Friday, July 12, 2019

Watanzania wachangamkia soko la biashara Komoro


Balozi wa Tanzania nchini Komoro, Mhe. Balozi Sylvester Mabumba akitoa hotuba yake kwenye ufunguzi wa  mkutano wa wafanyabiashara (hawapo pichani) wa Tanzania na Komoro, katika hotuba yake aliwahakikishia wafanyabiashara kutoka Tanzania kuwa Ubalozi unaendelea kufanya kazi kwa bidii katika kuratibu shughuli za biashara baina ya Tanzania na Komoro, pamoja na kuwashauri wafanyabiashara hao kufika Ubalozini pindi watakapo kabiliwa na changamoto za aina yoyote ile.

Katika Mkutano huo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Biashara wa Komoro Mhe. Mohamed M'saidie, ambapo aliambata na 
Rais wa Chamber of Commerce ya Comoro, Ndg. Ahmed Bazi, Rais wa Chamber of Commerce wa Anjouan, Ndg. Soyad Mohamed, Rais wa Chamber of Commerce ya Ngazidja, Ndg. Soibroi Eddine Mohamed Balozi wa Sudan, Mhe. Issam Muhi El Dine Khalili na Kaimu Balozi kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini Bi. Chwane Nomcebo Valentia Mthethwa.

Aidha, 
washiriki kutoka Tanzania walipata fursa ya kuonesha, kuuza na kutangaza bidhaa zao. Sambamba na hilo washiriki waliweza pia kufanya majadiliano ya kibishara (B2B) na kuweza kuingia makubaliano ya kufanya biashara na Wakomoro.

 Sekta ambazo zimeonekana kuchangamkiwa zaidi ni sekta ya ufugaji wa kuku, mayai, bidhaa za mboga mboga na biashara ya nyama ya Ng’ombe.


Mkutano huo umefanyika katika Hoteli ya Retaj nje kigodo ya mji wa Moroni. 
Mhe Ahmed Bazi Rais wa Chamber of Commerce ya Komoro naye akitoa hotuba yake kwenye ufunguzi wa Mkutano uliowakutanisha wafanyabiashara kutoka Tanzania na Komoro
Mwakilishi wa Waziri wa Uchumi na Uwekezaji wa Komoro naye akitoa hotuba yake kwenye ufunguzi wa mkutano wa wafanyabiashara.
Add caption
Wadau wa Biashara kutoka Tanzania na Komoro wakisikiliza Hotuba zilizokuwa zikiendelea 
Maonyesho ya Bidhaa za Tanzania yakiendelea nje ya Hotel Retaj Moroni
Wajumbe wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza ufunguiz wa Mkutano ulio wakutanisha wafanyabiashara kutoka Tanzania na Komoro.








No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.