Friday, June 23, 2017

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA NGAZI ZA JUU WA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Ngazi ya Juu wa Mapambano dhidi ya Rushwa uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima (wa kwanza kushoto), akiwa pamoja na wageni waalikwa wengine wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Ngazi ya Juu wa Mapambano dhidi ya Rushwa.
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa walio hudhuria mkutano huo.
Rais wa zamani wa nchi ya Georgia, Mhe. Mikheil Saakshvili akihutubia na kutoa uzoefu wa nchi yake kuhusu mapambano dhidi ya rushwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Ngazi ya Juu wa Mapambano dhidi ya Rushwa uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Sehemu nyingine ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akielezea ratiba nzima ya Mkutano huo.
Sehemu ya Wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa  wa Ngazi ya Juu wa Mapambano dhidi ya Rushwa , Rais huyo wa zamani alitoa uzoefu wake na wa nchi yake katika kupambana na rushwa.
Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa tatu kutoka kushoto), Mhe. Mikheil Saakshvili (mwenye tai nyekundu),
wakifurahia jambo kwa pamoja na Mhe. Angela Kairuki Waziri Ofisi ya Rais na Manajimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora wa tatu kutoka kulia.
Bi Mindi Kasiga akifurahia jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anaye hudumia nchi za Tanzania, Malawi, Burundi, Bella Bird mara baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Ngazi ya Juu wa Mapambano dhidi ya Rushwa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.