Saturday, July 29, 2017

Balozi Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Uganda

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Tumusiime Kabonero katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera, leo tarehe 29/07/2017. Waziri Mahiga yupo Mkoani Kagera kwaajili ya kuhudhuria Mkutano wa Ujirani mwema Kati ya Tanzania na Uganda. 
Waziri Mahiga akizungumza na Balozi Mteule Kabonero
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mej.Gen. Salum M. Kijuu ( wa pili kutoka kulia), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga ( wa kwanza kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Grace Mgavano (wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, nao walikuwepo kushuhudia tukio hilo
Balozi Mgavano akisalimiana na Balozi Mteule Kabonero
Waziri Mahiga akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kupokea nakala za utambulisho za Balozi Mteule Mhe. Kabonero.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.