Wednesday, October 5, 2016

Naibu Waziri akutana na Wabunge wa Tanzania Bunge la Afrika Mashariki

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kati ya Uongozi wa Wizara na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (hawapo pichani) walipofika Wizarani kwa ajili ya kujadili suala la EPA na masuala mbalimbali yenye maslahi kwa Tanzania yanayoendelea katika Bunge hilo.
Baadhi ya Wabunge hao wakimsikiliza Mhe. Kolimba (hayupo pichani). Kutoka kulia ni Mhe. Shy-Rose Bhanji (Mb.), Mhe. Abdallah Mwinyi (Mb.) na Mratibu kutoka EALA.
Sehemu ya Wajumbe kutoka Wizarani waliohudhuria kikao hicho. Kushoto ni Bw. Stephen Mbundi, Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Bw. Joachim Otaru, Mkurugenzi Msaidizi.
Mhe. Shy-Rose Bhanji akizungumza jambo wakati wa kikao hicho
Mhe. Naibu Waziri kwa pamoja na Waheshimiwa Wabunge hao wakifuatilia mada zilizowasilishwa wakati wa kikao hicho
Wabunge wakifuatilia uwasilishwaji wa mada. Kushoto ni Mhe. Angela Kizigha
Mhe. Kolimba (kushoto) pamoja na Wakurugenzi wa Wizara. Kutoka kulia ni Bw. Oswald Kiamani, Mkurugenzi Msaidizi, Sera na Mipango, Balozi Baraka Luvanda, Mkurugenzi wa Sheria na Bw. Bernard Haule, Kaimu Mkurugezni wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji.
Maafisa walioshiriki kikao hicho.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.