Thursday, March 20, 2014

Binti Mfalme wa Sweden awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimpokea Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria Lugrid Alice Desiree mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere, nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Tarehe 19 hadi 21 Machi, 2014. 
Mhe. Membe akiwa katika mazungumzo na Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria Lugrid Alice Desiree mara baada ya kuwasili nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu kwa pamoja na wajumbe walioambatana na Binti Mfalme Victoria Ludrid Alice Desiree nchini wakifuatilia kwa karibu mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Binti Mfalme wa Sweden, Mtukufu Victoria (hawapo Pichani).
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Victoria Mwakasege pamoja na Afisa Mambo ya Nje Bi. Tunsume Mwangolombe wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Membe na Binti Mfalme Victoria Ludrid Alice Desiree (hawapo pichani) 

Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.