Wednesday, November 4, 2015

Katibu Mkuu akutana kwa mazungumzo na Msajili wa ICTR

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia), akisalimiana na Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda  (ICTR), Bw. Bongani C. Majola (kushoto) alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu utendaji wa Mahakama hiyo iliyopo Jijini Arusha. 

Bw. Majola akimweleza Balozi Mulamula majukumu na namna wanavyoendesha kesi katika mahakama hiyo .
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda ( kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga ( kulia) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mustafa Makame (katikati) nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo yaliyo kuwa yakiendelea kati ya Balozi Mulamula na Bw. Majola (hawapo pichani).
Balozi Mulamula kwa pamoja na Bw. Majola wakifurahia jambo wakati wa mazungumzo yao.
Mazungumzo yakiendelea


Picha ya Pamoja



Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.