Thursday, August 30, 2012

Kikao cha Mawaziri wa NAM


Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki kwenye Mkutano wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya Ukumbi wa Mkutano huo nchini Iran.  Pichani ni Balozi Celestine Mushy (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa iliyopo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Justin Seruhere (wa pili kulia), Kaimu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa na Bw. N.M Mboyi (wa kwanza kulia), Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Sera na Mipango.  Wengine ni Bw. Christopher Mvula (kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati na Bi. Eva Ng’itu, Afisa Dawati wa NAM hapa Wizarani. 


Balozi Mushy (wa pili kushoto-nyuma) akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Justin Seruhere (wa kwanza kulia-mbele), Bw. N.M. Mboyi (wa kwanza kulia-nyuma), Bw. Christopher Mvula (wa kwanza kushoto-nyuma) na Bw. Ally Kondo (kushoto-mbele), Afisa Mawasiliano, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.



Kikao cha Mawaziri wa NAM 

Na Ally Kondo, Tehran


Kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) kilianza nchini Iran siku ya Jumanne tarehe 28 Agosti, 2012 kwa kupitia na kuridhia nyaraka zilizoandaliwa na Wataalam katika kikao chao cha tarehe 26 na 27 Agosti, 2012.

Nyaraka hizo zimebainisha mapendekezo mbalimbali ambayo yatawasilishwa kwa  Wakuu wa Nchi na Serikali katika mkutano wao utakaofanyika tarehe 30 na 31 Agosti, 2012, ili kotoa  mwongozo kwa nchi wanachama kwa ajili ya utekelezaji. Masuala yaliyojadiliwa katika nyaraka hizo ni kuhusu hali ya kisiasa, uchumi na kijamii duniani.

Baada ya Mawaziri kupitia na kuridhia nyaraka hiyo, walipewa fursa ya kuchangia kaulimbiu ya mkutano huo ambayo inahusu mfumo wa utawala wa amani duniani (Lasting Peace through Joint Global Governance).

Takribani, Mawaziri wote waliopata nafasi ya kuchangia walisisitiza umuhimu wa nchi za NAM kushirikiana katika kutekeleza mapendekezo yaliyokubaliwa pamoja na kutafuta mbinu za kukabiliana na changamoto ambazo zinazojitokeza duniani. Walizibainisha changamoto hizo kuwa ni pamoja na uvunjifu wa amani, maamuzi ya kibabe, migogoro ya kiuchumi, kuenea kwa silaha za maangamizi na mapigano ya kutumia silaha. Changamoto nyingine ni ugaidi, uharamia, mabadiliko ya tabianchi, biashara ya madawa ya kulevya na kitendawili cha kufanya mabadiliko katika Umoja wa Mataifa hususan, Baraza la Usalama.

Kuhusu hali ya kisiasa duniani, hususan katika Mamlaka ya Palestina, Mawaziri walisisitiza umuhimu wa nchi hiyo kupewa haki ya kuunda Taifa huru kwa kuzingatia mipaka ya kabla ya mwaka 1967. Aidha, waliitaka Israel kuyaachia maeneo yote ya Palestina inayoyakalia kwa mabavu pamoja na kuwaruhusu Wapalestina wanaoishi uhamishoni kurejea katika nchi yao.

Sanjari na hilo, Mawaziri walieleza kuwa mzozo unaoendelea nchini Syria utatuliwe na Wasyria wenyewe bila kuingiliwa kwa namna yoyote iwe kijeshi kutoka nje.    

Aidha, Mawaziri walitoa wito wa kuharakisha mchakato wa kufanya mabadiliko kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ikiwa ni pamoja na kuongeza  idadi ya  wanachama wa kudumu katika Baraza hilo kwa kuzingatia jiografia ya dunia. Hivyo, walionyesha athari zinazotokana na kuchelewa kulifanyia mabadiliko Baraza hilo, ni nchi zinazoendelea kushindwa kufikia malengo yake. Baadhi ya nchi zilishangazwa na vitendo vya nchi zinazojiita watetezi wa amani duniani, kumbe kwa mlango wa nyuma nchi hizo zinapiga ngoma ya kuchochea vita.

Kuhusu masuala ya kijamii, ilisisitizwa umuhimu wa kutambua na kuheshimu tamaduni za nchi mbalimbali. Kwa mfano nchi nyingi zilitahadharisha kuwa Jumuiya ya Kimataifa izingatie tofauti za tamaduni duniani inapoyafanyia kazi masuala ya haki za binadamu. Ilielezwa kuwa haki za binadamu zisitumike kama kisingizio cha kupandikiza tamaduni za kigeni katika nchi nyingine.

Aidha, ilisisitizwa kuwa ili kubadili hali ya mambo duniani hivi sasa, NAM sharti ibuni utaratibu wake wa kutatua mizozo, kubadilishana habari na taarifa za kitelejensia pamoja na kuunda chama cha wafanyabiashara na soko la hisa.   

