Friday, May 22, 2015

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Mbelwa Kairuki (Kulia) akimkaribisha na kufanya mzazungumzo na Mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika Mashariki katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Australia, Bi. Henderson. Mazungumzo yao yalijikita katika kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini hususani katika sekta ya Mafuta na Gesi.
Bi. Henderson akielezea jambo kwa Balozi Kairuki.
Wakwanza kushoto ni Bertha Makilage, (Katikati) ni   Bi. Zainabu Angovi, Maafisa Mambo ya Nje na kushoto ni Bi. Juliet Mutayoba ambaye yupo katika mafunzo  ya vitendo Wizara ya Mambo ya Nje.
Mazungumzo yakiendelea.
Picha ya Pamoja

Picha na Reginald Philip


MKUTANO NA BI. HENDERSON, MKURUGENZI WA KITENGO CHA AFRIKA MASHARIKI KATIKA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA AUSTRALIA

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia amekutana na kufanya mazungumzo na Bi. Henderson, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Mashariki kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Australia leo tarehe 21 Mei 2015.

Katika mazungumzo yao, waligusia juu ya maendeleo ya maandalizi ya ziara ya Dkt. Kim Hames, Naibu Waziri Mkuu wa Jimbo la Magharibi mwa Australia na Waziri wa Afya na Utalii. Aidha Bi. Henderson aliipongeza Tanzania kwa kuandaa warsha na mikutano ya kutangaza fursa mbalimbali zipatikanazo nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na  uwekezaji katika sekta ya mafuta, gesi na madini ambapo mwaka jana alihudhuria moja ya warsha iliyofanyika jijini Adelaide, Australia.

Kwa upande wake Balozi Kairuki alichukua fursa hiyo kuishukuru serikali ya Australia kwa nafasi za ufadhili wa masomo ya muda mfupi na mrefu katika sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo na Afya.

Kwa kuhitimisha, Balozi Kairuki alimweleza Bi. Henderson juu ya uwepo wa fursa mbalimbali za uwekezaji nchini na kuwasihi wawekezaji kutoka Australia wasisite kuja kuwekeza katika sekta ya madini, nishati na gesi nchini.

Thursday, May 21, 2015

Tanzania kukuza Ushirikiano na Indonesia

Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari na Diplomasia kwa Umma kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Ndonesia Balozi Esti Andayane, Balozi Kairuki pamoja na mgeni wake walikutana kwa mazungumzo yaliyo jikita katika kukuza Ushirikiano kati ya Tanzania na Indonesia kwenye nyanja mbalimbali za Kiuchumi.   
Balozi Kairuki akimsikiliza Balozi Esti Andayane wakati wa mazungumzo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Bi. Mindi Kasiga (Wa kwanza Kushoto), katikati Afisa Mambo ya Nje Khatibu Makenga na wakwanza kulia ni Dora Lucas Maina akiwa katika Elimu ya Vitendo.
Ujembe ulioambatana na na Balozi Esti Andayane nao wakisikiliza mazungumzo kati ya Balozi Kairuki na Balozi Andayane (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea
Picha ya pamoja baada mazungumzo.

Picha na Reginald Philip


MKUTANO NA MKURUGENZI MKUU WA IDARA YA HABARI NA DIPLOMASIA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA INDONESIA

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Habari na Diplomasia ya Umma (Director General for Information and Public Diplomacy) kutoka Wizara ya mambo ya Nje ya Jamhuri ya Indonesia, Balozi Esti Andayane.

Katika mazungumzo yao, Mabalozi hao wamekubaliana kukuza ushirikiano baina ya Indonesia na Tanzania katika nyanja za uchumi.  Balozi Andayane ameelezea utayari wa Indonesia kuendelea kuisaidia Tanzania katika sekta ya Kilimo kwa kutoa fursa za mafunzo kwa ajili ya wataalam wa kilimo nchini.  Tayari Indonesia imeisaidia Tanzania kwa kujenga Kituo cha Utafiti wa Kilimo kilichopo Mkindo mkoani Morogoro. Aidha, katika mazungumzo hayo Balozi Andayane alitoa taarifa kuwa serikali ya Indonesia imeisaidia Tanzania matrekta pamoja na vifaa vyake. Tayari Wizara ya Kilimo imeshughulikia uingizaji wa matrekta hayo.

