Tuesday, July 18, 2017

Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa SADC ngazi ya Wataalam wafunguliwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Organ Dkt. Aziz Mlima akitoa hotuba ya ufungunzi  wa Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa SADC kwenye Ushirikiano wa Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama ngazi ya wataalam.
Mkurugenzi mtendaji wa SADC Dkt. Stargomena Tax (wa pili kushoto) akizungumza kwenye mkutano wa 19 wa Mawaziri wa SADC mara baada ya ufunguzi wa ngazi ya wataalam, kulia kwake  ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Organ Dkt. Aziz Mlima, kushoto ni Mkurugenzi wa Organ kwenye masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama Bw. Jorge Cardoso, Mwisho kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Innocent Shiyo, Mkutano huo unafanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 17 - 21 Julai.
Juu na Chini ni wajumbe wakifuatilia kwa makini mkutano huo wa 19 wa Mawaziri wa SADC kwenye ushirikiano wa masuala ya siasa, ulinzi na Usalama ngazi ya wataalam.
Balozi Innocent Shio (wa kwanza kulia), akichangia hoja wakati mkutano ukiendelea, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Usalama nchini Dkt. Modestus Francis Kipilimba, kushoto kwake ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Mhe. Simon Sirro na anayefuata ni Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Mhe. Valentino Mlowola wakimsikiliza balozi Shiyo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.