Aidha, Mawaziri walipinga tabia iliyojijenga wakati huu ya nchi chache zenye nguvu kufanya maamuzi kwa niaba ya nchi nyingine. Kukabiliana na hali hiyo, ilisisitizwa umuhimu wa kuwa na uwiano mzuri wa uwakilishi katika taasisi za kimataifa zinazofanya maamuzi kama vile Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Taasisi za Fedha.

Wednesday, August 29, 2012

IHL’s One-Day Seminar

  
Mr. Christoph Luedi, Head of the ICRC’s Regional Delegation in Nairobi, Kenya welcomes Hon. Angela Kairuki (MP) (2nd left), Deputy Minister of Justice and Constitutional Affairs, as the guest of honor during a one-day Seminar on the National Committee on International Humanitarian Law (IHL) held today at Coral Beach Hotel in Dar es Salaam.  Others are Hon. Adam O. Kimbisa (MP) (1st left), Secretary General of the Tanzania Red Cross and Member of the East Africa Legislative Assembly and Ms. Zainabu Gama (2nd right), National Vice-Chairperson for the Tanzania Red Cross Society (TRCS).   The one-day IHL Seminar is hosted by the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation in collaboration with International Committee of the Red Cross (ICRC) and the Tanzania Red Cross Society (TRCS).


Hon. Angela Kairuki (MP) gives her opening remarks during the IHL Seminar hosted by the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation in collaboration with International Committee of the Red Cross (ICRC) and the Tanzania Red Cross Society (TRCS).

 
Government officials listening to Hon. Kairuki (not in the photo), including Mr. Richard Maridadi (2nd left), who was present on behalf of Ambassador Irene Kasyanju, the Head of the Legal Affairs at the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation.

 
Hon. Angela Kairuki (MP), Deputy Minister of Justice and Constitutional Affairs, officially opens a one-day Seminar on the National Committee of International Humanitarian Law (IHL),  hosted by the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation in collaboration with International Committee of the Red Cross (ICRC) and the Tanzania Red Cross Society (TRCS).


 Prof. Umesh Kadam (left), Regional Legal Adviser for International Committee of the Red Cross (ICRC) Nairobi, Kenya and various Government Officials listening on to Hon. Kairuki's remarks during the IHL Seminar.


Dr. Khoti Kamanga, Coordinator from University of Dar es Salaam also was in attendance and gave his overview on Tanzania implementation in IHL.   


Other participants, included Ms. Zulekha Fundi (3rd right), Foreign Service Officer (Legal) from Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation and Ms. Linda Bore (1st right), Legal Officer for ICRC Nairobi in Kenya. 
  

Hon. Kairuki (MP) speaking to reporters about the Government's commitment to fully implement the IHL.


A group photo of Hon. Kairuki (MP) (center-seated), Ms. Gama (3rd left-seated), Dr. Kamanga (2nd left-seated), Prof. Kadam (1st left-seated) and Mr. Maridadi (1st left-standing).  Others are Mr. Luedi (3rd right-seated), Hon. Kimbisa (MP) (2nd right-seated) and Government Stakeholders during a one-day Seminar on the National Implementation of International Humanitarian Law hosted by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation in collaboration with the International Committee of the Red Cross (ICRC) and the Tanzania Red Cross Society (TRCS).   



IHL’s One-Day Seminar
By Tagie Daisy Mwakawago

“Tanzania stands ready to fully implement the International Humanitarian Law and I believe we have an important role in charting the way forward,” says Hon. Angela Kairuki (MP), Deputy Minister of Justice and Constitutional Affairs, as she launches a one-day Seminar on the National Committee on International Humanitarian Law (IHL) held today at Coral Beach Hotel in Dar es Salaam.
“It is now time for Tanzania to seriously ponder and reflect on the need of establishing such a National Committee at a national level,” said Hon. Kairuki.
The one day seminar, which was hosted by the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation in collaboration with International Committee of the Red Cross (ICRC) and the Tanzania Red Cross Society (TRCS), aimed to assist the Government bodies which are responsible to implement IHL through national legislation for its promotion and ratification in the country.  
Tanzania has already demonstrated that commitment to this ideal by signing up of the Geneva Conventions and their additional protocols, along with other treaties which limit methods and means of warfare and provide protection for people during conflicts.
“Like other countries in the world, Tanzania is duty bound to fulfill her treaty obligations under the IHL, such as the Penal Code and the Law of the Child Act to mention few,” said Hon. Kairuki, urging the participants in seminar “to share experiences, identify gaps for both policy and legal review in order to keep our system in line with the new changes which occur from day to day.” 
“The seminar demonstrates the Tanzania Government’s commitment to ensure that IHL is known and implemented in Tanzania,” commented Mr. Christoph Luedi, Head of the ICRC’s Regional Delegation in Nairobi, Kenya, on the press release issued earlier today by the International Committee of the Red Cross (ICRC).  In attendance were officials from the office of Public Service Management, Prime Minister’s Office, Ministry of Defence and National Service, Ministry of Home Affairs, Ministry of Justice and Constitutional Affairs, Ministry of Information, Youth, Culture and Development, Ministry of Health and Social Welfare and to name few. 
Making a presentation on the overview of implementation of IHL Treaties in Tanzania on behalf of Ambassador Irene Kasyanju, the Head of the Legal Affairs at the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Mr. Richard Maridadi reminded the Government Stakeholders to reflect back on the previous meetings held last year, including this seminar and coordinate with each other to find a common ground solutions to move this matter forward in realizing the implementation process for the IHL.
“As the Coordinator for the implementation of IHL Treaties within Government Institutions, we call upon fellow Stakeholders to find immediate remedies to charter forward the IHL implementation process,” said Mr. Maridadi. 