Kwa upande wake, Balozi Mbelwa Kairuki aliishukuru serikali ya Indonesia kupitia Mkurugenzi huyo kwa misaada mbalimbali wanayotoa kwa serikali ya Tanzania. Pia alishukuru serikali ya Indonesia kwa kuialika Serikali ya Tanzania katika maadhimisho ya miaka 60 ya ushirikiano kati ya bara la Afrika na Asia zilizofanyika Jakarta na Bandung mwishoni mwa mwezi wa nne mwaka 2015. 


Wednesday, May 20, 2015

Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi lihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania



Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza na pia anakuwa Rais wa kwanza wa Msumbiji kulihutubia Bunge la Tanzania. Katika Hotuba yake nzuri Rais Nyusi iliwasifu Waasisi wa Mataifa ya Msumbiji na Tanzania na kusifia mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi hizi mbili na kuahidi kuimarisha mahusiano katika Siasa na Uchumi. Rais Nyusi alifanya ziara ya kitaifa ya siku tatu ikiwa ni ziara yake ya  kwanza tangu aingie madarakani. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) wa kwanza kushoto mstari wa pili, pamoja na Wabunge wengine wakisikiliza Hotuba kutoka kwa Mhe. Rais Nyusi (Hayupo pichani)


Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Ombeni Sefue (Kushoto) naye akisikiliza Hotuba kutoka kwa Rais Nyusi
Viongozi Mbalimbali wa Serikali wakisikiliza Hotuba ya Mhe. Rais Nyusi Bungeni. 
 Balozi wa Tanzania nchni Msumbiji, Balozi Shamimu Nyanduga (kulia)  naye akiwa bungeni akifuatilia Hotuba ya Mhe. Rais Nyusi.
Mkurugenzi wa Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge Bw. Jossey Mwakasyuka (Wa kwanza kulia), na Maafisa Mambo ya Nje (wa pili Kulia) ni Bw. Khatibu Makenga akifuatiwa na Bw. Mudrick Soraga (wa tatu Kushoto)
Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda akizungumza
Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akipokelewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda alipowasili katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma na kupata fursa ya kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (katikati) ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
Mhe. Rais Filipe Jacinto Nyusi akiwa kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa  zikipigwa.
Kikosi cha Brass Bendi cha Jeshi la Polisi kikipiga Nyimbo za Taifa mara baada ya Rais wa Msumbiji, Mhe. Nyusi kuwasili katika Viwanja vya Bungeni Mjini Dodoma
Makaribisho ya Rais wa Msumbiji, Mhe. Nyusi yakiendelea katika viwanja vya Bungeni.
Rais wa Msumbiji akikagua gwaride la Heshima wakati wa mapokezi yake mjini Dodoma.
Rais wa Msumbiji Mhe. Nyusi pamoja na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete wakiongozwa kuingia Bungeni na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda.
Rais wa Msumbiji Mhe. Nyusi na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakiongozwa na Spika wa Bunge kutoka Nje ya Bunge mara baada ya Kumaliza kulihutubia Bunge.


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika, Bi. Zuhura Bundala (wa kwanza kushoto), Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Bw. Thobias Makoba (watatu kutoka kushoto), na katikati na Bi Talha Mohamed wakiwa Bungeni. 
Rais wa Msumbiji akipokea Picha yenye mwonekano wa Jengo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Spika wa Bunge,  Mhe. Anna Makinda huku ikishuhudiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete (Wa kwanza Kulia).


Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi na Rais Kikwete wakiwa katika picha ya Pamoja na Viongozi wa Serikali na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Picha na Reginald Philip

Monday, May 18, 2015

Rais wa Msumbiji awasili Zanzibar.

Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar akitokea Jijini Dar es Salaam,ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kitaifa ya siku tatu nchini Tanzania.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Ali Mohamed Shein akiwa ameongozana na mgeni wake Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi mara baada ya kuwasili katika  Zanzibar leo tarehe 18 Mei, 2015.
 Rais Shein akiwa na Rais Nyusi kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa  zikipigwa kwa heshima ya Rais Nyusi.
 Rais wa Msumbiji Mhe.Nyusi akikagua Gwaride la Heshima wakati wa mapokezi yake. 
 Rais wa Msumbiji, Mhe.Nyusi pamoja na Rais wa Zanzibar Mhe.Dr.Shein wakifurahia burudani ya kikundi cha ngoma wakati wa mapokezi hayo huku Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe.Maalim Seif Sharif Hamad (kulia kwa Rais Shein) na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe.Balozi Seif Ali Iddi (kulia) wakifurahia pia burudani hiyo.
 Rais Nyusi na Rais Shein wakiteta jambo wakati wakiangalia burudani ya ngoma za asili.


