Friday, October 22, 2021

Rais Samia ampokea Rais Ndayishimiye wa Burundi Ikulu Chamwino jijjini Dodoma


 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye alipowasili ikulu ya Chamwino jijini Dodoma
 
Rais wa Burundi Mhe. Everiste Ndayishimye akiwa jukwaani na mwenyeji wake Mhe, Samia Suluhu Hassan wakati nyimbo za Taifa za mataifa ya Burundi na Tanzania zikipigwa kwa heshima yake baada ya kuwasili Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Everiste Ndayishimiye akikagua gwaride la heshima katika viwanja vya Ikulu  Chamwino jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwatambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Everiste Ndayishimiye viongozi mbalimbali waliofika kumlaki katika viwanja vya Ikulu Chamwino

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Everiste Ndayishimiye wakiwa katika mazungumzo Ikulu Chamwino


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Everiste Ndayishimiye wakifuatilia utaratibu wa kufuata kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari  katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

 Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza mbele ya waandishi wa habari kuhusiana na mazungumzo yao na ujumbe wa Burundi yaliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Everiste Ndayishimiye akimshukuru Mhe. Rais Samia baada ya kumaliza kuongea na waandishi wa habari  katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

 

 

RAIS NDAYISHIMIYE WA BURUNDI AWASILI NCHINI

      

Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye akiwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma kwa ziara ya siku tatu ya kitaifa nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimtambulisha Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Dkt. Jilly Maleko kwa  Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.
   
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimtambulisha Mkurugenzi Idara ya Afrika, Balozi Naimi Aziz kwa  Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwatambulisha viongozi mbalimbali walifika uwanjani kumlaki  Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma
Mhe. Rais Ndayishimiye akisalimia wananchi waliofika uwanjani  kumlaki alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.
 
 

MAADHIMISHO YA SIKU YA UMOJA WA MATAIFA KUFANYIKA DODOMA

 


Wednesday, October 20, 2021

SERIKALI YAZIHAKIKISHIA KAMPUNI ZA UFARANSA MAZINGIRA SALAMA UWEKEZAJI

 Na Mwandishi Wetu, Dar

Tanzania imezihakikishia Kampuni za Kifaransa kuwa mazingira ya biashara na uwekezaji ni salama na kuwasihi kuwekeza kwa wingi hapa nchini.

Akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika kwa kongamano lililowakutanisha Mawaziri wa Kisekta, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Ufaransa Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amesema Serikali imewahakikishia wafanyabishara na wawekezaji wa kampuni za Kifaransa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inajenga na inaendelea kuboresha mazingira rafiki ya uwekezaji kwa kuondoa kero mbalimbali zilizokuwa zinawakabili wawekezaji hapa nchini.

“Serikali ya Awamu ya Sita iko serious….. na tuna azma kubwa ya kuhakikisha kwamba tunajenga mazingira rafiki ya kuweza kuwekeza na kuondoa kero zote ambazo zimekuwa zinajitokeza….na makampuni mengine yameeleza hizo kero lakini tunafurahi kuona kero hizo tayari zimeanza kuondolewa,” amesema Balozi Mulamula

Balozi Mulamula ameongeza kuwa Wafaransa wamekuwa na uhusiano mzuri na Tanzania kwa muda mrefu na hivi sasa wamekuwa na shauku ya kufanya biashara na kuwekeza kwa wingi hapa nchini…..ambapo takwimu zinaonesha watalii kutoka Ufaransa kuja Tanzania kila mwezi ni zaidi ya watalii 7000 wanaokuja kutembelea vivutio mbalimbali hapa nchini, hivyo ni changamoto kwetu kuchangamkia fursa hii adhimu.

Kwa upande wake, Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester amesema Ufaransa inatambua jitihada zinazofanywa na Serikali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji mambo ambayo pia yanatiliwa mkazo na serikali ya Ufaransa.

“Ufaransa imedhamiria kuongeza ushirikiano na Tanzania na kama mlivyoshuhudia leo tumeanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Paris hadi Zanzibar ambao ulisimama tangu mwaka 1974, huu ni mwanzo mzuri” amesema Mhe. Riester  

Mhe. Riester ameongeza kuwa wataendelea kuwaeleza na kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji wa Ufaransa juu ya fursa mbalimbali zinazopatika Tanzania ikiwemo katika sekta ya Nishati, Utalii, Viwanda, Usafirishaji pamoja na Uwekezaji ili kuja kuwekeza na kukuza ucbumi wa pande zote mbili.

