Wednesday, October 5, 2016

Rais Kabila aweka Jiwe la Msingi la Jengo la Bandari ya Dar es Salaam nchini Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe. Joseph Kabila Kabange akikata utepe pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (wa kwanza kulia), na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Pro. Makame Mbarawa (wa kwanza kulia) wakati wa kuweka jiwe la msingi katika Jengo la Mamlaka ya Bandari lililopo nchini Jijini Dar es Salaam. Mhe. Magufuli amatumia nafasi hiyo kumuhakikishia Mhe. Kabila kuwa wafanyabiashara kutoka Congo hawatopata matatizo kwa kutumia Bandari ya Dar es Salaam, kwa kuwa Serikali imerekebisha mapungufu yaliyokuwepo kipindi cha nyuma.
Rais Kabila na Dkt. Magufuli pamoja na Prof. Mbarawa wakifurahia kwa pamoja kwa kupiga makofi mara baada ya kumaliza uwekaji wa Jiwe la msingi la Jengo la Mamlaka ya Bandari Jijini Dar es Salaam
Marais wakiangalia michoro ya jengo jipya la Mamlaka ya Bandari
Mhe. Kabila pamoja na Mwenyeji wake Rais Magufuli wakipata maelezo juu michoro ya Ghorofa hilo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu Mhandisi, Deusdedit Kakoko (aliyeshikilia kipaza sauti).


Rais Kabila akipokea zawadi inayoonesha mwonekano wa Bandari ya Dar es Salaam 
Viongozi mbalimbali wa Serikalini wakishuhudia tukio la hilo la uwekwaji wa Jiwe la Msingi wa Jengo la Mamlaka ya Bandari. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Aziz Mlima.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo Mhe. Joseph Kabila Kabange pamoja na viongozi mbalimbali alioongozana nao. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.