Kikundi cha Ngoma kikitumbuiza wakati wa mapokezi hayo

Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt.Ali Mohamed Shein akiwa na mgeni wake Rais wa Msumbiji pale alipomkaribisha Ikulu kwa mazungumzo.


.....Kuelekea Hotelini


 Halaiki ya Wanafunzi waliokuwa wamejipanga barabarani kusherehesha mapokezi ya Rais wa Msumbiji Visiwani Zanzibar.
 Rais wa Msumbiji akiangalia  mmoja wa watumbuizaji anavyopuliza kifaa chake  kwa ustadi mkubwa huku akiwa  amejilaza chini wakati Rais huyo akiwasili hotelini kwake 

Picha na Reuben Mchome

Rais wa Msumbiji atembelea Chuo cha Diplomasia, afungua Kongamano la Uwekezaji na kuzungumza na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini



Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akiwajadiliana jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia (CFR),  Balozi Mwanaidi Maajar  huku Mkuu wa Chuo hicho Balozi Mohammed Maundi akisiskiliza wakati viongozi hao wakisubiri kumpokea Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi alipotembelea Chuoni hapo leo tarehe 18 Mei, 2015 wakati akiendelea na ziara yake ya kitaifa ya siku tatu hapa nchini. Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini, Dar es Salaam kilianzishwa mwaka 1978 kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Msumbiji.
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Balozi Maundi alipotembelea Chuoni hapo wakati wa ziara yake hapa nchini
Balozi Maundi akiwatambulisha baadhi ya Wahadhiri wa Chuo hicho kwa Mhe. Rais Nyusi
Juu na Chini:  Mhe. Rais Nyusi akizungumza na Wahadhiri, Wanafunzi na Wageni mbalimbali alipotembelea Chuo cha Diplomasia (CFR)
Wajumbe wakifurahia jambo wakati Rais Nyusi (hayupo pichani) alipozungumza nao 
Mhe. Rais Nyusi akifurahia zawadi ya picha ya kuchora inayowaonesha Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Msumbiji, Hayati Samora Machel aliyozawadiwa alipotembelea Chuo cha Diplomasia
Rais Nyusi akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Tanzania na Msumbiji pamoja na  Uongozi wa Chuo cha Diplomasia. Kushoto ni  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, Mhe. Hawa Ghasia (wa kwanza kushoto) ambaye ni Waziri anayeongozana nae kwenye ziara hii.
Mhe. Rais Nyusi akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia
Rais Nyusi akiangalia bango linalosomeka "CHUO HIKI KILIKUWA CHUO CHA ELIMU YA JUU KWA WAPIGANIA UHURU WA AFRIKA" ikiwa ni jina la awali kabla Chuo cha Diplomasia hakijaanzishwa.
Mhe. Rais Nyusi akiangalia Jiwe la Msingi la kuanzishwa kwa Chuo hicho



......Rais Nyusi alipozugumza na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini


Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akifurahia kikundi cha ngoma cha Raia kutoka Msumbiji wanaoishi hapa nchini alipowasili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kuzungumza nao.

Sehemu ya umati wa Raia wa Msumbiji wanaoishi hapa nchini wakimpokea kwa shangwe Rais Nyusi alipokutana  na kuzungumza nao wakati wa ziara yake ya kitaifa ya siku tatu hapa nchini


Mhe. Rais Nyusi akizungumza na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini (hawapo pichani)


Mhe. Rais Nyusi akipokea zawadi kutoka kwa mmoja wa Raia wa Msumbiji wanaoishi hapa nchini



......Rais Nyusi aliposhiriki Kongamano la Biashara na Uwekezaji 


Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano kwa ajili ya kushiriki na kufungua rasmi Kongamano la kukuza Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Msumbiji. Wakati wa Kongamano hilo mada mbalimbali kuhusu fursa za uwekezaji baina ya nchi hizi mbili zilitolewa.

Mhe. Rais Nyusi kwa pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Mhe. Christopher Chiza (kushoto) wakifuatilia mada za uwekezaji zilizowasilishwa wakati wa kongamano la kukuza uwekezaji kati ya Tanzania na Msumbiji
Wajumbe waliohudhuria kongamano hilo.