Wednesday, March 5, 2014

Mhe. Rais Kikwete akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufaransa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Biashara za Kimataifa wa Ufaransa, Mhe. Nicole Bricq mara baada ya Waziri huyo kuwasili Ikulu. Mhe. Bricq ameitembelea Tanzania kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya nchini hizi mbili.
Mhe. Rais Kikwete katika mazungumzo na Mhe.Bricq
Mhe. Rais Kikwete akimsikiliza Mhe.Bricq wakati wa mazungumzo yao.

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu pamoja na Wajumbe wengine wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais Kikwete pamoja na Waziri wa Biashara za Kimataifa wa Ufaransa (hawapo pichani).
Balozi wa Ufaransa (katikati) nchini Tanzania pamoja na Ujumbe uliofuatana na Mhe. Bricq wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais Kikwete na Mgeni wake Mhe. Bricq hawapo pichani.
Mhe. Bricq akimkabidhi Mhe. Rais Kikwete ujumbe aliokuja nao.
Mhe. Rais Kikwete akiongozana na Mhe. Bricq mara baada ya mazungumzo
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Bricq, na wajumbe wengine.

Picha na Reginald Kisaka



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.