Thursday, January 16, 2020

PROF. KABUDI ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA SULTAN WA OMAN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokelewa na Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi katika ubalozi wa Oman - Tanzania. Prof. Kabudi amekwenda ubalozini hapo kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Sultan wa  Oman, Sultan Qaboos bin Said.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Oman uliopo Jijini Dar es Salaam kufutia kifo cha Sultan wa Oman, Sultan Qaboos bin Said. Waliosimama ni Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Ramadhan Muombwa Mwinyi.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Oman uliopo Jijini Dar es Salaam kufutia kifo cha Sultan wa Oman, Sultan Qaboos bin Said. 
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Ramadhan Muombwa Mwinyi na viongozi wa Ubalozi wa Oman hapa Nchini pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na Balozi wa Oman hapa Nchini Mhe.  Ally Abdallah Almahruqi,mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Sultan wa Oman,Sultan Qaboos bin Said.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.