Wednesday, August 10, 2022

JITAHADA ZAIDI ZINAHITAJIKA KUTANGAZA KAZI ZA WIZARA NDANI NA NJE YA NCHI- BALOZI MINDI



Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga akiwasilisha mada ya Diplomasia ya Umma (Public Diplomacy) wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika katika Chuo cha Diplomasia jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika katika Chuo cha Diplomasia jijini Dar es Salaam


Balozi Mindi Kasiga akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam
                                     
Mkurugenzi Msaidizi  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Songalieli Shila akiwasilisha mada ya Umuhimu wa Tanzania kuwa mwanachama wa Jumuiya za Kikanda na Kimataifa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Msaidizi  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Songalieli Shila akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam


 Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Bw. Bernard Haule akiwasilisha mada ya Umuhimu wa Soko Huru la Biashara Barani Afrika iliyowasilishwa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam


Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam wakifuatilia mafunzo hayo 


 Mkurugenzi Msaidizi  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Songalieli Shila akiwa na baadhi ya washiriki wa mafunzo  ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mindi Kasiga amesema kuwa kuwa jitahada zaidi zinahitajika kutangaza ndani na nje ya nchi kazi ambazo Wizara inazifanya.

Balozi Mindi ametoa kauli hiyo alipowasilisha mada ya Diplomasia ya Umma (Public Diplomacy) wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari na utaalamu na ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia yaliyofanyika katika Chuo cha Diplomasia jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa licha ya Wizara kufanya kazi kubwa bado kazi hizo hazijapata fursa ya kutangazwa ipasavyo na kuna haja ya kuongeza jitihada zaidi ili kuhakikisha kazi hizo zinajulikana ndani na nje ya nchi.

Amesema waandishi wa habari ni wadau muhimu katika kufanikisha azma hiyo ya Wizara kwa kushirikiana na Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara. Balozi Kasiga aliahidi kuwa Wizara itaendelea kuandaa mafunzo hayo ambayo pamoja na mambo mengine yatawezesha kuwepo na orodha ya waandishi wenye ujuzi wa kuandika taarifa za kidiplomasia ambao watatambulishwa katika Jumuiya ya wanadiplomasia nchini na hivyo kuendelea kufanya nao kazi kwa ufanisi zaidi kuitangaza diplomasia ya Tanzania ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu.

Mafunzo hayo ya siku mbili (tarehe 27-28/ Julai, 2022) yameandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Kitengo chake cha Mawasiliano (GCU) yamewashirikisha waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari vya hapa nchini ikiwemo mitandao ya kijamii ambapo walieleza jinsi walivyofaidika na mada za mafunzo hayo zilizowasilishwa na mabalozi wabobezi na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

 

Waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo hayo walipata nafasi ya kusikiliza mada za Utekelezaji wa diplomasia ya uchumi iliyowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. Justin Kisoka; Uandishi wa taarifa za kidiplomasia iliyowasilishwa na Balozi Mstaafu Peter Kallaghe; Uzalendo katika kujenga na kulinda tasiwra ya Tanzania iliyowasilishwa na Balozi Mstaafu Patrick Tsere; Diplomasia ya Umma iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali (GCU), Balozi Mindi Kasiga; Umuhimu wa Tanzania kuwa mwanachama wa Jumuiya za Kikanda na Kimataifa iliyowasilishwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Songalieli Shila; na Umuhimu wa Soko Huru la Biashara Barani Afrika iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji, Bw. Bernard Haule.

Mada hizo zililenga kuwapatia waandishi wa habari ufahamu kuhusu majukumu, malengo na mikakati ya Wizara katika utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayojikita katika diplomasia ya uchumi.

Wawasilishaji mada walitumia fursa hiyo kuwaelimisha waandishi wa habari hao kuhusu agenda za nchi katika Jumuiya ya Kimataifa zikiwemo kutumia Soko Huru la Biashara barani Afrika kwa manufaa ya kiuchumi.

Mafunzo hayo yalifunguliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula tarehe 27 Julai, 2022 ambapo aliwaeleza waandishi wa habari kuwa ni wadau muhimu na kuwaahidi kuwa Wizara itaendelea kuimarisha uhusiano na kundi hilo muhimu kwa kuwawekea mazingira mazuri ikiwa ni pamoja na kuwaandalia mafunzo ya mara kwa mara ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.