Monday, March 3, 2014

Tanzania na Sweden zakubaliana kuimarisha ushirikiano


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule akisalimiana na Mhe. Tanja Rasmusson, Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Kimataifa wa Sweden alipofika Wizarani leo. Mhe. Rasmusson yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Katika mazungumzo yao waligusia masuala ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara, uwekezaji, elimu, haki za binadamu na vita dhidi ya rushwa.
Mhe. Rasmusson akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Wizarani.
Bw. Haule akizungumza na Mhe. Rasmusson
Mhe. Rasmusson akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule
Wajumbe waliofuatana na Mhe. Rasmusson wakifuatilia mazungumzo kati ya Bw. Haule na Mhe. Rasmusson (hawapo pichani). Wa kwanza kulia ni Balozi wa Sweden hapa nchini, Mhe. Lennarth Hjelmaker.
Wajumbe wa Tanzania wakifuatilia mazungumzo. Kushoto ni Bibi Victoria Mwakasege, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Lucas Mayenga, Afisa Mambo ya Nje.
Mhe. Rasmusson akifurahia jambo kwa pamoja na Bw. Haule na Balozi Hjelmaker.
Bw. Haule akimsindikiza Mhe. Rasmusson mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Bw. Haule akiagana na Mhe. Rasmusson.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.