Friday, October 21, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Iran Nchini aliyemaliza muda wake

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Iran Nchini aliyemaliza  Muda wake Mhe.Mehdi Aghajafari. Balozi Mhe. Mehdi Aghajafari wiki ijayo anatarajia kuondoka Nchini kurejea Iran. 
Kutoka Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdalah Kilima, maafisa kutoka Wizarani Bi. Zainab Angovi, Bw. Gerald Mbwafu na Kisa Doris Mwaseba wakifuatilia mazungumzo
Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga na Balozi wa Iran Nchini aliyemaliza muda wake Mhe.Mehdi Aghajafari wakionesha zawadi ya picha iliyokabidhiwa Mhe. Balozi


Wakati huo huo Waziri Mahiga amekutana na kuongea na Balozi wa Kuwait Nchini Mhe. Jasem Al-Najem  

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Agustine Mahiga akimsikiliza Balozi wa Kuwait Nchini Mhe. Jasem Al-Najem wakati wakifanya mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam


Waziri Mhe. Mahiga akielezea jambo wakati akifanya mazungumzo na Balozi wa Kuwait Nchini Mhe. Jasem Al-Najem. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya kati Balozi Abdallah Kilima akifuatilia mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.