Tuesday, October 4, 2016

Makamu wa Rais wa Cuba atembelea Kiwanda cha Dawa za Mbu kilichopo Kibaha

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa akisalimiana na Dkt. Samuel Nyantahe,  Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha Dawa za Kuua Viluwiluwi wa Mbu kilichopo Kibaha, Pwani mara baada ya kuwasili Kiwandani hapo kwa ajili ya kukitembelea. Katikati yao ni Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu.
Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Bw. Mkucha akitoa taarifa fupi kuhusu Kiwanda hicho ambapo alisema kitaanza uzalishaji mwezi Oktoba, 2016 na tayari kimeajiri watu 126. Kiwanda hicho ambacho kimejengwa kwa ushirikiano wa Tanzania na Cuba kina uwezo wa kuzalisha lita milioni 6 za dawa ambazo zitatosheleza matumizi ya Tanzania na nchi nyingine jirani.
Sehemu ya Wananchi na Wageni waalikwa waliohudhuria tukio hilo
Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa akizungumza kuhusu umuhimu wa Kiwanda hicho katika kupambana na malaria na kwamba Serikali ya Cuba itaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania katika kupambana na ugonjwa huo.
Mhe. Mesa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Viongozi wa Wataalam kutoka Cuba wanaofanya kazi Kiwandani hapo
Mtaalam mwingine kutoka Cuba akitoa maelezo ya namna maabara kiwandani hapo zinavyofanya kazi
Mhe. Mesa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Wataalam wanaofanya kazi kiwandani hapo
Mhe. Mesa akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kiwanda hicho.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.