Wednesday, October 12, 2016

Waheshimiwa Mabalozi watembelea Chuo Kikuu cha Afya kilichopo Mloganzila.



Balozi wa Tanzani Moscow Mhe. Luteni Generali Wynjones Mathew Kisamba (wa kwanza kushoto) akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea walipotembelea Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili kilichopo Mloganzila, Jijini Dar es Salaam. Waheshimiwa Mabalozi walipata fursa ya  kuona miradi inayoendelea Chuoni hapo, sambamba na uwekezaji katika miundombinu ya vifaa vya kisasa vya matibabu. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki 
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe.Radhia Msuya akizungumza wakati wa ziara yao katika Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili kilichopo Mloganzila, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Ephata Kaaya
Makamu Mkuu wa Chuo  Kikuu cha Afya Muhimbili cha Mloganzila Jijini Dar es Salaam Profesa Ephata Kaaya (katika) akiwakaribisha Waheshimiwa Mabalozi walipotembelea chuo hicho
Picha ya pamoja mbele ya Jengo la Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili kilichopo Mloganzila Jijini Dar es Salaam



Mabalozi waahidi neema MUHAS

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzanikatika nchi mbalimbali duniani wameahidi kuzishirikisha Serikali na Sekta binafsi kwenye nchi walizopo kuja kuwekeza na kuchangia katika miradi mbalimbali ya afya hapa nchini ikiwemile ya Chuo Kikuu  cha Afya na Sayansi Kishiriki cha Muhimbili (MUHAS) hususan kwenye maendeleo ya teknolojia, miundombinu na kutoa mafunzo kwa wataalam wa afya.

Mabalozi hao walitoa ahadi hiyo walipotembelea na kuonana na Uongozi wa juu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na Sayansi Mhumbili kilichojengwa katika  eneo la Mloganzila nje kidogo ya Jiji Dar es Salaam.
          Taswira ya Jengo la Chuo Kikuu Shirikishi cha Afya na Sayansi Muhimbili
kilichojengwa eneo la Mloganzila Jijini Dar es Salaam.


Akizungumza na Uongozi wa Chuo hicho na wadau waliojitokeza kwenye ziara hiyo, kwa niaba ya  Mabalozi wengine Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya alitoa pongezi kwa Serikali na Uongozi wa Chuo hicho kwa hatua madhubuti zinaoendelea kufanyika ili kuboresha mazingira ya tiba nchini sambamba na mazingira ya kufundishia wataalam wa kutoa huduma za afya.

Kwa upande wake, Makamu   Mkuu wa Chuo hicho Profesa Ephata Kaaya alisema kuwa Hospitali hiyo iliyojengwa kwa mkopo wa masharti nafuu wenye thamani ya Dola za Kimarekani 49,500,000 kutoka Serikali ya Korea Kusini ni ya kisasa na itatoa huduma za kiafya za hali ya juu. 

Pia aliongeza kusema kuwa  Mafunzo bora kwa wanafunzi wa fani za afya, uchunguzi wa magonjwa na tafiti zenye ubora katika fani za afya hapa nchini yatatolewa chuoni hapo na kwamba kukamilika kwa chuo hicho kutapunguza gharama za kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu.

"Waheshimiwa Mabalozi, njambo la faraja kuwa Hospitali hii itakapoanza kufanyakazi itapunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya wagonjwa na gharama zinazotumika kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu" alisema Prof. Kaaya.

Katika hatua nyingine, Prof. Kaaya aliwaomba Mabalozi waliotembelea Chuo hicho kusaidia katika upatikanaji wa wataalam waliobobea kwenye masuala ya afya kutoka nchi za nje kutokana na upungufu wa wataalam hao nchini, ili waweze kushirikiana nao katika kutoa huduma bora za afya pamoja na kufundisha wataalam wetu.



Aidha alieleza kuwepo kwa mpango wa kuanza kwa mradi wa ujenzi wa Kituo Kilichobobea katika masuala ya Utafiti, mafunzo na Tiba ya Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu katika Ukanda wa Afrika Mashariki kitakachojengwa katika eneo hilo la Chuo la MloganzilaUjenzi wa kituo hicho utaanza mwezi Mei 2017. Ilielezwa kuwa kupitia Mradi huu jumla ya wataalamu 24 wa kada  mbalimbali za magonjwa ya moyo na mishipa ya damu watapewa mafunzo katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi. 

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wapo nchini kufuatia kikao kati yao na Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kilichofanyika tarehe 07 Oktoba, 2016.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.