  END.



Tuesday, August 28, 2012

Ministry of Foreign Affairs to host IHL Meeting

  
ICRC logo
International Committee of the Red Cross


ICRC News Release
28 August 2012

Tanzania: Government Oficials discuss implementation of International Humanitarian Law

Dar es Salaam (ICRC) – Tanzanian government officials are to attend a seminar on the national implementation of international humanitarian law in Dar es Salaam. The Tanzanian ministry of foreign affairs and international cooperation will host 20 officials on 29 August 2012 at the Coral Beach Hotel, with organisation in the hands of the International Committee of the Red Cross (ICRC) and the Tanzania Red Cross Society (TRCS).

"The seminar demonstrates the Tanzanian government’s commitment to ensure that IHL is known and implemented in Tanzania," explained Christoph Luedi, head of the ICRC’s regional delegation in Nairobi. “The ICRC welcomes this sign of commitment on the part of the Tanzanian authorities.”

The seminar will provide guidance to government bodies such as the Public Service Management and Prime Minister’s offices and the Ministries of Defence and National Service, Home Affairs, Justice and Constitutional Affairs, Information, Youth, Culture and Sports, Education and Vocational Training, Community Development, Gender and Children, Health and Social Welfare, Social Justice, and Communication, Science and Technology, which are responsible for implementing IHL in the country. Topics will include ratifying, implementing and promoting IHL treaties and the impact of IHL in today's world. It will be opened by Tanzanian deputy minister of justice and constitutional affairs, Hon. Angela Kairuki (MP). Christoph Luedi and the TRCS vice chairperson, Ms Zainabu Gama will officiate the occasion.

For some time now, the ICRC has been supporting Tanzania’s efforts to promote and implement IHL through national legislation. International humanitarian law aims to limit the effects of armed conflict on humanitarian grounds, and Tanzania has already demonstrated its commitment to this ideal by signing up to the Geneva Conventions and their additional protocols, along with other treaties that regulate weapons of war and provide protection for people during conflicts.






For further information, please contact:
Lynette Mukuhi, ICRC Nairobi, tel: +254 733 660076
Martha Kassele, ICRC Dar es Salaam, tel: +255 782 099383
or visit
www.icrc.org




Rais Kikwete atuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange kuomboleza vifo vya askari wawili wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF) waliokuwa wanalinda amani katika eneo la Darfur, Sudan, vilivyotokea mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika salamu zake hizo, Mheshimiwa Rais Kikwete amemwambia Jenerali Mwamunyange: “Nimepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa za vifo vya vijana wetu watatu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF) ambao walikuwa wanalinda amani katika Darfur, Sudan ambavyo nimejulishwa kuwa vilitokea Jumapili iliyopita.”
Ameongeza Rais Kikwete: “Vifo vya vijana wetu hawa vinasikitisha zaidi kwa kuzingatia kuwa wamepoteza maisha yao katika utumishi muhimu sana wa nchi yetu na katika kulinda amani ya Bara letu la Afrika. Tutaendelea kuwakumbuka kwa utumishi uliotukuka na mchango wao kwa nchi yetu na kwa Bara letu la Afrika.”
Amesema Mheshimiwa Rais Kikwete: “Kufuatia vifo hivyo, nakutumia wewe, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange salamu za rambirambi. Aidha, kupitia kwako, naomba uniwasilishie pole zangu nyingi kwa familia za vijana wetu ukiwajulisha kuwa moyo wangu uko nao wakati wa kipindi hiki kigumu cha kuwapoteza wapendwa wao. Naungana nao kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, aziweke pema peponi roho za marehemu.”
Rais Kikwete pia amemtaka Jenerali Mwamunyange kuwafikishia salamu za pole Makamanda na askari wote wa Tanzania wanaolinda amani katika Darfur.
Askari hao wawili ambao ni sehemu ya wanajeshi 850 wa Tanzania wanaolinda amani katika Darfur na mwenzao mmoja ambaye hajulikani alipo mpaka sasa walipoteza maisha yao katika ajali ya gari lao kusombwa na maji wakati wakivuka mto katika Kijiji cha Hamada, eneo la Manawasha, Darfur.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
28 Agosti, 2012



Monday, August 27, 2012

The DICOTA Convention

main banner 12




About the Convention

The DICOTA 2012 Convention – themed “Tanzania’s Diaspora - Investment, Citizenship and Relationship” – this year will be held at the Chicago Marriott O'Hare, 8535 West Higgins Road, Chicago, Illinois 60631 U.S.A. from 30th August to 2nd September, 2012.

