Thursday, November 26, 2015

Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Kuwait

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula (kulia), akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Ibrahim Al-Najem alipokuja kumtembelea Wizarani. Mazungumzo hayo yalijikita katika kuimarisha mahusiano zaidi kati ya Tanzania na Kuwait katika sekta mbali mbali zikiwemo zile kiuchumi na biashara. Pia Balozi Jasem Ibrahim Al-Najem alitumia fursa hiyo kuipongeza Wizara na Watanzania kwa kumpata Rais wa Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mazungumzo yakiendelea huku Afisa Mambo ya Nje Bw. Tahiri Bakari (wa kwanza kulia) akisikiliza na kunukuu.

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.