Thursday, October 13, 2016

Tanzania na China zasaini Mkataba kusaidia sekta za maendeleo nchini

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Dkt. Charles Mwijage akizungumza katika mkutano kati yake na Naibu wa Viwanda wa Jamhuri  ya Watu wa China, Mhe. Dkt. Qian Keming.Mazungumzo yao yalijikita katika kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na China katika kuboresha miundombinu.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Dkt. Keming wakimsikiliza kwa makini Dkt. Mwijage hayupo pichani.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wakisaini Mkataba wa Makubaliano ya Kushirikiana katika masuala ya uchumi na teknolojia
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda (wa kwanza kushoto), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Ramadhani Muombwa Mwinyi (katikati), na Mwakilishi kutoka Kituo cha Uwekezaji wa Tanzania kwa pamoja wakishuhudia uwekwaji saini katika mkataba huo.
Dkt. Mwijage na Dkt. Keming wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mkutano.


***********************************************************




Serikali ya Watu wa China imeahidi kuipatia Tanzania msaada wa fedha wa kiasi cha Shilingi bilioni 97 kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Kauli hiyo ilitolewa leo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Mb) baada ya kukutana na ujumbe kutoka China unaongozwa na Naibu Waziri wa Biashara wa nchi hiyo, Mhe. Dkt. Kian Keming.

Dkt. Kian na ujumbe wake upo nchini ambapo pamoja na mambo mengine walishiriki kikao cha tano cha Kamati ya pamoja ya Uchumi, Biashara, Uwekezaji na Ushirikiano wa Kiteknolojia kilichofanyika jijini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Fedha na Mipango.

Mhe. Mwijage alieleza kuwa katika kikao hicho walijadili masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji katika viwanda, miundombinu na nishati. Alisema Serikali ya awamu ya tano imeweka mkazo katika maeneo hayo ili kufikia lengo la nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Alieleza kuwa katika harakati za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020, viwanda viwili vya chuma na marumaru vilivyojengwa na wawekezaji kutoka China vinatarajiwa kufunguliwa mwishoni mwa mwaka huu au mwanzoni mwa mwaka ujao. Kiwanda cha tatu kitaanza kujengwa na wawekezaji wa China muda wowote watakapopewa eneo kwa ajili ya ujenzi huo.

Kiwanda cha kwanza ni cha chuma kilichopo Mlandizi mkoani Pwani ambapo kitakapoanza kazi, kitazalisha tani 1,200,000 za chuma kwa mwaka. Aidha, kiwanda kingine cha marumaru kilichopo Mkuranga mkoani Pwani kinatarajiwa kuingiza pato la Dola za Marekani nilioni 150 kwa mwaka, kitakapoanza uzalishaji.

Kiwanda kinachosubiri kujengwa ni cha nguo ambacho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mita milioni 240 kwa mwaka. Mhe. Waziri alieleza kuwa juhudi za kupata ekari 700 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda hicho kwenye Wilaya ya Mkuranga zinaendelea na hivi karibibuni eneo hilo litakabidhiwa kwa wawekezaji hao.

Kwa upande wake, Dkt. Kian aliihakikishia Serikali ya Tanzania kuwa China itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania ya kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Aidha, aliwakaribisha makampuni ya Tanzania kushiriki maonesho ya biashara yanayofanyika nchini China ili kuzitangaza bidhaa za Tanzania kwa madhumuni ya kupata soko nchini humo.

Mawaziri hao wawili waliweka saini Mkataba wa Makubaliano ya Kushirikiana katika masuala ya uchumi na teknolojia.