The convention brings together members of the Tanzanian Diaspora in the United States of America, Tanzanian private sector and government officials; key decision makers from Tanzania and U.S. businesses; financial institutions, charitable organizations and international organizations with vested interest in investment and social and economic growth in the country. The conference presents attendees with the latest trade and investment opportunities in all sectors of the economy, while providing a forum for potential partnership formations through many networking opportunities.

Venue: Chicago Marriott O'Hare Hotel
8535 West Higgin Road
Chicago, Illinois 60631, USA.

Dates: August 30 - September 2, 2012 

For more information, click:  http://www.dicotaus.org/


Mkutano wa NAM waanza nchini Iran


 
Na Ally Kondo,
Tehran, Iran

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikari wa Nchi Zisizofungama na Upande Wowote (NAM) umeanza jijini Tehran, Jamhuri ya Kiislam ya Iran siku ya Jumapili, tarehe 26 Agosti 2012. Mkutano huo utakaoisha tarehe 31 Agosti 2012 umeanza na kikao cha wa Wataalam ambacho kitafuatiwa na Mkutano wa Mawaziri tarehe 28 na 29 Agosti 2012 na kisha ule wa Wakuu wa Nchi na Serikali tarehe 30 na 31 Agosti 2012.

Katika Mkutano wa Wataalam, Ujumbe wa Tanzania unajumuisha Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dkt Justin Seruhere, Kaimu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York, pamoja na maafisa wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atamwakilisha Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali.

Wakati wa ufunguzi wa kikao cha wataalam, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Dkt. Ali Akbar Salehi alieleza kuwa nchi yake ambayo imechukuwa Uenyekiti wa NAM kutoka kwa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri katika kipindi cha miaka mitatu ijayo, itajitahidi kuhakikisha kuwa Umoja huo unaendelea kuimarika katika kutekeleza malengo yake ya msingi. Waziri huyo aliendelea kueleza kuwa kufanyika kwa Mkutano huo ni ishara ya wazi kuwa NAM ina dhamira ya dhati ya kuuenzi umoja huo na kuufanya kuwa chombo madhubuti cha  kutetea na kulinda maslahi ya wanachama wake.

Mhe. Salehi alifafanua baadhi ya masuala ambayo NAM imekuwa ikiyapa umuhimu mkubwa tangu kuundwa kwake mwaka 1961 na yanayotakiwa kundelea kupewa kipaumbele ni pamoja na: kutambua na kuheshimu tofauti za tamaduni duniani na kupinga jitihada zozote za kupandikiza tamaduni za kigeni zisizokubalika katika nchi nyingine.

Hivyo, alibainisha kuwa NAM inafanya juhudi kubwa kufanya majadiliano miongoni mwa jamii, tamaduni na dini tofauti kwa lengo la kukuza na kuimarisha ushirikiano, amani na kuondoa ubaguzi.

Waziri huyo alibainisha kwamba nchi zote duniani zinauona Umoja wa Mataifa kuwa ni Taasisi kubwa ulimwenguni ambayo iliundwa kutokana na athari za Vita Kuu vya pili vya dunia. Hivyo, wanachama wa NAM hawaungi mkono masuala yote ambayo yanatokea duniani yenye dhamira ya ukandamizaji kama vile dhuluma, ubaguzi, matumizi mabaya ya madaraka, ubabe, aina zote za ukoloni pamoja na mizozo inayohusisha matumizi ya silaha.

Aidha, Mhe. Salehi katika hotuba yake aligusia masuala ambayo yanajiri hivi sasa duniani, hususan Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika. Alisisitiza umuhimu wa kusikiliza ujumbe unaotolewa na watu wa maeneo hayo ambao wanapigania uhuru, haki na utu. Alisema kuwa mafunzo yanayopatikana kutokana na vitendo hivyo ni kwamba hakuna utawala ambao unaweza kupuuza matakwa na malengo halali ya watu wake. Hivyo, njia pekee ya kuepukana na masuala hayo ni tawala za kiimla zikubali kufanya majadiliano, kuheshimu haki za msingi za binadamu na kutimiza mahitaji ya msingi ya watu wao.

Kuhusu mradi wa nyuklia wa Iran, Waziri Salehi alisema kuwa mpango huo ni wa amani na hauna lengo la kutengeneza silaha za nyuklia. Alisisitiza kuwa Iran ipo tayari wakati wowote kushirikiana na upande wowote katika masuala yanayohusu masuala ya nyuklia na ambayo hayakiuki haki na wajibu wa nchi. Alisisitiza msimamo wa nchi yake kwamba haitafuti mzozo wowote au kitu chochote kile zaidi ya haki zake za kimsingi ambazo haziwezi kuzuiliwa na mtu yoyote.

