Mkutano ukiendelea |
Monday, January 25, 2021
MHE. SAHLE-WORK ZEWDE, RAIS WA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA SHIRIKISHO LA ETHIOPIA KUFANYA ZIARA NCHINI
Friday, January 22, 2021
DKT. MWINYI: MAZINGIRA YA KISIASA ZANZIBAR YANATOA FURSA YA KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema
Zanzibar iko salama na mazingira ya kisiasa yanatoa fursa ya kuwaletea wananchi
wa Zanzibar maendeleo kutokana na uwepo wa Serikali ya umoja wa kitaifa.
Rais
Mwinyi ameyasema hayo Ikulu ya Zanzibar wakati alipokutana na ufanya mazungumzo
na uongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Palamagamba John Kabudi na kuongeza kuwa uongozi wake unajipanga kutimiza ahadi
alizotoa kwa wananchi.
Pia
Rais Mwinyi ameongeza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja
na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetoa kipaumbele katika kuimarisha Uchumi
wa Bahari kuu hasa Uchumi wa bluu kama chanzo mbadala cha mapato kitakachosaidia
kukuza uchumi na kupunguza mzigo wa kodi kwa wananchi.
“Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimetoa
kipaumbele katika kuimarisha Uchumi wa Bahari kuu hasa Uchumi wa bluu kama
chanzo mbadala cha mapato kitakachosaidia kukuza uchumi,” Amesema Dkt.
Mwinyi
Katika
tukio jingine, Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje umekutana na kufanya
mazungumzo na Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad ambaye amesisitiza kuwa uchumi wa bluu ni muhimu
sana kwa maendeleo ya Zanzibar hivyo ni muhimu kwa Serikali zote mbili
(Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania) kulinda mipaka yake ya bahari ambapo pia ulinzi huo utasaidia kuzuia
na kupambana na uingizwaji wa dawa za kulevya hapa nchini.
“Naamini
kabisa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tukishirikiana katika kuimarisha ulinzi wa baharini itasaidia
kupunguza uingizwaji wa dawa a kulevya hapa nchini,” Amesema Maalim Seif
Kwa
upande wake Prof. Palamagamba John Kabudi ameupongeza uongozi wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa kwa hatua ulizozichukua katika kuhakikisha uwepo wa
amani na utulivu visiwani humo na kwamba uwepo wa amani na utulivu utachangia
kuleta maendeleo haraka kwa wananchi wa Zanzibar.
“Zanzibar
imetulia na uchumi wake umezidi kuimarika sote ni mashahidi wa ongezeko la
watalii hapa Zanzibar hii ni ishara ya kuwa na amani na utulivu, na jambo hili
linachangia kukua kwa uchumi wa Zanzibar,” Amesema Prof. Kabudi
Mbali
na kukutana na Rais wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais, pia Uongozi huo
umekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ambapo wamejadili masuala
mbalimbali ya maendeleo yanayohusu Tanzania Bara na Zanzibar hususan yanayohusu
Muungano.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
Kabudi katika ziara yake ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. William Olenasha pamoja na Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiongea
na uongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Palamagamba John Kabudi (Mb) Ikulu Zanzibar wakati wa ziara ya kikazi ya Prof.
Kabudi Zanzibar. Prof. Kabudi ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. William Olenasha pamoja na Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiongea
na viongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, (hawapo pichani) katika Ikulu ya Zanzibar
Kikao
cha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali
Mwinyi na uongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, kikiendelea katika Ikulu ya Zanzibar
Makamu
wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Maalim Seif Sharif
Hamad akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Prof. Palamagamba John Kabudi wakati alipokuwa akimuelezea jambo wakati uongozi
wa Wizara ulipomtembelea Mhe. Seif kwa zaiara ya kikazi mjini Zanzibar
Kikao
cha Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad na uongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki kikiendelea katika Ikulu ya Zanzibar
BALOZI IBUGE AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR
Na Nelson Kessy, Zanzibar
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge akutana na kufanya mazungumzo na Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji katika Afisi za Mwanasheria Mkuu mjini Zanzibar
Mazungumzo
hayo yamelenga kuimarisha ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu ya kazi
baina Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Balozi
Ibuge amesema kuwa jukumu kubwa la watendaji wa Serikali hizi mbili ni
kuhakikisha wanatekeleza maono (vision) viongozi wakuu wa Serikali hasa kwa
kuzingatia maelekezo yaliyopo katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). “Ni
jukumu letu sisi kama watendaji wa serikali kuwasaidia viongozi wetu kutekeleza
maoni ya viongozi wetu kwa kuzingatia Ilani ya CCM ya 2020 – 2025,” Amesema
Balozi Ibuge.
