Wednesday, June 28, 2017

Waziri Mahiga ampokea Mjumbe Maalum kutoka Sahrawi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) amepokea Ujumbe Maalumu kutoka kwa Rais wa Sahrawi ambao uliwasilishwa kwake na Mjumbe Maalum ambaye pia ni Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Hamdi Mayera. Baada ya kuwasilisha ujumbe huo viongozi hao wawili walifanya mazungumzo yaliyojikita kwenye kuendeleza mahusiaono ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Saharawi. Mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na Balozi wa Sahrawi nchini Tanzania Mhe. Brahim Buseif.
Dkt. Mahiga akimsikiliza Mhe.Mayera
Balozi wa Sahrawi hapa nchini Mhe. Buseif (wa kwanza kushoto) pamoja na Dkt. Mahiga wakimsikiliza Mhe. Mayera alipokuwa akiendelea kuzungumza.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Bw. Suleiman Salehe (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Nicholus Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Gerald Mbwafu na katikati ni  nao kwa pamoja wa kisikiliza mazungumzo kati ya Mhe. Mayera na Dkt. Mahiga (hawapo pichani).
Waziri Mahiga (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mjumbe Maalum, Mhe. Mayera (wa tatu kushoto) pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Wizarani pamoja na Balozi Buseif.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.