Sunday, August 26, 2012

Membe: no quick fix to border crisis in Lake Nyasa

Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe on Saturday ruled out any "quick fix" in negotiations over a border dispute with Malawi.
"It's not a rush to negotiated settlement. There is no quick fix to negotiated settlement," Membe told a bilateral ministerial meeting on the dispute over Lake Malawi, where Lilongwe has awarded an oil exploration license to a British firm.
"It is a long way with corners, sometimes with sharp corners, but we must negotiate through and we negotiate because we want a solution," he said. "This is a serious business that requires serious minds."
Technical experts from the two countries wrapped up five days of talks on Friday over a long-ignored dispute that has assumed new importance with the prospect of oil revenues in the region.
The experts presented their recommendations to the ministers but a final decision rests with the countries' two presidents.
"Each side has a serious case. If you think that the other side has no serious case, that is self-deception," Membe said.
Surestream of Britain has won the right to explore for oil in northeastern waters near Tanzania, a largely undeveloped swath of Lake Malawi.
Malawi claims ownership of the entire lake under an 1890 agreement -- whose validity is disputed by Tanzania.
Membe said: "Neighbours must endure, neighbours must always remain neighbours, and we are here because of differences in positions."
He said whatever the outcome of the negotiations, "the basis must be scientific for generations to come."
Membe's Malawian counterpart Ephraim Mganda Chiume, for his part, advocated a "quick solution" on the 50-year-old dispute.
"This issue has been going on for too long. ... It has brought tension among our people and the feeling is that we should resolve it for our people to continue to co-exist in peace."
He appealed for "amicable discussions and hopefully we should come up with a long-lasting and amicable solution."

Hotuba ya Mhe. Rais Kikwete ya kuhamasisha Sensa




 

HOTUBA YA MHESHIMIWA DK JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI KUHAMASISHA SENSA YA WATU NA MAKAZI,
TAREHE 25 AGOSTI, 2012

Ndugu wananchi;
Imekuwa ni mazoea yetu kuwa Rais huzungumza na taifa kila mwisho wa mwezi.  Lakini, leo nazungumza nanyi siku saba kabla ya mwisho wa mwezi kwa sababu maalum.  Sababu yenyewe si nyingine bali ni Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika kwa siku saba kuanzia kesho Jumapili tarehe 26 Agosti, 2012. Shabaha yangu ni kutaka kuwakumbusha Watanzania wenzangu wote kuhusu wajibu wao wa kujitokeza kuhesabiwa siku hizo.  Naomba kila mmoja wetu ahakikishe kuwa anakuwepo kuhesabiwa na kujibu maswali yote yatakayoulizwa na makarani wa sensa kwa ufasaha.  

Ndugu wananchi;
Katika historia ya nchi yetu, Sensa ya mwaka huu itakuwa ni ya tano tangu Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Mapinduzi ya Zanzibar ya tarehe 12 Januari, 1964 na kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 1964.  Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988 na 2002.  Kumbukumbu zinaonesha kuwa kwa upande wa Tanzania Bara wakati  wa ukoloni zilifanyika Sensa mwaka 1910, 1931, 1948 na  1957.  Kwa upande wa Zanzibar wakati wa ukoloni na utawala wa Sultan kulifanyika Sensa mara moja mwaka 1958. 

Ndugu Wananchi;
Kama ilivyokuwa kwa Sensa zilizotangulia, madhumuni makubwa ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni kujua idadi ya watu,  mahali walipo, jinsia zao, umri wao, elimu, shughuli wazifanyazo, vipato vyao, upatikanaji wa huduma mbalimbali pamoja na makazi. Taarifa hizi hutumiwa na Serikali kupanga mipango ya maendeleo, kutengeneza programu mbalimbali na kubuni miradi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.  Aidha, huisaidia Serikali kupanga na kupeleka huduma za kiuchumi na kijamii kwa wananchi kwa kuzingatia mahitaji halisi ya maeneo yao wanayoishi kwa mujibu wa idadi yao na mgawanyiko wao kijinsia, kiumri na huduma zinazohitajika.  Hivyo basi, idadi halisi isipojulikana kuna hatari ya wananchi kukosa huduma wanazohitaji kwa kiwango kinachostahili.  Vilevile, takwimu hizi hutumiwa na Serikali katika kufikia uamuzi wa kugawa majimbo ya uchaguzi na maeneo ya utawala kama vile mikoa, wilaya, kata, vijiji na vitongoji vipya.