Kwa upande wake Dkt. Mwinyi Talib Haji amemuahidi Balozi Ibuge kuwa wataendelea kushirikiana katika kuhakikisha kuwa malengo ya serikali zote mbili yanatekelezwa kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.
“Nakuahidi kuwa sisi kama
Afisi ya Mwanasheria Mkuu – Zanzibar tutashirikina na Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikino wa Afrika Mashariki katika kuhakikisha tunatekeleza majukumu ya
serikali,” Amesema Dkt. Haji.
Mwanansheria Mkuu wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji akimkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika Ofisi za Mwanasheria Mkuu Zanzibar leo
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge akisaini kitabu
cha wageni katika Ofisi za Mwanasheria Mkuu Zanzibar, kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Dkt. Mwinyi Talib Haji
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge akiongea na Mwanansheria
Mkuu wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji katika Ofisi za Mwanasheria Mkuu
Zanzibar
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji akimkabidhi moja ya zawadi Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge
Mwanasheria
Mkuu wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Talib Haji akiwa katika picha ya pamoja na Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mambo ya Nje –
Zanzibar Bw. Masoud Balozi Masoud (kushoto) pamoja na Msaidizi wa Katibu Mkuu
Bw. Hangi Mgaka (kulia).
Thursday, January 21, 2021
KAIMU KATIBU MKUU AKUTANA NA BALOZI WA VITNAM
Wednesday, January 20, 2021
Friday, January 15, 2021
BALOZI MBUNDI AONGOZA MAJADILIANO BAINA YA TANZANIA NA POLAND
Sehemu ya wajumbe wakifuatilia mazungumo |
Monday, January 11, 2021
RAIS NYUSI AWEKA JIWE LA MSINGI HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA - CHATO
Na Nelson Kessy, Chato
Rais
wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi amewasili nchini leo kwa ziara ya kikazi na
kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John
Pombe Magufuli katika uwanja wa ndege wa Geita - Chato na kisha kuweka jiwe la
msingi la ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Kanda- Chato.
Akizungunza
katika hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya Rufaa
ya Kanda-Chato, Rais Magufuli alimshukuru Rais Mhe. Filipe Nyusi kwa
kumtembelea Chato na kuongeza kuwa
Msumbiji ni rafiki wa muda mrefu wa Tanzania na nchi hizo zina makubaliano ya kushirikiana katika mambo
mbalimbali ikiwemo biashara na uwekezaji.
"Biashara
kati ya Tanzania na Msumbiji imeongezeka, hadi kufikia mwaka 2020 ilifikia
shilingi bilioni 93.6, kuna makampuni ya Msumbiji yanafanya kazi hapa na baadhi
ya makampuni ya Tanzania yanafanya kazi kule." Amesema Rais Magufuli.
Rais
Magufuli ameongeza kuwa Januari 9, 1967 Hayati Mwalimu Julius Nyerere
alitembelea Wilaya ya Chato na kufungua kiwanda cha pamba kilichojengwa kwa
shilingi milioni 2 ambacho kilikuwa na uwezo wa kuchakata marobota 20,000.
Aidha,
Rais Magufuli amesema kuwa Mwalimu Nyerere alichangisha fedha na yeye binafsi
kuchangia shilingi 2,000 kwa ajili ya kujenga bandari ya Nyamirembe ili iweze
kusafirisha pamba kwenda Mwanza na Dar es Salaam kwa hiyo wa Rais Nyusi amefika
eneo ambalo alifika Mwalimu Nyerere.
"Kwetu
sisi tunaona hii ni zawadi kubwa kwa wewe kuja kuzindua hospitali hii ambayo ni
kubwa na itahudumia pia nchi za jirani.Nawashukuru Wizara ya Afya na
Wakandarasi, nitawabana Wizara ya Afya
ili hospitali hii ikamilike mara moja." Alisema Rais Magufuli
Kwa
upande wake Rais Nyusi amempongeza Rais Magufuli kwa juhudim kubwa za
kushughulikia maisha ya wananchi wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha sekta pamoja
na huduma za afya nchini.
