Thursday, September 18, 2014

Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai akutana na Mkuu wa Majeshi

Mkuu wa Majeshi Nchini Tanzania Davids Mwamunyange akisalimiana na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai (NAKHEEL) Mhe. Ali Rashid Ahmed Lootah alipo mtembelea Ofisini kwake jijini Dar es salaam.
Mh. Davis Mwamunyange akifanya mazungumzo na Mhe. Lootah mara tu baada ya kuwasili ofisini kwake, Mhe. Lootah katika ziara yake anaangalia fursa za uwekezaji katika uchumi, ujenzi wa nyumba na makaazi
Afisa Mambo ya Nje Bw. Hangi Mgaka akifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Mhe. Davis Mwamunyange na Mhe. Lootah (Hawapo pichani) na (wakwanza na wapili kutoka kulia) ni wajumbe walioambatana na Mhe. Lootah katika ziara
Viongozi mbalimbali wa Serikali wakisikiliza kwa makini mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea.
Kulia ni Balozi Mdogo Omar Mjenga akizungumza jambo huku Mhe. Davis mwamunyange (wakwanza kushoto) na Mhe. Lootah (katikati) wakimsikiliza wakielekea nje mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo. 
Katikati ni Mkurugenzi wa Nyumba kutoka Dubai Mhe. Ali Rashid Ahmed lootah, nawa kwanzakushoto ni Mkuu wa Majeshi nchini Tanzania Mhe. Davis Mwamunyange na wakwanza kulia ni Balozi mdogo wa Tanzania, Dubai Mhe. Omar Mjenga wakiwa katika picha ya pamoja.
Picha ya Pamoja.
Picha na Reginald Philip.


Wednesday, September 17, 2014

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje akutana na Balozi wa Tanzania Paris, Ufaransa

Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Begum Taj, Balozi wa Tanzania Paris Ufaransa mara baada ya kuwasili Paris, Ufaransa leo tarehe 17 Septemba 2014.
Waziri Membe akiwa kwenye mazungumzo na mwakilishi wa kampuni ya Airbus Bw. Pierre-Etienne Courage. Akiwa Mjini Paris, Waziri Membe pia alikutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa Kampuni ya Renault. Pia alipokea taarifa ya maendeleo ya ununuzi wa jengo jipya la Ubalozi wa Tanzania nchini humo kutoka kwa Balozi Taj. Baada ya mikutano hiyo Mhe. Membe alielekea nchini Marekani kuhudhuria mikutano ya Umoja wa Mataifa. Wengine pichani ni maafisa wakuu wa Wizara ya Mambo ya Nje James Bwana na Olivia Maboko. Upande wa kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ulaya na Marekani Mama Vicky Mwakasege na Balozi Begum Taji.



Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba Serikali ya Dubai afanya ziara nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akisalimiana na Mkurugenzi wa Nyumba kutoka Dubai Mhe. Ali Rashid Ahmed Lootah walipokutana kwa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kampuni inayojishughulisha na masuala ya Nyumba ya OYO. Bw. Lootah yupo nchini kwa ziara ya siku mbili ya kuangalia fursa za uwekezaji katika Sekta ya Nyumba na Makazi.
Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai Bw. Omar Mjenga (katikati) akimtambulisha Mhe. Lootah (wa kwanza kulia) kwa Mkurugenzi wa IPP Media Bw. Reginald Mengi walipokutana katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam
Bw. Mjenga (wa kwanza kulia) akimtambulisha Bw. Harbert Marwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya OYO kwa Mhe. Ali Rashid Ahmed Lootah mara baada ya kuwasili nchini. 
Bw. Mjenga akiwa na mmoja wa wajumbe waliofutana na Mhe. Lootah wakati wa chakula cha jioni kwa wageni hao katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.


Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Adadi Rajabu (wa kwanza kulia) akisalimiana na Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati Balozi Simba Yahya (wa kwanza kushoto) huku Mhe. Lootah akishuhudia  
Mwenyekiti wa Kampuni ya NAKHEEL Mh. Lootah akizungumza na viongozi mbali mbali kutoka Tanzania, kabla ya chakula cha jioni, Jijini Dar es Salaam
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya OYO  Bw. Hubert Marwa akimkaribisha Mhe. Lootah katika chakula cha jioni kilichoandaliwa na kampuni yake.
Balozi Simba akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika hafla iliyoandaliwa na Kampuni ya OYO  katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam
Mwenyekiti wa kampuni ya NAKHEEL Mh. Lootah akizungumza katika hafla iliyoandaliwa na Kampuni ya OYO jijini Dar es salaam
 Meya wa Ilala,  Mh. Jerry Slaa (wa kwanza kushoto), akifuatiwa na  Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, (watatu  kushoto) ni Mkurugenzi Masood Al Zarooni aliyeambatana na Mh. Lootah na wa kwanza kulia ni Bw. Harbert Marwa, wakimsikiliza kwa makini mh. Al Rashid Ahmed Lootah alipokuwa akizungumza.
Balozi Simba akimsikiliza Mh. Lootah wakati wanazungumza.


