Friday, July 28, 2017

Tanzania kuimarisha mipaka yake na nchi jirani

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi (Mb.), katikati, anaongoza ujumbe wa Tanzania kwenye ziara ya kutembelea na kujifunza juu ya mipaka iliyopo kati ya Tanzania na Uganda. Watatu kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Isaack Kamwele, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba (wa tatu kutoka kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima (wa pili kutoka kulia), Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe Gerson John Mdemu (wa kwanza kulia) na wa kwanza kushoto ni Bw. Deogratias Nholope, wakitizama Mto Kagera ulipopita.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba akisalimiana na wanakijiji wanaoishi mpakani mwa Tanzania na Uganda, mara baada ya kuwasili kwenye eneo hilo na kujionea alama za mipaka.
Mhe. Lukuvi pamoja na ujumbe wa Manaibu Waziri wakisalimiana na wanakijiji wa pande zote mbili, ambapo wananchi hao walionekana kufurahishwa na ziara hiyo.
Mhe. Lukuvi pamoja na ujumbe alioambatana nao, wakiwemo wataalamu kutoka sekta mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja.
Mhe. Lukuvi akijadiliana jambo na Manaibu Waziri alioambatana nao kwenye ziara ya kujifunza na kujionea mipaka iliyopo kati ya Tanzania na Uganda. Wa pili kutoka kulia ni Mhe. Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mhandisi Isaack Kamwelwe Naibu Waziri wa Maji (wa pili kutoka kulia), na Naibu Waziri wa TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora Mhe. Jafo Selemani Said (wa kwanza kulia).
Ziara ikiendelea ambapo Ujumbe ulioongozwa na Mhe. Lukuvi alipata fursa ya kutembelea majengo yanayotumika kwenye kukagua mizigo na kukusanya ushuru wa forodha kati ya Tanzania na Uganda yanayopatikana eneo la Mtukula.
Picha ya pamoja ya ujumbe wa viongozi na wataalam wa Tanzania ulioongozwa na Waziri Lukuvi wakiwa kwenye moja ya alama iliyopo mpakani mwa Tanzania na Uganda.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.