Friday, July 19, 2019

Ubalozi wa Tanzania nchini India wafanikisha hafla ya uzinduzi wa safari za Air Tanzania mjini Mumbai

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi Isack Kamwele akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa safari za  Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania) katika mji wa Mumbai nchini India. Uzinduzi huo ulifanyika katika Hoteli ya Bandra Kurla mjini Mumbai tarehe 18 Julai 2019
Waziri wa Elimu, Michezo na Ustawi wa Vijana wa India ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi rasmi wa safari za a Shirika la Ndege la Tanzania mjini Mumbai nae akizungumza kwenye hafla hiyo
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa safari za ndege za Shirika la Air Tanzania mjini Mumbai nchini India
Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Ndege ya Tanzania, Mhandisi Emmanuel Korosso nae akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa safari za Air Tanzania mjini Mumbai, India
Wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla hiyo
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akiwa tayari kukata utepe kuashiria kuanza rasmi kwa safari za Shirika la Air Tanzania mjini Mumbai, India
Mhe. Kamwele akiwa na Viongozi wengine kutoka Tanzania na India wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa safari za Shirika la Air Tanzania mjini Mumbai
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akikata keki maalum kuashiria kuanza rasmi kwa safari za Ndege za Air Tanzania mjini Mumbai, India
Matukio mbalmbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na India wakati wa uzinduzi wa safari za ndege za Air Tanzania mjini Mumbai
Mhe. Waziri Kamwelwe akipokea Jarida la Travel ambalo ambalo huandika taarifa kuhusu masuala ya usafirishaji na uchukuzi kwa ujumla
Mhe. Waziri Kamwelwe (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (wa tatu kushoto), viongozi mbalimbali kutoka Tanzania na India pamoja na Marubani waliofamikisha ndege ya kwanza ya Air Tanzania kutua Mumbai kwa ajili ya safari za kibiashara 
Mhe. Balozi Luvanda katika picha ya pamoja na wadau walioshiriki uzinduzi wa safari za ndege ya Air Tanzania mjini Mumbai. Kushoto ni Bw. Kheri Goloka, Afisa wa Ubalozi Mwandamizi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.