Mawaziri wa Kisekta waliohudhuria kongamano hilo ni Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb), Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (Mb) Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb) Waziri wa Uwekezaji – Zanzibar Mhe. Mudrick Soraga, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb) na Waziri wa Ofisi ya Rais Uwekezaji Mhe. Geoffrey Mwambe (Mb).

Kampuni zilizoshiriki katika kongamano hilo ni pamoja na; CMA-CGM, Bolloré, Airbus, Thales, Lagardére, Total, Chama cha Wafanyabiashara wa Ufaransa-Tanzania, Engie pamoja na Maurel & Prom.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea na washiriki wa Kongamano lililowakutanisha Mawaziri wa Kisekta, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Ufaransa Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester akiongea na washiriki wa Kongamano lililowakutanisha Mawaziri wa Kisekta, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Ufaransa Jijini Dar es Salaam


Mawaziri wa Kisekta pamoja na Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ufaransa wakiendelea na Kongamano Jijini Dar es Salaam


Mawaziri wa Kisekta pamoja na Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ufaransa wakiendelea na Kongamano Jijini Dar es Salaam


Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ufaransa wakiendelea na Kongamano Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kumalizika kwa Kongamano lililowakutanisha Mawaziri wa Kisekta, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Ufaransa Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb)  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa Kongamano lililowakutanisha Mawaziri wa Kisekta, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Ufaransa Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester 



RAIS NDAYISHIMIYE WA BURUNDI KUZURU TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Evariste Ndayishimiye, anatarajiwa kuwasili nchini kwa ziara ya Kitaifa ya siku tatu kuanzia tarehe 22 hadi 24 Oktoba, 2021.

Akiongea na Waandishi wa Habari ofisini kwake jijini Dodoma, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula amesema Mhe. Rais Ndayishimiye atawasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma tarehe 22 Oktoba na kuelekea Ikulu ya Chamwino ambako atapokelewa rasmi na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Waziri Mulamula amesema baada ya kuwasili Ikulu ya Chamwino, Rais Ndayishimiye atakagua gwaride la heshima na kupigiwa mizinga 21 kwa heshima yake na baadae viongozi hao watakuwa na mazungumzo ya faragha na kufuatiwa na mazungumzo rasmi.

Balozi Mulamula amesema akiwa jijini Dodoma tarehe 22 Oktoba mchana, Mhe.Rais Ndayishimiye atatembelea na kuweka jiwe la msingi katika kiwanda cha kuzalisha mbolea ya asili yenye mchanganyiko wa madini ya phosphate na samadi kinachojengwa katika eneo la viwanda la Nala, kiwanda ambacho kinajengwa na Wawekezaji wa kampuni ya Itracom Fertilizers Limited (ITRACOM) kutoka nchini Burundi na baadaye jioni atahudhuria dhifa ya kitaifa itakayofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Balozi Mulamula ameongeza kuwa tarehe 23 Oktoba 2021 Mhe. Rais Ndayishimiye ataelekea Zanzibar ambako atapokelewa na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na kuwa na mazungumzo na mwenyeji wake huyo na baadaye ataelelekea Mkoani Dar es Salaam ambapo ataungana na mwenyeji wake Mhe. Rais Samia .

Amesema akiwa jijini Dar es Salaam Rais Ndayishimiye anatarajiwa kutembelea Bandari ya Dar es Salaam na kukagua ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) unaoendelea nchini kutokea stesheni ya Dar es salaam hadi stesheni ya Kwala - Ruvu pamoja na kutembelea bandari kavu ya Kwala inayojengwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania katika eneo hilo la Kwala mkoani Pwani ili kujionea maendeleo ya ujenzi wa bandari kavu hiyo.

Akizungumzia ziara hiyo ya Rais Ndayishimiye nchini, Balozi Mulamula amesema ni mwendelezo wa hatua zinazochukuliwa na Serikali za Tanzania na Burundi za kuimarisha uhusiano na ushirikiano kwa maslahi ya pande zote na itaendeleza na kukuza ushirikiano uliopo na kufungua fursa ya kuanzisha maeneo mingine ya ushirikiano ikiwa ni pamoja na kuwawezesha Waheshimiwa Marais hao (wa Tanzania na Burundi) kufahamu hatua zilizofikiwa katika kutekeleza maagizo yao waliyoyatoa wakati wa ziara ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan aliyoifanya nchini Burundi tarehe 16 na 17 Julai, 2021.

Balozi Mulamula amesema Mhe. Rais Ndayishimiye na ujumbe wake wanatarajiwa kuondoka nchini kurejea Burundi tarehe 24 Oktoba 2021 baada ya kumaliza ziara yake.