Ndugu wananchi;
Pamoja na umuhimu huo wa jumla wa Sensa kwa maendeleo ya nchi yetu,  Sensa ya mwaka 2012 ina umuhimu wa aina yake.  Taarifa zake zitatumika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Dira za Taifa za Maendeleo za Tanzania Bara na Zanzibar;  Mkakati wa Kukuza na Kupunguza Umaskini Tanzania Bara (MKUKUTA II); Mkakati wa Kupunguza Umaskini  Zanzibar (MKUZA II); na Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa 2011/12 – 2015/16. Vilevile taarifa zitakazopatikana zitatumika kupima maendeleo ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia (Millenium Development Goals) yaliyowekwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2000. Kama tujuavyo, itakapofika mwaka 2015 ndicho kilele cha utekelezaji wa Malengo hayo hivyo kujua hatua tuliyofikia sasa itasaidia kujipanga vizuri katika miaka mitatu iliyosalia. 

Ndugu Wananchi;
Pamoja na faida hizo, taarifa za Sensa hii zitasaidia kufanikisha zoezi linaloendelea sasa, la kuwapatia Watanzania vitambulisho vya taifa. Baadhi ya maswali yatakayoulizwa kwenye Sensa ya Watu na Makazi  yatasaidia katika kuhakiki maombi ya vitambulisho vya taifa. Bila ya shaka sote tunatambua vyema manufaa ya vitambulisho vya taifa, hivyo basi ndugu yangu, shiriki zoezi la sensa ili kuirahisishia Serikali kazi ya utoaji wa vitambulisho kwa raia wake.

Ndugu wananchi;
Shughuli yoyote kukabiliwa na changamoto mbalimbali ni jambo la kawaida.  Lakini, tofauti na miaka ya nyuma, Sensa ya mwaka huu imekabiliwa na changamoto ambazo hazijawahi kuwepo.  Kuna baadhi ya wenzetu wamekuwa wanafanya jitihada za makusudi za kutaka kulivuruga zoezi la Sensa nchini.  Wamekuwa wanawashawishi watu wasishiriki kuhesabiwa, kwa sababu ambazo baadhi yake hazina uhusiano wo wote na Sensa.  Zipo sababu nyingine ambazo hata haziingii akilini. Kwa mfano, wapo watu wanaodai kuwa hawatashiriki Sensa mpaka mjusi aliyeko kwenye Jumba la Makumbusho kule Berlin, Ujerumani atakaporudishwa.  Kinachozungumzwa hapa ni mabaki ya mifupa ya mnyama wa kale aliyekuwepo hapa nchini zaidi ya miaka milioni 200 iliyopita.  Mwaka 1906 wana sayansi wa Kijerumani waliyagundua mabaki hayo kule Tendaguru, Lindi, wakayafukua na kuyapeleka Ujerumani ambako yamehifadhiwa tangu wakati huo.

Ndugu Wananchi;
Kudai mifupa hiyo irejeshwe nchini si jambo baya, watu wataona wanyama wa kale waliokuwepo wakati huo wanafananaje.  Huenda pia kikawa kivutio cha utalii.  Hata hivyo, kugeuza kurejeshwa kwa mabaki hayo kuwa sharti la kushiriki Sensa ni jambo ambalo mantiki yake siielewi.  Watu wakisusia Sensa kwa sababu hiyo itakuwa siyo tu haieleweki wala haielezeki, bali hata watu wengine nchini na duniani watawashangaa.  Lakini, jambo ambalo ningependa wajiulize ni kuwa hivi hasa wanamsusia nani?  Mjerumani au wanajisusia wenyewe?  Hivi kweli mtu uko tayari kuacha manufaa yako ya maendeleo yapotee au yaathirike kwa sababu ya mjusi ambaye hata akirejeshwa huna manufaa ya moja kwa moja?  Hasara anapata nani sisi au wao?  Nawasihi, Watanzania wenzangu, tusiwasikilize watu wanaoeneza maneno yahusuyo Mjusi au mambo mengine ya upotoshaji na uvurugaji wa mambo yenye maslahi makubwa zaidi kwetu binafsi na nchi yetu.  Tuachane nao hawatutakii mema na wala hawaitakii mema nchi yetu.  Nawaomba tusitumie vibaya uhuru wa kutoa maoni. 

Ndugu Wananchi;
Wapo ndugu zetu wengine wanaotaka liongezwe swali la dini ya mtu katika orodha ya maswali yatakayoulizwa katika Sensa ya mwaka huu.  Wahusika wakuu hasa ni baadhi ya viongozi na wanaharakati wa Kiislamu. Wao wanasema bila ya swali hilo kuwepo, Waislamu wasikubali kuhesabiwa.  Wamekuwa wanafanya juhudi kubwa ya kuwashawishi Waislamu wawaunge mkono katika msimamo wao huo.  Nimesoma baadhi ya nyaraka na vipeperushi vyao kuhusu madai hayo.  Nilipata pia bahati ya kukutana na kuzungumza na baadhi ya wanaharakati na viongozi wa harakati hizo.  Nia yangu katika kufanya hayo ilikuwa ni kutaka kuelewa kwa undani hoja na madai yao.  Yako mambo kadhaa yanayotajwa kama sababu, lakini ukweli ni kwamba jambo linaloweza kuhusishwa moja kwa moja na Sensa, ni lile la takwimu za idadi ya Waislamu, Wakristo na Wapagani zilizotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki, Shirika la Utalii na Shirika la Utangazaji Tanzania.

