Wednesday, June 28, 2017

Balozi wa Tanzania nchini Brazil awasilisha Hati za Utambulisho

Balozi wa Tanzania nchini Brazil Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Brazil Mhe. Michel Temer, Tarehe 26 Juni, 2017. Rais Temer alisifu jitihada za Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kupigana na umasikini na kuleta maendeleo kwa wananchi. Brazil imeihakikishia kuunga mkono juhudi za Serikali  ya Tanzania katika kufanikisha miradi mbalimbali ya ushirikiano.
Mhe. Rais Michel Temer na Waziri wa Mambo ya Nje wa Brazil Mhe. Aloysio Nunes Ferreira Filho (wa tatu kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, watatu kutoka kulia ni Mama Balozi Jane Nchimbi, Bw. Frank J. Mhina, Afisa Ubalozi na Mkuu wa Utawala; na Bw. Suleiman Mombo, Afisa Mwandamizi wa Ubalozi.
Balozi Dkt. Nchimbi na Mama Balozi Jane Nchimbi, wakisindikizwa Mara baada ya kumaliza kuwasikisha hati za Utambulisho kwa Rais.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.