Wednesday, October 12, 2016

PRESS RELEASE


    
         
                           PRESS RELEASE 
SADC ORGAN TROIKA MINISTERIAL ASSESSMENT MISSION KINSHASA, DRC



The Southern African Development Community (SADC) Troika of the Organ on Politics, Defence and Security Cooperation undertook an assessment mission to the Democratic Republic of Congo (DRC) from 10th to 13th October 2016. The objective of the mission was to conduct an assessment of the political and security developments in the DRC aimed at assessing the on-going efforts related to peace and political stability of the DRC. H.E. John Pombe Joseph Magufuli, President of the United Republic of Tanzania in his capacity as the Chairperson of the Organ on Politics, Defence and Security cooperation mandated the Mission.

The assessment mission was led by Hon. Dr. Augustine P. Mahiga, Minister of Foreign Affairs and East African Cooperation of the United Republic of Tanzania and Chairperson of the Ministerial Committee of the Organ (MCO), who was accompanied by Hon. Georges Rebelo Chikoti, Minister of External Relations of the Republic of Angola and Deputy Chairperson of the MCO, Hon. Patricio Jose, Deputy Minister of National Defence of the Republic of Mozambique representing the outgoing chairperson of the MCO. The Mission was supported by the SADC Secretariat led by H.E. Dr. Stergomena Lawrence Tax, Executive Secretary of SADC. The mission also included SADC Ambassadors accredited in the DRC.

The Mission consulted with various stakeholders, including SADC Ambassadors accredited to the DRC, H.E. Edem Kodjo, African Union Facilitator of the National Dialogue, Hon. Raymond Tshibanda, Minister of Foreign Affairs and International Cooperation of DRC, Mr. Corneille Nangaa, and Mr. Nobert Katintima, Chairperson and Deputy of the Independent Electoral Commission (CENI) respectively, Senior Officials of the DRC Government, Representatives of Opposition Outside the  Dialogue (Rassemblement), Representatives of Opposition in the Dialogue, political parties in the Presidential majority led by Hon. Aubin Minaku, civil society and religious groups.

Following consultations and exchange of views with the various stakeholders, the Organ Troika Ministerial Mission:

1.   Noted the encouraging progress in the on-going AU-led National Dialogue and voters’ registration;

2.   Commended all stakeholders participating in the National Dialogue and noted progress made so far. Further urged all stakeholders who are not part of the National Dialogue to join the process;

3.   Encouraged all stakeholders to put the interest of the country and the people of the DRC first in the National Dialogue in order to ensure consensus on outstanding issues;

4.   Strongly condemned the violence that took place on 19th to 20th September 2016, which resulted in the loss of lives of innocent civilians and police officers as well as destruction of property. Further called on all stakeholders to act responsibly and avoid any actions that would result in any acts of violence;

5.   Strongly discouraged any attempts and threats that are aimed at undermining the process of Dialogue.

6.   Urged all stakeholders to create a conducive environment for free, fair democratic, peaceful, transparent and credible elections in the interest of peace, national unity, stability and socio-economic development of the country and to uphold the principles; ideals and aspirations of the Congolese people as enshrined in the Constitution and in accordance with SADC and AU principles and guidelines governing democratic elections;

7.   Urged all eligible Congolese voters to fully participate in the on-going voters registration process in order to exercise their democratic right as enshrined in the Constitution in the next elections;

8.   Called upon all stakeholders in the DRC, the international community and the Support Group to continue supporting the Africa Union-led National Dialogue and the electoral process, with a view to ensure sustainable peace, security and stability in the DRC; and

9.   Re-affirmed SADC’s support to the ongoing National Dialogue and pledged its full support to the final outcome.



Done in Kinshasa, Democratic Republic of Congo
12th October 2016

Waheshimiwa Mabalozi watembelea Chuo Kikuu cha Afya kilichopo Mloganzila.



