Tuesday, October 4, 2016

Rais Dkt. Magufuli akutana na Rais Kabila Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe. Joseph Kabila. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Oktoba, 2016. Mhe. Rais Kabila yupo nchini kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Mhe. Rais Magufuli akipeana mkono na Rais Kabila mara baada ya mazungumzo kati yao
Mhe. Rais Magufuli akizungumza na Waandishi wa  Habari (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano waliyokubaliana na Rais Kabila.
Mhe. Rais Kabila naye akizungumza na Wanahabari na Wageni waaalikwa
Wakuu wa Vyombo vya Usalama nchini wakifuatilia mkutano Ikulu
Balozi wa DRC nchini, Mhe. Jean Pierre Mutamba (kushoto) na wageni wengine waalikwa wakiwa Ikulu
Rais John Pombe Magufuli na Rais Joseph Kabila wakishuhudia uwekwaji saini wa Makubaliano kati ya Tanzania na DRC kuhusu Utafiti na Uendelezaji wa Utafiti wa Mafuta katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika.
Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Mhongo na Mwenzake wa DRC wakibadilishana Mkataba huo wa Makubaliano mara baada ya kuusaini
Mazungumzo rasmi
Mhe. Rais Magufuli akimpatia Rais Kabila zawadi ya Kinyago mashuhuri cha Umoja kinachoonesha Umoja na Mshikamano wa Watanzania.
Rais Kabila naye akimpatia Rais Magufuli zawadi
Picha ya pamoja
Rais Kabila akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga
Rais Kabila akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, . Dkt. Aziz Mlima
Rais Kabila akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo
Mhe. Rais Magufuli akiwa ameongozana na mgeni wake Mhe. Rais Kabila alipompokea Ikulu

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.