"Nashukuru
kwa Rais Magufuli kunipa nafasi ya kuweka jiwe la msingi kwa sababu Serikali
inayoaangalia afya za wananchi hiyo ni Serikali inayopenda wananchi wake. Rais
Magufuli anashughulikia sana maisha ya wananchi wa watanzania kwa kuangalia
nyumba bora za kuishi, huduma za maji, chakula
na afya bora" amesema Rais Nyusi.
"Kwa
hiyo hii ni zawadi kwetu kwa kutupa
nafasi ya kuweka jiwe la msingi katika hospitali hii kubwa, kule Msumbiji
tumeanza (Program ya presidential
initiatives) ya kujenga hospitali kila wilaya hii ni zawadi kubwa kwetu ya kutupa nafasi ya kuweka jiwe la msingi katika afya ya wananchi," Ameongeza Rais
Nyusi
Aidha,
Rais Nyusi amesema kuwa mkoa wa Geita ni
tajiri kwa kuwa kuna kilimo cha mpunga,
madini ya dhahabu na uvuvi wa
samaki, hivyo kuwataka wananchi wa mkoa huo kufanyakazi kwa bidii.
Naye,
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy
Gwajima amesema kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda -
Chato ilikadiriwa kutumia sh. bil.16, Serikali imeshatoa sh. bil.14 ambapo
ujenzi umekamilika kwa asilimia 90 na makabidhiano yanatarajiwa kufanyika mwezi
Machi, 2021.
Ameongeza
kuwa awamu ya pili ya ujenzi imeshaanza
kwa jumla ya gharama ya shilingi bilioni 14 ambapo mpaka sasa Serikali imetoa
shilingi bilioni 4.1 na utekelezaji wake umefikia asilimia 37.
"Hospitali
ya Rufaa ya Kanda - Chato itakapokamilika itakuwa na uwezo wa kuhudumia
wananchi zaidi ya milioni 14 ambapo kwa siku itakuwa na uwezo wa kuhudumia
wagonjwa kati ya 700 - 1000." Amesema Dkt. Gwajima
Rais
wa Msumbiji, Filipe Jacinto Nyusi yupo nchini kwa ziara ya siku moja ambapo
atafanya mazungumzo na Rais Magufuli kuhusu namna ya kuboresha maisha wananchi wetu
pamoja na usalama.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) muda mfupi kabla ya Rais wa
Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi kuwasili katika uwanja wa ndege wa Geita - Chato
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli na mgeni wake Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi wakipita katikati ya
gadi ya heshima mara baada ya Rais Nyusi kuwasili nchini
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli na mgeni wake, Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi wakipata maelezo
kuhusu ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Kanda - Chato kutoka kwa Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Prof. Mabula Mchembe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli na mgeni wake, Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi wakimsikiliza maelezo
ya Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy
Gwajima wakati walipofanya ziara katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda - Chato
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli na mgeni wake Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi wakiweka rasmi jiwe
la msingi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda - Chato
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli akihutubia hadhara ya wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kuweka
jiwe la msingi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda - Chato
Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi akihutubia hadhara ya wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda - Chato |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Pombe Joseph
Magufuli pamoja na Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi wakiwaaga wananchi (hawapo
pichani) mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda
- Chato
Sunday, January 10, 2021
RAIS WA MSUMBIJI FILIPE NYUSI KUFANYA ZIARA YA KIKAZI NCHINI TANZANIA
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongea na waandishi wa Habari Chato mkoani
Geita (Hawapo pichani) kuhusu ziara ya siku mbili ya Rais wa Jamhuri ya
Msumbiji hapa nchini, Mhe. Filipe
Jacinto Nyusi. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali, Wilbert Ibuge, na kushoto ni Mkuu
wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Luhumbi. Picha na Nelson Kessy
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiongea na waandishi wa Habari Chato mkoani
Geita kuhusu ziara ya siku mbili ya Rais wa Jamhuri ya Msumbiji hapa nchini, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi. Kulia ni Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali, Wilbert Ibuge, na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert
Luhumbi. Picha na Nelson Kessy
Na Nelson Kessy, Chato
Rais
wa Jamhuri
ya Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi anatarajia
kufanya ziara ya kikazi ya siku mbili hapa nchini Tanzania kuanzia tarehe 11 -
12 Januari 2021 kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
John Pombe Joseph Magufuli.
