Wednesday, September 16, 2015

Mhe. Rais Kikwete awaapisha rasmi Balozi Mwakasege, Bundala, Kilima, Luvanda, Mbega na Shiyo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Bi. Victoria Richard Mwakasege aliyekuwa Naibu Balozi wa Tanzania nchini Burundi. Balozi Victoria R. Mwakasege anaiwakilisha Tanzania nchini Malawi. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 16 September, 2015
Balozi Mwakasege akisaini kiapo chake mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Mwakasege vitendea kazi
Mhe. Rais Kikwete (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mwakasege na familia ya Balozi Mwakasege
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha aliyekuwa  Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi.Zuhura Bundala kuwa Balozi na Msaidizi wa Rais (Diplomasia) anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Samweli Shelukindo. 
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Bundara vitendea kazi 
Mhe. Rais Kikwete (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Bundala na familia ya Balozi Bundala
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha aliyekuwa  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Innocent E. Shiyo kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara hiyo
Balozi Shiyo akisaini kiapo chake mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Shiyo vitendea kazi
Mhe. Rais Kikwete (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Shiyo na familia yake
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha aliyekuwa Afisa Ubalozi Mkuu, Ubalozi wa Tanzania, Muscat, Oman, Bw. Abdallah Kilima kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 
Balozi Kilima naye akisaini kiapo chake mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Kilima vitendea kazi
Mhe. Rais Kikwete (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Kilima na familia yake
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi, Ubalozi wa Tanzania, Kampala, Uganda Bi. Anisa Mbega kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 

Balozi Mbega naye akisaini kiapo chake mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Mbega vitendea kazi
Mhe. Rais Kikwete (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mbega na wanafamilia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha aliyekuwa Mratibu wa Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu Bw. Baraka H. Luvanda kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 
Balozi Luvanda naye akisaini kiapo chake mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Luvanda vitendea kazi
Mhe. Rais Kikwete (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Luvanda na familia yake

Balozi Irene Kasyanju (wa kwanza kulia), akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Celestine Mushy (katikati) na wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar Balozi Silima Haji Kombo walipokuwa katika hafla ya uapisho wa Mabalozi na wakurugenzi wapya

Wakurugenzi wasaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali watu wakifuatilia zoezi la uapisho wa Mabalozi na Wakurugenzi likiendelea
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Asha Rose Migiro (katikati) ambaye alikuwepo kwenye sherehe hizo akisalimiwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kulia). Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula (Kushoto).
Balozi Mwakasege (kushoto),  Balozi Bundala (kulia) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Diaspora Bi. Rosemary Jairo wakiwa katika picha ya pamoja na nyuso za furaha mara baada ya kumaliza kuapishwa kuwa Mabalozi 
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Itifaki Bw. James Bwana (kushoto) akimpongeza Balozi Zuhura Bundala (kulia) mara baada ya kuapishwa kuwa Balozi.
Bi. Mindi Kasiga (kushoto) akimpongeza Balozi Mbega (kulia) mara baada ya kuapishwa kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wapya pamoja na Waziri Membe, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mabalozi wapya wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Balozi Liberata Mulamula (wa nne kushoto mstari wa mbele), Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya (wa tatu kutoka kushoto), Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Juu na chini ni Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje wakiwasubiri Mabalozi wapya kuwasili Wizarani hapo mara baada ya kuapishwa. 
Maafisa Mambo ya Nje wakiwa na maua wakisubiri  kuwakabidhi Mabalozi wapya kama ishara ya pongezi na kuwakaribisha Wizarani.
Sehemu nyingine ya watumishi wa Wizara hiyo wakiwatizama Mabalozi (hawapo pichani) wakiwasili Wizarani hapo mara baada ya kuapishwa Ikulu
Balozi Mwakasege akifuatana na Mabalozi wenzake kuteremka kwenye Basi maalumu lililoandaliwa kwaajili yao wakiwasili Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mara baada ya kuapishwa kuwa Mabalozi
Balozi Mwakasege (kushoto) akipokea maua kutoka kwa Afisa Mambo ya Nje Felista Rugambwa (kulia)
Balozi Samweli Shelukindo aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Afrika naye akipokea maua kutoka kwa Afisa Mambo ya nje Eliet Magogo, mara baada ya kuwasili Wizarani.
Balozi Luvanda naye akipongezwa na Balozi Irene Kasyanju mara baada ya kuwasili Wizarani hapo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard  Membe (Mb.), katikati akipongezwa na Watumisho wa Wizra ya Mambo ya Nje kwa uongozi mzuri katika Wizara hiyo.
Waziri Membe akizungumza neno huku watumishi wa Wizara hiyo wakimsikiliza

Picha na Reginald Philip

Tuesday, September 15, 2015

Balozi Mulamula akutana na Balozi wa Canada hapa Nchini.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Alexandre Leveque ofisini kwake katika mazungumzo ya kudumisha ushirikiano. 
 Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Alexandre Leveque akisisitiza jambo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakati wa mazungumzo hayo, kulia ni Afisa Mambo ya Nje wa Wizara hiyo Bw. Lucas Mayenga akifuatilia mazungumzo hayo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula, akizungumza na Balozi wa Canada hapa nchini.
Balozi Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Alexandre Leveque, mara baada ya mazungumzo yao.
=========================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

Monday, September 14, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Balozi Mteule Victoria Richard Mwakasege
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Ndugu Victoria Richard Mwakasege kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi. Kabla ya uteuzi wake, Ndugu Mwakasege alikuwa Naibu Balozi wa Tanzania nchini Burundi.    


Balozi Samwel Shelukindo

 Aidha, Rais Kikwete amemteua Msaidizi wa Rais wa Diplomasia, Balozi Samwel Shelukindo kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje naUshirikiano wa Kimataifa





Balozi Mteule Zuhura Bundala
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue pia imesema kuwa Rais Kikwete ameteua Ndugu Zuhura Bundala kuwa Balozi na Msaidizi wa Rais (Diplomasia) kujaza nafasi iliyoachwa na Ndugu Shelukindo. Kabla ya uteuzi wake, Ndugu Bundala alikuwa Mkurugenzi Msaidizi na Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Afrika. 



Balozi Mteule Abdallah Kilima
Taarifa hiyo iliyotolewa leo, Jumatatu, Septemba 14, 2015, imesema vile vile kuwa Rais Kikwete amewateua wakurugenzi wengine wanne wa Wizara hiyo ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimatiafa na kuwapandisha cheo kuwa mabalozi.

Walioteuliwa ni Ndugu Abdallah Kilima ambaye anakuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati. Kabla ya uteuzi wake, Ndugu Kilima alikuwa Afisa Ubalozi Mkuu, Ubalozi wa Tanzania, Muscat, Oman.

Balozi Mteule Baraka H. Luvanda

Ndugu Baraka H. Luvanda ambaye anakuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Sheria. Kabla ya uteuzi  wake, Ndugu Luvanda alikuwa Mratibu wa Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu.







Balozi Mteule Innocent E. Shiyo
Ndugu Innocent E. Shiyo ambaye anakuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda. Kabla ya uteuzi wake, Ndugu Shiyo alikuwa Mkurugenzi Msaidizi katika Idara hiyo hiyo.



Balozi Mteule Anisa K. Mbega


Bibi Anisa K. Mbega ambaye ameteuliwa kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora. Kabla ya uteuzi wake, Ndugu Mbega alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Ubalozi wa Tanzania, Kampala, Uganda.


Uteuzi huo wote umeanza leo, Jumatatu, Septemba 14, 2015.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

14 Septemba, 2015