Hawazikubali taarifa hizo kwa hoja kwamba, Waislamu hawajawahi kuhesabiwa na watoaji wa takwimu hizo.  Kwa sababu hiyo hawaelewi ni kwa vipi watoe idadi ya kuwa ni asilimia fulani Watanzania.  Hawana ugomvi nao kuhusu takwimu za Wakristo na Wapagani kwani huenda waliwahesabu.  Kwa maoni yao, taarifa hizo si za kweli na ni upotoshaji unaofanywa maksudi kwa sababu wanazozijua watoaji wa taarifa hizo.  Ili kuondoa upotoshaji huo, wanaharakati na viongozi hao wa Waislamu wakataka swali la dini liwepo katika Sensa hii ili ukweli ujulikane.

Katika mazungumzo yangu na baadhi ya viongozi wa Waislamu niliwaambia kuwa naelewa sababu na hoja za wao kukasirishwa na kutokuzikubali takwimu hizo.  Vile vile, niliwaeleza kuwa takwimu hizo si za Serikali bali ni za mashirika hayo.  Nilisisitiza kuwa takwimu za Serikali kuhusu idadi ya watu hutolewa na Ofisi Kuu ya Takwimu na si chombo kingine chochote cha Serikali.  Bahati nzuri Ofisi Kuu ya Takwimu haijatoa takwimu hizo na wala siyo chanzo cha takwimu zilizotolewa na mashirika hayo.  Walikozipata wanajua wenyewe.  Taarifa hizo hazina ithibati yo yote na ndiyo maana zinatofautiana. Niliwasihi waachane nazo, wazipuuze na wakipenda watoe tamko la kuzikataa. 

Ndugu Wananchi;
Niliwaambia pia kuwa kuelekeza lawama kwa Serikali kwa ajili ya taarifa hizo ni kuionea na kutoitendea haki.  Vile vile  kuibebesha dhima ya kuongeza swali la dini ili kuyajibu mashirika hayo ni kuipa mzigo usiostahili.  Napenda, kutumia nafasi hii kuwasihi wale wote wanaotoa takwimu za namna hiyo kutambua unyeti wake na kuepuka kufanya hivyo. Zinatuletea mifarakano isiyokuwa ya lazima kama ilivyo sasa.

Ndugu Wananchi;
Kwa upande wetu, yaani Serikali, imekuwa vigumu kukubali maombi ya kuliingiza swali la dini katika Sensa hii kwa sababu za kisera na kiutekelezaji.  Wakati wa ukoloni maswali ya rangi, dini na kabila la mtu yaliulizwa katika Sensa.  Baada ya uhuru, maswali hayo yaliulizwa katika Sensa ya kwanza ya mwaka 1967 kwa vile ilikuwa bado inafuata misingi ya kikoloni.  Baada ya hapo ulifanyika uamuzi wa kisera wa kutokuuliza maswali hayo kwani nia ya wakoloni kuuliza maswali yale ilikuwa ni kwa sababu ya sera yao ya wagawe uwatawale.  Walitoa huduma kwa ubaguzi, sera ambayo Serikali zetu ziliachana nayo baada ya Uhuru na Mapinduzi.  Huduma hazikuwa zinatolewa kwa ubaguzi wa rangi, kabila wala dini, bali kwa msingi wa haki ya uraia na ubinadamu wake. 

Ndugu Wananchi;
Sera hiyo pia ilikuwa na lengo la kudumisha umoja na mshikamano wa taifa letu na watu wake.  Badala ya watu kubishana juu ya watu wa dini ipi ni wengi na hivyo kufarakana kwa kutokubaliana na takwimu zilizotolewa, sera mpya inawataka watu wajivunie uwingi wao kama Watanzania.   

Ndugu Wananchi;
Nionavyo mimi Sera hii ni nzuri na kwamba ulikuwa ni uamuzi wa busara na hekima kubwa.  Tuendelee kuidumisha na kuienzi.  Kufanya vinginevyo,  na hasa kuingiza sera ya kutoa huduma kwa misingi ya dini zetu  ni kuliingiza taifa letu ambalo lina sifa ya  amani, upendo na utulivu, katika migogoro isiyokuwa ya lazima.  Ni migogoro inayoweza kuepukika kwa kuenzi na kudumisha sera yetu hii  nzuri na sahihi.
  
Ndugu Wananchi; 
Sababu ya pili inayotupa ugumu kiserikali ni ya kiutekelezaji.  Imechukua miaka kadhaa ya maandalizi mpaka kufikia hatua hii ya sasa ya kuwa tayari kutekeleza zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.  Isitoshe Sensa ya majaribio imeshafanyika kwa kutumia vifaa, madodoso na maswali yaliyopo na marekebisho kufanywa baada ya hapo.  Kuingiza mambo au jambo jipya sasa itakuwa viguku kiutekelezaji.  Kutachelewesha zoezi zima na kusababisha hasara kubwa kwa taifa. 
Kwa vile watu wote hawataulizwa swali la dini na kwa kuwa dini si kigezo cha kutoa huduma kwa wananchi, hakuna ulazima wa kusisitiza swali hilo liwepo. Napenda kuwasihi ndugu zangu wanaokereketwa na jambo hili waache kuling’ang’ania na badala yake wajitokeze kuhesabiwa. Tujitokeze kuhesabiwa ili na Waislamu nao wawemo katika idadi ya wananchi wa Tanzania. 

