Thursday, July 27, 2017

TAARIFA YA KIFO CHA BI. LOVENESS HERMAN, MTANZANIA MWENYE URAIA WA UBELGIJI

 
Mwenye picha katika kitambulisho hapo juu ni Bi. Loveness Herman (69), Mbelgiji mwenye asili ya Tanzania ambaye alifariki huko Liege, Ubelgiji tokea tarehe 18 Mei 2017. Marehemu Loveness Herman kabla ya kuhamia Ubelgiji na kuchukuwa uraia wa nchi hiyo katika miaka ya 1980 alikuwa akiishi Dar es Salaam. Tokea alipohamia Ubelgiji, Marehemu alikuwa akiishi peke yake na hakuwahi kupata mtoto. Kwa taarifa hii, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Ubalozi wake wa Brussels inawatafuta ndugu zake ili iwape taarifa kamili za msiba huo
Kwa maelezo zaidi  piga simu katika namba hii +3226406500 au barua pepe brussels@nje.go.tz.

                             

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.