Thursday, June 29, 2017

Waziri Mahiga akutana na kaimu Balozi wa Marekani nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Dkt. Inmi K. Patterson, alipokutana naye Wizarani Jijini, Dar es Salaam, tarehe 29 Juni, 2017. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala ya ushirikiano ambapo wameahidi kuendeleza ushirikiano katika sekta za maendeleo kwa lengo la kukuza uchumi ili kuendana na kasi ya utendaji wa Serikali zao.   

Mazungumzo yakiendelea, kushoto ni ujumbe uliombatana na Kaimu Balozi, wa kwanza kushoto ni afisa tawala wa ubalozi wa Marekani Bw.Jay Zimmerman, pembeni yake ni afisa habari wa Ubalozi huo, Bi. Lauren Ladenson na kulia ni afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Redempta Tibaigana.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.