Saturday, March 8, 2014

Wanawake Mambo ya Nje washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani

Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wameungana na Wanawake wengine kote duniani katika kusheherekea Siku ya Wanawake Duniani, iliyofanyika katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke, jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alikuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Hawa Ghasia (Mb.). Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "CHOCHEA MABADILIKO KULETA USAWA WA KIJINSIA"
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa na nyuso za furaha wakati wa maadhimisho hayo.
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika maandamano.
 Mhe. Ghasia (wa tatu kutoka kushoto) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Said Mecky Sadick pamoja na wageni waalikwa katika jukwaa wakiwashangilia Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani) walipokuwa wakipita mbele yao .
Wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakiwa wamejawa na furaha.
Wanawake  kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika Picha ya Pamoja
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bibi Amisa Mwakawago akiwaongoza wanawake wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Kimataifa kutoka uwanjani mara baada ya maadhimisho.
Picha na Reginald Kisaka


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.