Tuesday, October 4, 2016

Makamu wa Rais wa Cuba ahitimisha ziara yake nchini

Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa akipungia wananchi wa Zanzibar waliojitokeza kumuaga katika uwanja wa ndege wa Abeid Aman Karume, Zanzibar. Mhe. Mesa aliondoka Zanzibar mapema leo asubuhi na kuwasili Dar es Salaam  ambapo alielekea Kibaha kutembelea mradi unaofadhiliwa na Cuba  nchini wa kuzalisha dawa za kuua viluwiluwi wa mbu wanaoeneza Malaria.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ameambatana na Makamu wa Rais wa Cuba, Mhe. Salvador Valdes Mesa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akiondoka nchini baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku tatu.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.