Thursday, January 23, 2020

BALOZI KANALI IBUGE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI MBALIMBALI, WAKUU WA MASHIRIKA YA KIMATAIFA YALIPO NCHINI


 Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa tarehe 22 na 23 Januari 2020 katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine, mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi hizo na mashirika hayo.

Mabalozi hao ni Balozi wa Visiwa vya Comoro, Mhe. Balozi Ahamada Elbadaour Mohamed, Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Balozi Frederic Clavie, Balozi wa Denmark nchini Mhe. Balozi Mette Norgaard, Balozi wa Iran nchini, Mhe. Balozi Mousa Farhang, Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe. Balozi Yonas Yosef Sanbe, pamoja na Balozi wa Italia nchini, Mhe. Balozi Roberto Mengoni.

Mbali na Mabalozi, Mkuu wa Itifaki, Balozi Kanali Ibuge amekutana na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa ambao ni Naibu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Bw. James Gitau na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Aga Khan (AKDN) Bw. Amin Kurji.



Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akimfafanulia jambo Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Balozi Ahamada Elbadaour Mohamed wakati wa mazungumzo yaliyofanyika 22 Januari 2020 katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Balozi wa Comoro nchini Tanzania Mhe. Balozi Ahamada Elbadaour Mohamed akiongea na Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati wa mazungumzo yaliyofanyika 22 Januari 2020 katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Balozi Frederic Clavie akimweleza jambo Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati wa mazungumzo yaliyofanyika leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibugea kiongea na Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe. Balozi Yonas Yosef Sanbe
Balozi wa Ethiopia nchini, Mhe. Balozi Yonas Yosef Sanbe akiongea na Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Wilbert Ibuge  
Balozi wa Iran nchini, Mhe. Balozi Mousa Farhang akimsikiliza Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa ajili ya mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Denmark nchini Mhe. Balozi Mette Norgaard akimsikiliza Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa ajili ya mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Italia nchini Meh. Balozi Roberto Mengoni akimsikiliza Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge wakati walipokutana kwa ajili ya mazungumzo leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akiongea na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Aga Khan (AKDN) Bw. Amin Kurji

Naibu Rais wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Bw. James Gitau, akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge.  Mazungumzo yaliyofanyika leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge akimfafanulia Naibu Rais wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Bw. James Gitau wakati wa mazungumzo yaliyofanyika leo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.