Wednesday, March 26, 2014

Matukio mbalimbali ya ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani nchini

Ndege iliyombeba Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Frank-Walter Steinmeier ikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam tarehe 25 Machi, 2014.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akimpokea Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Frank-Walter-Steinmeier alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja nchini. Lengo la ziara ya Waziri Steinmeier lilikuwa ni kuimarisha ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Ujerumani hususan katika nyanja za biashara na uwekezaji.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Frank-Walter-Steinmeier  akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam. 
Mhe.Steinmeier akiongea na Wahadhiri, Wanafunzi, Mabalozi na watu mbalimbali ( hawapo pichani) kuhusu ushirikiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Ujerumani. Katika mjadala huo Mhe. Steinmeier aliipongeza Tanzania kwa kudumisha amani katika Ukanda wa Maziwa Makuu na Afrika kwa ujumla. Mhadhara huo ulifanyika katika Ukumbi wa Nkurumah chuoni hapo.
Waziri Membe pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo  Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Rwekaza Mukandala wakifuatilia kwa makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mhe.Steinmeier ( hayupo pichani ).
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) naye akifuatilia kwa makini hotuba ya Mhe.Steinmeier ambaye hayupo pichani. 
Washiriki mbalimbali waliokuwepo wakati wa Mhadhara uliotolewa na Mhe.Steinmeier (hayupo pichani).  
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu ( kushoto) akiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Bw. Reginald Mengi wakifuatilia kwa makini mhadhara uliokuwa ukitolewa na Mhe. Steinmeier ambaye hayupo pichani.
Kaimu Balozi wa Ujerumani hapa nchini Bw. Hans Koeppel (wa kwanza kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Philip Marmo (wa tatu kulia), Balozi  Dora Msechu, (watano kulia) pamoja na Washiriki wengine wakifuatilia Mhadhara uliokuwa ukitolewa na Mhe.Steinmeier (hayupo pichani)
Baadhi ya  Wajumbe waliofuatana na Mhe. Steinmeier (hayupo pichani) 
Picha ya Pamoja.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikianio wa Kimataifa, Bw. John Haule akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Steinmeier.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) pamoja na Mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Mhe. Steinmeier walipokuwa wakiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani)  
Waziri Membe (Mb) akifafanulia jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani)
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Steinmeier. Wakati wa ziara hiyo Mhe Steinmeier alimkabidhi Waziri Nyalandu ndege ndogo kwa ajili ya kukabiliana na uwindaji haramu  wa wanyamapori.
Waziri Membe akiagana na Waziri Steinmeier mara baada ya kumaliza ziara yake nchini. 
Mhe. Steinmeier akiagana na Balozi Philip Marmo.
Mhe. Steinmeier akiagana na Balozi Msechu.
Mhe. Steinmeier akipunga mkono kuaga kabla ya kuondoka nchini.


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.