Friday, March 21, 2014

Matukio mbalimbali ya ziara ya Binti Mfalme wa Sweden hapa nchini

Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria Lugrid Alice Desiree akisalimiana na mmoja wa Maafisa waliompokea alipotembelea Mradi wa Maji wa WaterAid unaofadhiliwa na nchi yake uliopo Kigamboni eneo la Tungi, Wilayani Temeke, Dar es Salaam. Anayeshuhudia katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Bi. Sofia Mjema. Mtukufu Victoria alitembelea Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 19 hadi 21 Machi, 2014.
Mmoja wa Vijana wa skauti akimvisha skafu Mtukufu Victoria alipowasili katika eneo hilo.
Mtukufu Victoria akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika eneo laTungi- Kigamboni Wilayani Temeke kwa ajili ya kuangalia miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na Sweden.

Mtukufu Victoria akifurahia mapokezi kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Tungi huko Kigamboni.

Mtukufu Victoria katika matukio ya uzinduzi wa miradi huko Kigamboni eneo la Tungi
Mtukufu Victoria akizindua huduma ya maji  safi ya bomba katika eneo la Tungi
Mtukufu Victoria akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Tungi (hawapo pichani) alipotembelea shuleni hapo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tungi wakimsikiliza Mtukufu Victoria (hayupo pichani)

 ...Binti Mfalme akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kwa kuondoka nchini


Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria Lugrid Alice Desiree akizungumza na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Victoria Mwakasege huku Mkurugenzi wa Idara hiyo Balozi Dora Msechu akisikiliza wakati Binti Mfalme huyo  akijiandaa kuondoka Tanzania baada ya kukamilisha ziara yake ya siku tatu.
Picha ya pamoja
Mtukufu Victoria akiagana na Balozi Msechu mara baada ya kuhitimisha ziara yake nchini tarehe 21 Machi, 2014.

Balozi Msechu kwa pamoja na Bibi Mwakasege na Bi. Tunsume Mwangolombe (wa kwanza kushoto), Afisa Mambo ya Nje na Afisa kutoka Ubalozi wa Sweden wakisubiri ndege iliyombeba Mtukufu Victoria (haipo pichani) kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.



Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.