Balozi wa Tanzani Moscow Mhe. Luteni Generali Wynjones Mathew Kisamba (wa kwanza kushoto) akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea walipotembelea Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili kilichopo Mloganzila, Jijini Dar es Salaam. Waheshimiwa Mabalozi walipata fursa ya  kuona miradi inayoendelea Chuoni hapo, sambamba na uwekezaji katika miundombinu ya vifaa vya kisasa vya matibabu. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki 
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe.Radhia Msuya akizungumza wakati wa ziara yao katika Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili kilichopo Mloganzila, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Ephata Kaaya
Makamu Mkuu wa Chuo  Kikuu cha Afya Muhimbili cha Mloganzila Jijini Dar es Salaam Profesa Ephata Kaaya (katika) akiwakaribisha Waheshimiwa Mabalozi walipotembelea chuo hicho
Picha ya pamoja mbele ya Jengo la Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili kilichopo Mloganzila Jijini Dar es Salaam



Mabalozi waahidi neema MUHAS

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzanikatika nchi mbalimbali duniani wameahidi kuzishirikisha Serikali na Sekta binafsi kwenye nchi walizopo kuja kuwekeza na kuchangia katika miradi mbalimbali ya afya hapa nchini ikiwemile ya Chuo Kikuu  cha Afya na Sayansi Kishiriki cha Muhimbili (MUHAS) hususan kwenye maendeleo ya teknolojia, miundombinu na kutoa mafunzo kwa wataalam wa afya.

Mabalozi hao walitoa ahadi hiyo walipotembelea na kuonana na Uongozi wa juu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na Sayansi Mhumbili kilichojengwa katika  eneo la Mloganzila nje kidogo ya Jiji Dar es Salaam.
          Taswira ya Jengo la Chuo Kikuu Shirikishi cha Afya na Sayansi Muhimbili
kilichojengwa eneo la Mloganzila Jijini Dar es Salaam.


Akizungumza na Uongozi wa Chuo hicho na wadau waliojitokeza kwenye ziara hiyo, kwa niaba ya  Mabalozi wengine Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya alitoa pongezi kwa Serikali na Uongozi wa Chuo hicho kwa hatua madhubuti zinaoendelea kufanyika ili kuboresha mazingira ya tiba nchini sambamba na mazingira ya kufundishia wataalam wa kutoa huduma za afya.

Kwa upande wake, Makamu   Mkuu wa Chuo hicho Profesa Ephata Kaaya alisema kuwa Hospitali hiyo iliyojengwa kwa mkopo wa masharti nafuu wenye thamani ya Dola za Kimarekani 49,500,000 kutoka Serikali ya Korea Kusini ni ya kisasa na itatoa huduma za kiafya za hali ya juu. 

Pia aliongeza kusema kuwa  Mafunzo bora kwa wanafunzi wa fani za afya, uchunguzi wa magonjwa na tafiti zenye ubora katika fani za afya hapa nchini yatatolewa chuoni hapo na kwamba kukamilika kwa chuo hicho kutapunguza gharama za kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu.

"Waheshimiwa Mabalozi, njambo la faraja kuwa Hospitali hii itakapoanza kufanyakazi itapunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya wagonjwa na gharama zinazotumika kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu" alisema Prof. Kaaya.

Katika hatua nyingine, Prof. Kaaya aliwaomba Mabalozi waliotembelea Chuo hicho kusaidia katika upatikanaji wa wataalam waliobobea kwenye masuala ya afya kutoka nchi za nje kutokana na upungufu wa wataalam hao nchini, ili waweze kushirikiana nao katika kutoa huduma bora za afya pamoja na kufundisha wataalam wetu.



Aidha alieleza kuwepo kwa mpango wa kuanza kwa mradi wa ujenzi wa Kituo Kilichobobea katika masuala ya Utafiti, mafunzo na Tiba ya Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu katika Ukanda wa Afrika Mashariki kitakachojengwa katika eneo hilo la Chuo la MloganzilaUjenzi wa kituo hicho utaanza mwezi Mei 2017. Ilielezwa kuwa kupitia Mradi huu jumla ya wataalamu 24 wa kada  mbalimbali za magonjwa ya moyo na mishipa ya damu watapewa mafunzo katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi. 

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wapo nchini kufuatia kikao kati yao na Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kilichofanyika tarehe 07 Oktoba, 2016.