Wageni waalikwa wengine
Mazungumzo yakiendelea.
Balozi mdogo wa Tanzania nchini Dubai Balozi Mdogo. Omar Mjenga alitoa shukrani kwa Menyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai, Mhe. Lootah kwa kukubali mwaliko wake wakuja nchini Tanzania, pia aliwashukuru Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuwa mwenyeji wa ugeni huo na mwisho kwa wageni wote walio udhuria.


Balozi Simba Yahya (wa kwanza kulia),  Balozi Adadi Rajabu (katikati) na  Balozi mdogo wa Tanzania nchini Dubai Bw. Omar Mjenga.
Picha ya Pamoja


Picha na Reginald Philip

Tuesday, September 16, 2014

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia akutana na Balozi wa China nchini

Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kulia) akutana na Balozi wa China nchini Mhe. Lu Youqing,  kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya miaka 50 ya ushirikiano kati ya Tanzania na China yatakayofanyika nchini China mwezi Oktoba 2014.  
Maafisa kutoka Hazina na Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo hayo kwa makini. 
Maafisa walioambatana na Balozi wa China wakinukuu mazungumzo kati ya Balozi Mbelwa na Balozi Lu Youqing (hawapo pichani).
Kikao kikiendelea.
Picha na Reginald Philip

Friday, September 12, 2014

Wizara ya Mambo ya Nje yakutana na Wadau kuandaa ushiriki kwenye Mkutano wa DICOTA


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya DIASPORA katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Rosemary Jairo akizungumza wakati wa kikao cha Wadau cha maandalizi ya Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Watanzania waishio Marekani (DICOTA 2014) utakaofanyika North Carolina nchini Marekani kuanzia tarehe 2 hadi 5 Oktoba, 2014. Wadau hao wanatoka katika Wizara, Taasisi za Serikali na Sekta Binafsi.
Sehemu ya wadau wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya DIASPORA (hayupo pichani)
Wajumbe wakati wa kikao cha maandalizi.
Wajumbe wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao
Kikao kikiendelea.
Sehemu nyingine ya wadau wakifuatilia kikao
Mdau kutoka CRDB, Bi. Lucy Naivasha akichangia wakati wa kikao hicho.
Baadhi ya wadau wakifuatilia kikao.


Thursday, September 11, 2014

Balozi Mushy akutana na Wawakilishi wa Nchi za G4 nchini Tanzania

Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiongea jambo wakati alipokutana na wawakilishi wa nchi za G4 hapa nchini ambazo ni India, Brazil, Ujerumani na Japan. Mwingine katika picha ni Bibi Ramla Khamis, Afisa katika Wizara ya Mambo ya Nje. Balozi Mushy na wawakilishi hao walijadili masuala ya mabadiliko katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo alisisitiza msimamo wa bara la Afrika wa kupatiwa nafasi mbili za ujumbe wa kudumu zenye kura ya turufu katika Baraza hilo pamoja na nafasi tano za ujumbe usio wa kudumu.

Wawakilishi wa nchi za G4 nchini wakimsikiliza kwa makini Balozi Mushy hayupo pichani. kutoka kulia ni Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Debnath Shaw; Naibu Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. John Reyels; Afisa wa Ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania; Naibu Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Mhe. Pedro Martins; Afisa wa Ubalozi wa Japan nchini Tanzania, Bibi Noriko Tanaka.  

Mazungumzo yakiendelea baina ya Balozi Mushy na Wawakilishi wa nchi za G4 nchini Tanzania

Picha ya Pamoja baina ya Balozi Mushy (watatu kutoka kulia) na Wawakilishi wa Nchi za G4.


Picha na Anthony Guninita



Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini

Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Mark Childress alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani na kukumbuka Wahanga wa tukio la kigaidi lililotokea Marekani miaka 13 iliyopita (September 11th, 2001). Mazungumzo yao yalifanyika tarehe 11 Septemba 2014.
Mhe. Membe akimweleza jambo Balozi Childress wakati wa mazungumzo yao.
Balozi Childress pamoja na Bw. Vincent Spera, Afisa kutoka  Ubalozi wa Marekani wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)


Wednesday, September 10, 2014

Rais Museveni awasili nchini kwa ziara rasmi ya siku moja

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimpokea Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ziara rasmi ya siku moja.

Mhe. Museveni akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Museveni akisaliamiana na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Ladislaus Komba wakati wa mapokezi yake.
Mhe. Museveni akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala alipowasili Jijini Dar es Salaam kwa ziara rasmi ya siku moja.
Mhe. Rais Kikwete akiongozana na Mhe. Rais Museveni.
Mhe. Museveni akipita katikati ya Gwaride Maalum mara baada ya kuwasili nchini kwa ziara rasmi ya siku moja huku akisindikizwa na Mhe. Rais Kikwete.
Mhe. Rais Museveni kwa pamoja na Mhe. Kikwete wakiangalia burudani iliyokuwa ikitolewa uwanjani hapo na kikundi cha matarumbeta wakati wa mapokezi.
Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Rais Museveni, Ikulu
Mhe. Rais Kikwete wakiwa katika chumba cha mazungumzo na Mhe. Rais Museveni.