Monday, January 27, 2020

WAZIRI PROF. KABUDI AKUTANA NA KUPOKEA HATI ZA UTAMBULISHO WA MABALOZI WASIO NA MAKAZI NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)  amekutana na kupokea hati za utambulisho kutoka kwa Mabalozi Wateule wasio na makazi hapa nchini leo Jijini Dar es Salaam.

Mabalozi waliowasilisha nakala za hati za utambulisho ni Balozi wa Ureno Mhe. Balozi Maria Amelia Maio de Paiva mwenye makazi jijini Maputo, Balozi wa Ufilipino, Mhe. Balozi Alex G. Chua ambae makazi yake yapo jijini Nairobi, Balozi wa Jamaica Mhe. Balozi Angela Veronica Comfort mwenye makazi jijini Pretoria na Balozi wa Austria, Mhe. Balozi Dkt. Christian Fellner ambae makazi yake ni Nairobi.

Wengine ni Balozi wa Ghana Mhe. Fransisca Ashietey-Odunton mwenye makazi Jijini Nairobi, Balozi wa Venezuele, Mhe. Jesús Agustin Manzanilla Puppo ambae makazi yake yapo Jijini Nairobi pamoja na Balozi wa Djibouti Mhe. Balozi Yacin Elmi Bouh mwenye makazi Nairobi.                                             
Awali kabla ya kukabidhi hati za utambulisho kwa Mhe. Waziri, Mabalozi wateule walipata semina kutoka kwa Mkuu wa Itifaki, wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)  akiangalia nakala ya hati ya utambulisho ya Balozi wa Ureno Mhe. Balozi, Maria Amelia  Maio de Paiva

Balozi wa Ghana Mhe. Fransisca Ashietey-Odunton akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) nakala ya hati ya utambulisho


Balozi wa Ufilipino, Mhe. Balozi Alex G. Chua akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) wakati alipokuwa akipatiwa ufafanuzi wakati wa mazungumzo mara baada ya kumkabidhi Waziri nakala ya hati ya utambulisho
   Balozi wa Jamaica Mhe. Balozi Angela Veronica Comfort akimkabidhi nakala ya utambulisho Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb)
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) akikagua nakala ya hati ya utambulisho ya Balozi wa Austria, Mhe. Balozi, Dkt. Christian Fellner
   Balozi wa Venezuele, Mhe. Jesús Agustin Manzanilla Puppo akimfafanulia baadhi ya maneno  yaliyopo kwenye nakala ya hati ya utambulisho Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb)
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) akiangalia nakala ya hati ya utambulisho kutoka kwa Balozi wa Djibouti Mhe. Balozi Yacin Elmi Bouh
 
   Mkuu Mkuu wa Itifaki, wa Wizara hiyo Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge (mwenye tai ya rangi ya chungwa) akiwapa Semina Mabalozi wateule kabla ya kuwasilisha nakala za Hati zao kwa Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
   Mkuu Mkuu wa Itifaki, wa Wizara hiyo Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge (mwenye tai ya rangi ya chungwa) akiwapa Semina Mabalozi Wateule









No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.