Mb.) akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea Mhe. Lee Nak-Yon mara baada ya kuwasili kwenye kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kilichopo Kibaha. Kituo hicho kilijengwa kwa Mkopo wa masharti nafuu kutoka Korea kupitia Banki ya Exim.
Mhe. Nak-Yon akiweka saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye kituo hicho. 
Mhe. Nak-Yon (katikati) akisiliza maelezo ya namna kituo cha kutunzia kumbukumbu cha mamlaka ya vitambulisho vya taifa kinavyotekeleza majukumu yake. wengine katika picha wa pili kutoka kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Mhe. Augustine Mahiga (Mb.), Mhe. Lugola Balozi wa Korea nchini Mhe.Song Geum-young.


Maafisa wa vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanaendelea kutolewa kwa mgeni rasmi.
Juu na chini ni seemu ya ujumbe wa mhe. Nak-Yon pamoja na ujumbe kutoka Tanzania wakisikiliza maelezo yaliyokuwa yanatolewa.  
Mhe. Nak-Yon akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza ziara yake kwenye kituo hicho cha kuhifadhia kumbukumbu cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).



 *******Hospitali ya Mnazi Mmoja*******

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman(TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo (Mb.) akisalimiana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea Mhe. Lee Nak-Yon mara baada ya kuwasili kwenye Hospitali ya Mnazi Mmoja. Katika hospitali hiyo, Mhe. Waziri Mkuu alipata fursa za kutembelea wagonjwa na kujionea utendaji kazi kwenye hospitali hiyo. Aidha, alipewa nafasi ya kumchagulia jina mtoto aliyezaliwa siku chache zilizopita hospiyalini hapo. Mhe. Nak-Yon pia alikabidhi msaada wa Magari mawili ya kubebea wagonjwa kwenye hospitali hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam tarehe 22.07.2018.
Mhe. Jafo akimtambilisha kwa Waziri Mkuu, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema mara baada ya kuwasili hospitali ya Mnazi Mmoja. 
Mhe. Nak-Yon akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Madaktari wa Mmnazi mmoja kuhusu matumizi ya kifaa cha maabara.  
Mhe. Nak-Yon akisalimiana na wagonjwa waliokuwepo hospitalini hapo
Mhe. Nak-Yon akimkabidhi zawadi mmoja wa wamama aliyejifungua Mtoto wa kike ambaye mtoto wake alipewa jina Laura na Mwaziri Mkuu huyo.
Mhe. Nak-Yon akikabidhi msaada wa magari mawili ya kubebea wagonjwa kwa Mhe. Jafo mara baada ya kumaliza kuitembelea Hospitali hiyo.
Mhe. Nak-Yon akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria tukio la kukabidhiwa kwa magari hayo. 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea Mhe. LEE NAK-YON awasili nchini

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb.) akimsuburia mgeni wake Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea Mhe. Lee Nak-Yon akishuka kwenye ndege yake mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusi Nyerere jijini Dar es Salaam, Mhe. Nak - Yon yupo nchini kwa ziara ya siku tatu ambapo atafanya mkutano na mweyeji wake, kisha watasaini Mkataba wa kuondoa hitaji la Viza kwa watu wenye hati za kusafiria za kidiplomasia na za utumishi. Pia ataenda Ikulu kumsalimia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, atatembelea Makumbusho ya Taifa, Hospitali ya Mnazi Mmoja na Kituo cha utunzaji taarifa cha NIDA kilichopo Kibaha. 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Mkuu wa Korea Mhe. Nak-Yon mara baada ya kuwasili nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), naye akisalimiana na Waziri Nak-Yon mara baada ya kupokelewa na Mhe. Majaliwa, wa kwanza kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwele naye akisubiria kusalimiana na Waziri Mkuu wa Korea.
Mhe. Nak - Yon akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea Mhe. Matilda Masuka
Mhe. Majaliwa pamoja na mgeni wake Mhe. Nak - Yon  pamoja na Dkt. Mahiga wakitizama kikundi cha ngoma kilichoandaliwa kusherehesha kwenye mapokezi hayo 

Friday, July 20, 2018

Makatibu Wakuu Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Habari wakutana kwa kikao kazi

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kushoto) pamoja na mwenyekiti mwenza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Suzan Mlawi wakiongoza kikao kazi cha pamoja baina ya wizara hizo mbili kilichofanyika wizarani jijini Dodoma tarehe 20 Julai 2018.

Wakurugenzi na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakifuatilia kikao ambacho ni sehemu ya vikao vinavyofanywa na Wizara ya Mambo ya nje katika kuratibu na kufanya ufuatiliaji wa masuala mbalimbali ya kikanda na kimataifa yanayotekelezwa na sekta nyingine nchini.