Akithibitisha
juu ya ziara hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema kuwa Mhe. Nyusi atawasili nchini kwa ziara
ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika uwanja wa ndege wa Geita -
Chato.
"Ziara hii ya Rais Nyusi ni ziara ya kindugu ambayo ilipangwa
kufanyika muda mrefu lakini haikuweza kufanyika mapema, kutokana na kutokana na
sababu mbalimbali, hususan Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
uliofanyika Oktoba 28, 2020," Amesema Prof. Kabudi.
Aidha,
Prof. Kabudi ameongeza kuwa, ziara ya Mhe Nyusi, ni kwa ajili ya kuendeleza na kuimarisha
mahusiano ya nchi zetu mbili katika maeneo anuwai, yakiwemo yale ya kidiplomasia,
kiuchumi, kisiasa na kijamii; kama yalivyoasisiwa na vyama vya ukombozi vya
nchi zetu, yaani, chama cha TANU na Chama cha Afro-Shirazi na baadaye Chama cha
Mapinduzi (CCM) kwa upande wa Tanzania na kile cha FRELIMO kwa upande wa
Msumbiji. Mtakumbuka, mahusiano haya yaliyotukuka, yaliasisiwa na viongozi
waanzilishi wa nchi zetu huru, yaani Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere kwa upande wa Tanzania na Hayati Dkt. Eduardo Tshivambo
Mondlane kwa upande wa Msumbiji.
"Uhusiano
huo pia umeendelea baada ya Msumbiji kupata uhuru wake kupitia mapambano ya
silaha mwaka 1975, ambapo, kama nyote mnavyofahamu, kuanzia Rais wa Kwanza wa
Msumbiji Huru, Hayati Samora Moises Machel, na wengine wote waliomfuatia hadi
leo, na Marais wa Tanzania baada ya Hayati Baba wa Taifa hadi leo, wote
wameendelea kuimarisha mahusiano hayo na undugu wa Watanzania na Watu wa
Msumbiji ambao kwa hakika ni ndugu wa damu," Ameongeza Prof. Kabudi
Prof. Kabudi ameeleza kuwa,
licha ya uhusiano wa Kihistoria na Kidiplomasia kati ya nchi zetu mbili, uhusiano
wa Kiuchumi nao umeendelea kuimarika. Tanzania inafanya biashara na Msumbiji
kupitia mazao ya chakula na biashara pamoja na bidhaa za viwandani. Kwa mfano,
takwimu kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) zinaonesha kuwa jumla ya mauzo
ya Nje (Export) kati ya nchi hizi mbili zilifikia Shilingi za Kitanzania
Bilioni 76.4 kwa mwaka 2018 na Shilingi za Tanzania Bilioni 93.5 kwa mwaka
2019.
Kuhusu uwekezaji, hadi sasa
makampuni makubwa ya Kitanzania yaliyowekeza mitaji mikubwa nchini Msumbiji ni
pamoja Bakheresa (Azam), Mohammed Enterprises, Quality Foam (Magodoro Dodoma),
n.k. Vilevile kuna Watanzania wanaomiliki kampuni za usafirishaji wa abiria na
mizigo pamoja na biashara za kati na ndogondogo nchini Msumbiji.
"Licha ya changamoto ya
Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu (COVID 19) SADC imeendelea kuwezesha na
kusimamia biashara miongoni mwa nchi wanachama. Wakati wa ziara hii viongozi
wetu watabadilishana mawazo ya namna ya kuendelea kuwezesha ufanyaji wa biashara,"
Ameongeza Prof. Kabudi
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa
wa Geita, Mhandisi Robert Luhumbi amewataka wananchi wa Geita kujitokeza kwa
wingi na kumpokea mgeni wakati atakapokuwa amewasili katika uwanja wa ndege wa
Geita - Chato.
"Nawasihi wananchi wa
Geita kujitokeza na kumpokea mgeni wetu, kwani hii ni fursa kwa mkoa wetu,
tunapaswa kuitumia fursa hii vizuri" Amesema Mhandisi Luhumbi.