Saturday, July 6, 2019

Prof. Palamagamba John Kabudi atembelea maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa (Sabasaba)

Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (wa kwanza kutoka kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa Bi. Tagie Daisy Mwakawago Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Bw. Hassan Mnondwa akielezea picha za Mawaziri waliowahi kuiongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa wanafunzi waliojitokeza kwenye banda hilo. 

Bw. Joseph Mwasoto akifanunua jambo kwa wateja waliyotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba
Bi. Praxida Gasper akifanunua jambo kwa wateja waliyotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kwenye maonesho ya sabasaba

Huduma zikiendelea kutolewa kwa Wananchi mbalimbali wanaoendelea kutembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya Sabasaba
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Chuo cha Diplomasia kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akitizama Ramani ya Majengo mapya ya Chuo hicho yanayoyengwa sasa hivi, Kurasini jijini Dar Es Salaam 
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa (AICC) kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akijionea ufanisi wa utengezaji wa bidhaa mbalimbali za Nyumbani zilizotengenezwa na Jeshi la Magereza, alipotembelea banda la Jeshi la Magereza kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.

Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba
Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika mahojiano na wanahabari kwenye maonesho ya biashara kimataifa maarufa sabasaba yanayofanyika jijini Dar  es Salaam
















No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.