Thursday, July 20, 2017

Makamu wa Rais Mhe. Samia Azindua Ripoti ya Nchi ya APRM

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria kuzindua ripoti ya nchi kuhusu Mpango wa Hiari wa Nchi za Ummoja wa Afrika kujipima kwa vigezo vya Utawala (APRM.), kushoto ni kiongozi wa Jopo la Mchakato huo kwa Tanzania ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Watu Mashuhuri Bi. Brigitte Silvia Mabandla, uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, APRM, na taasisi nyingine za kiserikali. Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam
Sehemu ya wawakilishi wa Nchi mbalimbali na Mashirika ya Kimataifa nchini wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
Sehemu ya viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nao wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya nchi kuhusu Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika kujipima kwa Vigezo vya Utawala (APRM).
Mhe. Samia Suluhu Hassan akionyesha kitabu chenye ripoti ya nchi kuhusu Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika kujipima kwa vigezo vya Utawala (APRM) mara baada ya kuzindua taarifa hiyo.
Bi. Brigitte Silvia Mabandla, naye akizungumza kwenye uzinduzi huo kwa kuishukuru Tanzania kwa kutoa ushirikiano mzuri wa kuhakikisha Ripoti hiyo inakamilika kwa wakati, pia alitumia fursa hiyo kulipongeza Jopo zima la watendaji walioshiriki katika kuiandaa ripoti hiyo kwa  ufanisi wa hali ya juu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki naye akizungumza katika uzinduzi huo, ambapo pia alitumia fursa hiyo kumkaribisha Bi. Brigitte Silvia Mabandla nchini, pia kuipongeza APRM kwa kufanya kazi nzuri.
Sehemu ya viongozi Mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania pamoja na wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa.
Profesa Hasa Mlawa naye akielezea namna ripoti hiyo ilivyo kusanywa na kuhakikiwa na viongozi wanachama.
Sehemu ya Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia wakiongozwa na Mkufunzi wao Bw. Jambo (wa tatu kutoka kusoto), nao walishiriki katika uzinduzi wa Ripoti hiyo
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga akitoa mwongozo wa ratiba kwenye hafla ya Uzinduzi wa ripoti hiyo.
Hafla ya Uzinduzi ikiendelea.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa pili kutoka kulia), Bi. Mabandla (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Aziz Mlima (wa pili kutoka kulia) Balozi Ombeni Sefue (wa kwanza kulia ) na Profesa Mlawa (wa kwanza kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi mbalimbali hapa nchini pamoja na wawakilishi wa mashirika ya Kimataifa hapa nchini. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa pili kutoka kulia), Bi. Mabandla (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Aziz Mlima (wa pili kutoka kulia) Balozi Ombeni Sefue (wa kwanza kulia ) na Profesa Mlawa (wa kwanza kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi kutoka chuo cha Diplomasia

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.