Friday, July 28, 2017

KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU CHA UJIRANI MWEMA BAINA YA TANZANIA NA UGANDA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Aziz Mlima akizungumza wakati akifungua mkutano wa ujirani mwema kati ya Tanzania na Uganda, ngazi ya Makatibu Wakuu. Mkutano huo unao jadili pia masuala ya mpaka umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa ELCT Mjini Bukoba, Mkoani Kagera.
Ujumbe kutoka nchi ya Uganda wakifuatilia kwa makini hotuba ya Dkt. Mlima (hayupo pichani),  alipokuwa akizungumza wakati wa ufunguzi.
Ujumbe wa upande wa Tanzania nao wakimsikiliza kwa makini Dkt. Mlima (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, wa kwanza kutoka kulia ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu (wa kwanza kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome, na wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi Dr. Florens Turuka
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda  Balozi Patrick Mugoya naye akizungumza kwenye ufunguzi  wa Mkutano huo kati ya Tanzania na Uganda kwa ngazi ya Makatibu wa Kuu.
Dkt. Mlima (katikati) akitoa miongozo ya kikao hicho, wa kwanza kulia ni Bw. Suleiman Salehe (kulia), Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na wa kwanza kushoto ni  Balozi Mugoya.
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania ukisikiliza  kwa makini miongozo iliyokuwa inatolewa na Dkt. Mlima (hayupo pichani).
Sehemu ya Makatibu wa Kuu upande wa Uganda, nao wakisikiliza kwa makini miongozo iliyokuwa ikiendelea kutolewa na Dkt. Mlima (hayupo pichani), wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Uganda, na kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Mazingira Uganda.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera Naibu Kamishina Jeremiah M. Nkondo (wa kwanza kulia) pamoja na Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kagera Bw. Butenge  Christopher.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.