Ndugu Wananchi;
Sioni ulazima wa kuunda Tume Huru ya Sensa yenye uwakilishi sawa wa Wakristo na Waislamu.  Tangu mwaka 1931 kazi ya Sensa imekuwa inafanywa na Ofisi Kuu ya Takwimu nchini na ndipo ujuzi na maarifa yote yapo.  Hata ukiamua uiite Tume bado utawatumia watu hao hao, hivyo mabadiliko hayo hayana sababu.  Vile vile, sioni haja ya kuwa na mgao wa wafanyakazi wake kwa msingi wa dini kwa sababu Sensa siyo kwa ajili ya kujua Wakristo na Waislamu.   Huduma hazitolewi kwa misingi ya dini za watu.

Ndugu Wananchi;
Katika maelezo yao kwangu, hivi karibuni Kamishna wa Sensa, Hajat Amina Mrisho Said na Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Muungano, Mama Albina Chuwa walinieleza kwamba kwa kawaida katikati ya Sensa moja na nyingine, hufanyika utafiti wa kidemografia, yaani Demographic Survey.  Huu ni utafiti wa kina unaofanywa katika ngazi ya kaya ambapo taarifa za mambo mengi yahusuyo watu ambazo hazikusanywi, katika Sensa hukusanywa.  Mara ya mwisho utafiti huo kufanyika ilikuwa mwaka 1973, yaani baada ya Sensa ya mwaka 1967 na kabla ya ile ya mwaka 1978.  Ni makusudio ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu kuanzisha tena utaratibu huo mwaka 2016 ambapo baadhi ya masuala yaliyoachwa yanaweza kujumuishwa.  Subira yavuta heri. 

Ndugu Wananchi;
Nimehakikishiwa na mamlaka zinazohusika kuwa maandalizi ya sensa yamefikia hatua nzuri na zoezi liko tayari kuanza siku ya Jumapili, tarehe 26 Agosti, 2012. Lakini, mafanikio ya zoezi lenyewe  yatategemea sana ushiriki wa watu ambao ndiyo walengwa na wadau wengine.    Naomba nitumie fursa hii kuwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya na Wenyeviti na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya na Miji na wadau wengine wa kisiasa na kiutendaji wa ngazi mbalimbali waendelee  kusimamia utekelezaji wa shughuli zote za Sensa katika maeneo yao ya uongozi.  Hawana budi kuhakikisha kuwa zoezi linakuwa na mafanikio makubwa.  Wale wote wanaofanya vitendo vya kuvuruga zoezi hili wachukuliwe hatua stahiki za kisheria.
     
Nawaomba viongozi wa kisiasa na kijamii nao waendelee kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kujitokeza kuhesabiwa na kushirikiana na Makarani wa Sensa watakapokuwa wanafanya kazi yao.  Wakumbusheni kukataa kuwasikiliza au kuwafuata watu wanaowashawishi wasijitokeze kuhesabiwa.  Watu hao si wema wao na wala hawaitakii mema nchi yetu. 

Ndugu wananchi;
Nitakuwa mwizi wa fadhila kama sitawapongeza Hajat Amina Mrisho Said, Kamishna wa Sensa wa Tanzania Bara na Ndugu Mwalim Ameir, Kamisaa wa Sensa Zanzibar kwa kazi kubwa na nzuri wanayoendelea kuifanya ya kutoa uongozi wa kisiasa, kusimamia na kuratibu zoezi la Sensa nchini. Nawapongeza pia Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na watendaji wengine wa Sensa katika ngazi mbalimbali katika Mikoa, Wilaya, Majimbo, Tarafa, Kata, Mitaa, Vijiji  na Shehia kwa kazi nzuri ya matayarisho na uendeshaji wa Sensa ya mwaka 2012.  Nawatakia mafanikio mema katika kazi hii muhimu na adhimu kwa nchi yetu na watu wake.

Ndugu zangu, Watanzania wenzangu, nawaomba sote tuwaunge mkono ndugu zetu hawa kwa kushiriki katika zoezi la Sensa kuanzia siku ya Jumapili tarehe 26 Agosti, 2012.  Haya shime sote tujitokeze kuhesabiwa kwani kujitokeza kwetu ndiyo ukamilifu na mafanikio ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.  Ewe Mtanzania mwenzangu shiriki Sensa   kwa maendeleo yako na ya taifa letu. 


Mungu Ibariki Tanzania!
Mungu Ibariki Afrika!
Asanteni kwa kunisikiliza