 

 


 

Tuesday, October 19, 2021

UFARANSA KUKARABATI UWANJA WA NDEGE “TERMINAL TWO”

 Na Mwandishi Wetu, Dar

Tanzania na Ufaransa zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika maeneo ya kimkakati ikiwemo Nishati, Elimu, Kilimo na Miundombinu ambapo Ufaransa imekubali kukarabati Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ‘Terminal Two’ Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameyasema hayo wakati akizungumza na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester leo alipowasili Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku moja.   

Kumekuwa na Miradi ambayo Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika lao la Maendeleo wamekuwa wakifadhili Miradi mbalimbali katika Sekta mbalimbali hapa nchini zikiwemo sekta za Nishati, Elimu, Kilimo na Miundombinu.

Mtakumbuka kuwa Ufaransa ndiyo waliojenga Uwanja wa Ndege wa “Termirnal Two” wa Julius Kambarage Nyerere sasa wanakuja na mradi wa kukarabati uwanja huo na kuufanya kuwa wa kisasa zaidi. Sasa hivi tu terminal three lakini terminal two imekuwa ikitumika na ndege zinazofanya safari zake za ndani hapa nchini……..mradi huu ni moja kati ya mradi mkubwa na utakamilika hivi karibuni.

Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester yupo nchini Tanzania kuzindua safari za Shirika la ndege la Ufaransa ‘Fance Airline’ kutoka Paris hadi Zanzibar ambapo mara ya mwisho kwa shirika hilo kufanya safari zake hapa nchini ilikuwa mwaka 1974.

Septemba 15, 2021 Balozi wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Nabil Hajlaouvi alisema Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika lake la ndege ‘Fance Airline’ inategemea kuanzisha safari mpya ya ndege kutoka Ufaransa moja kwa moja hadi Zanzibar kuanzia 19 Oktoba 2021.

Katika tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Colin Powell.

“Kwa kweli Serikali ya Tanzania tumeshtushwa sana na kifo chake………katika kipindi chake aliendeleza uhusiano wa Marekani na Mataifa mbalimbali, kwa kweli ni masikitiko makubwa tutamkumbuka daima,” Amesema Balozi Mulamula

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisalimiana na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester leo alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku moja


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) (wa saba kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester (kushoto kwa Balozi Mulamula) na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (wa tano kutoka kulia) pamoja na viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku moja


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb).


Maongeza baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester yakiendelea. Maongezi hayo pia yamehudhuriwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine, Balozi wa Tanzania Nchini Ufaransa Mhe. Samwel Shelukindo, Balozi wa Ufaransa Nchini Tanzania Mhe. Nabil Hajlaouvi pamoja na viongozi mbalimbali.    


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine, (kulia) akiwa na Balozi wa Tanzania Nchini Ufaransa Mhe. Samwel Shelukindo, pamoja na Mkurugezi wa Idara ya Amerika na Ulaya Balozi Swahiba Mndeme  wakifuatilia kikao cha Waziri Mulamula na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam 


Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester akieleza jambo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) pamoja na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa leo Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimkabidhi zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester leo Jijini Dar es Salaam


Mawaziri wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi leo Jijini Dar es Salaam



TANZANIA, CHINA ZAAHIDI KUIMARISHA MISINGI YA DIPLOMASIA

 Na Mwandishi wetu, Dar

Tanzania na China zimeahidi kuendelea kuimarisha misingi ya uhusiano wa diplomasia baina ya mataifa hayo iliyodumu kwa zaidi ya miaka 50 kwa lengo la kukuza na kuendeleza maendeleo endelevu kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Ahadi hiyo imetolewa na Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Chen Mingjian, wakati alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) leo jijini Dar es Salaam.

Balozi Mulamula amesema kuwa pamoja na mambo mengine, wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo suala la kukuza na kuendeleza misingi ya uhusiano wa kidiplomasia iliyowekwa wakati wa kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya mataifa haya 1964.

“Uhusiano wa Tanzania na China ni wa muda mrefu na umekuwa imara katika nyakati zote hii ni kutokana na kila taifa kuheshimu misingi ya taifa jingine na kutokuingilia masuala ya ndani ya taifa jingine, naamini kwa kuzingatia misingi hii uhusiano huu utaendelea kukua na kuimarika zaidi,” Amesema Balozi Mulamula

Balozi Mulamula ameongeza kuwa wakati wote Tanzania na China zimekuwa na maelewano mazuri ambayo yamechangia kuimarisha diplomasia kwa mataifa hayo.

Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Chen Mingjian, ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano ambao imekuwa ikimpatia tangu aliwasili na kuongeza kuwa China itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kufanya kazi kwa pamoja kwa manufaa ya mataifa mawili.

“Naamini kuwa mimi ni kiungo cha kuimarisha na kuendeleza uhusiano baina ya China na Tanzania…..tumekuwa tukishirikiana katia sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo, biashara na uwekezaji, miradi ya mikopo nafuu na misaada, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Uchukuzi, Utalii na utamaduni naahidi kuwa China itaendelea kushirikiana na Tanzania kwa maslahi mapana ya pande zote mbili,” Amesema Balozi Mingjian

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongea na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Chen Mingjian wakati walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Balozi wa China hapa nchini Mhe. Chen Mingjian akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakati walipokutana kwa mazungumzo leo katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Chen Mingjian yakiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Chen Mingjian yakiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Balozi wa China hapa nchini Mhe. Chen Mingjian akimkabidhi zawadi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Monday, October 18, 2021

TANZANIA, KENYA KUMALIZA VIKWAZO VYA KIUTAWALA DISEMBA

Na Mwandishi Wetu, Dar

Tanzania na Kenya zimedhamiria kumalizia kuondoa vikwazo vya kiutawala vilivyosalia ifikapo Disemba 2021 baada ya kuondoa vikwazo 46 visivyokuwa vya kikodi.

Hayo yamesemwa wakati wa mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Mhe. Dany Kazungu jijini Dar es Salaam ambapo takwimu zinaonesha urari wa biashara kati ya Nchi hizo umeongezeka mara sita zaidi baada ya kuondolewa kwa vikwazo hivyo.

Kutokana na hatua hiyo, Tanzania imeonekana kunufaika zaidi kwa kuondolewa kwa vikwazo hivyo kwa kuuza zaidi bidhaa zake nchini Kenya.

“Hii ni ishara nzuri kwa Tanzania lakini pia ni fursa kwa Tanzania na Kenya kuondoa umaskini kwa watoto wetu na ndugu zetu kupata ajira kwa wingi katika sekta ya biashara,” Amesema Mhe. Kazungu

Pia Balozi Kazungu amemueleza Waziri Mulamula kuhusu azma ya Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta kufanya ziara rasmi hapa nchini na kisha kuhudhuria sherehe za Uhuru tarehe 9 Disemba 2021 ambapo alialikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipotembelea Kenya mapema mwaka huu.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amesema Tanzania inaheshimu makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa awali wa kuondo vikwazo hivyo na dhamira ni kuwa ifikapo Disemba 2021 vikwazo vya kiutawala navyo viwe vimeondolewa ili kukuza zaidi mahusiano ya Kidiplomasia na Biashara baina ya Tanzania na Kenya.

“Tumekubaliana kuhakikisha ifikapo mwezi Disemba 2021 vikwazo vyote vya kitawala viwe vimetatuliwa……….azma yetu ni kuhakikisha kuwa kila kitu kinakuwa sawa kwa Ustawi wa Diplomasia na biashara baina ya Tanzania na Kenya,” amesema Balozi Mulamula.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Mwakilishi wa Taasisi ya Sister Cities ya Marekani Bi. Ronda Pierce katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Mhe. Dany Kazungu akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimuleleza jambo Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Mhe. Dany Kazungu walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam


Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Mhe. Dany Kazungu yakiendelea katika Ofisi ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam


Mwakilishi wa Taasisi ya Sister Cities ya Marekani Bi. Ronda Pierce akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam


Mazungumzo baina ya wakilishi wa Taasisi ya Sister Cities ya Marekani Bi. Ronda Pierce na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) yakiendelea katika Ofisi ndogo za Wizara leo Jijini Dar es Salaam



  

Friday, October 15, 2021

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI ATETA NA BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) aakiwa katika mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa Nchini Balozi Chen Mingjian.

Katika mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekumbushia utekelezwaji wa ahadi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi ya kuipa Tanzania masoko ya bidhaa za asali na mabondo, ahadi aliyoitoa Chato Mkoani Geita mwezi Januari,2021 wakati wa ziara yake hapa nchini


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa Nchini Balozi Chen Mingjian mara baada ya kumaliza mazungumzo.

VACANCY ANNOUNCEMENT AT THE CONSULATE OF THE REPUBLIC OF KENYA IN ARUSHA, TANZANIA.

 


CLICK HERE TO OPEN THE LINK