Sunday, March 12, 2017

Waziri Mahiga ampokea Mjumbe Maalum kutoka Ujerumani

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akizungumza na Mjumbe Maalum, Balozi Harro Adt aliyewasilisha Ujumbe Maalum kutoka kwa Kansela wa Ujerumani, Mhe. Angela Merkel kwenda kwa  Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Pamoja na mambo mengine walizungumzia pia namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Deus Kaganda wakifuatilia  mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Balozi Adt (Hawapo pichani).
Sehemu ya Wajumbe waliofuatana na Balozi Adt (hayupo pichani) nao wakifuatilia mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea
Waziri Mahiga akiagana na Balozi Adt mara baada ya kumaliza mazungumzo.
Waziri Mahiga (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mjumbe Maalum, Balozi Adt (wa nne kushoto) pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Wizarani pamoja na Ubalozi wa Ujerumani nchini.
===================================================
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

Taarifa kuhusu Mjumbe Maalum kutoka Ujerumani

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga amesema kuwa Tanzania na Ujerumani zitaendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ikiwemo yale yanayohusu kudumisha amani na usalama duniani pamoja na kuheshimu misingi ya haki za binadamu kupitia Jumuiya za Kikanda na Kimataifa.

Mhe. Waziri Mahiga  ameyesema hayo alipokutana kwa mazungumzo na Balozi Harro Adt, Mjumbe Maalum wa Kansela wa Ujerumani, Mhe. Angela Merkel kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli alipofika Wizarani kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe huo.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Waziri Mahiga alisema kuwa, Ujerumani na Tanzania zina mahusiano ya kihistoria tangu enzi za ukoloni hadi sasa. Katika  masuala ambayo Tanzania inanufaika na ushirikiano huo ni pamoja na ujenzi wa miundombinu, maboresho katika sekta ya elimu na mchango katika uhifadhi wa wanayamapori.

“Uhusiano wa Tanzania na Ujerumani ni wa kihistoria tangu ukoloni. Hata hivyo Ujerumani  wamejaribu kutafsiri ushirikiano wetu katika misingi bora sasa kuliko ile ya kikoloni. Ujerumani imekuwa ikiisaidia Tanzania moja kwa moja  katika sekta mbalimbali kama elimu, wanyamapori na miundombinu na misaada mingine imekuwa ikipitia Umoja wa Ulaya” alisema Waziri Mahiga.

Akizungumzia ziara ya Balozi Adt nchini, Mhe. Waziri Mahiga alisema Mjumbe huyo Maalum wa Kansela wa Ujerumani ameleta ombi kwa Mhe. Rais na kwa Watanzania la kuiunga mkono Ujerumani kwenye nafasi ya  Mjumbe asiye wa Kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa  wakati wa uchaguzi utakaofanyika mwaka 2018. Aliongeza kusema kuwa, Ujerumani imedhamiria kugombea nafasi hiyo ikiwa na dhamira ya kuunga mkono mageuzi ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ikiwemo kuziunga mkono nchi za Afrika kwenye harakati za kupatiwa nafasi mbili za kudumu kwenye Baraza hilo.

Aidha, Mhe. Waziri Mahiga alifafanua kwamba, katika kufikia malengo hayo Ujerumani imejiwekea misingi mikuu minne ambayo ni:- Kusaidia jitihada za amani na usalama duniani; Kusimamia Haki ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa; Kuhamasisha mageuzi ya Teknolojia na Kuhimiza ushirikiano na Ubia wa Kimataifa.

Mhe. Mahiga alieleza kuwa kwa kuzingatia misingi hiyo, amemueleza Balozi Adt azma ya Tanzania kuiomba Ujerumani iisadie Afrika kujenga Jengo la Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ambapo Tanzania ndio Makao yake Makuu huko Mjini Arusha.

Mhe. Mahiga pia alimhakikishia Balozi Adt kuwa ameupokea ujumbe wa Kansela wa Ujerumani na atauwasilisha kwa Mhe. Rais.

Kwa upande wake Balozi Adt, Mjumbe Maalum kutoka Ujerumani alisema kuwa amefurahishwa na mapokezi aliyoyapata baada ya kuwasili nchini. Pia ana imani kuwa Tanzania ambao ni rafiki wa kihistoria wa Ujerumani itawaunga mkono kwenye nafasi hiyo ili kuwawezesha kutekeleza malengo waliyojiwekea ikiwemo kuhakikisha Afrika inapata nafasi mbili za kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

-Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 12 Machi, 2017

Thursday, March 9, 2017

Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa aipongeza Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Antonio Guterres (kushoto) kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam jana. Mhe. Guterres alisimama kwa muda katika uwanja huo akitokea nchini Kenya kwa ajili ya kufanya mazunguzmo na Balozi Mahiga. Katika mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine, Mhe Guterres aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa juhudi zake za kutafuta amani nchini Burundi kupitia kwa Msuluhishi wa Mgogoro huo Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Benjamin Willium Mkapa. 
Aidha, Dkt. Mahiga aliwasilisha Salamu Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Waziri Mahiga akizungumza jambo huku Mhe. Guterres akimsikiliza kwa makini.
 Dkt. Mahiga akiendelea kuzungumza na Mhe. Guterres huku Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy wakiwasikiliza kwa makini.
 Picha ya pamoja   

  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Bi. Mindi Kasiga naye akiagana na Mhe. Guterres  

Mhe. Guterres akiagana na Dkt. Mahiga mara baada ya kumaliza kufanya mazungumzo yao.



   PRESS RELEASE



UN SECRETARY GENERAL STOPS IN DAR ON HIS WAY TO NEW YORK

H.E. Dr. John Pombe Magufuli, the President of the United Republic of Tanzania has urged the United Nations to continue its support in bringing about political stability in Burundi and the Democratic Republic of Congo.

In his special message to the United Nations Secretary General Mr. Antonio Guterres President Magufuli explained that the recent instability in the two countries has created refugees’ influx in Tanzania and its neighbors, hence the region is committed to ensure political stability is restored.

Delivering President Magufuli’s message to the United Nations Secretary General Mr. Antonio Guterres, Tanzania’s Foreign Minister Augustine Mahiga said that as the chair of EAC, Tanzania is hopeful with the progress been made in the mediation process in Burundi under the leadership of President Yoweri Museveni of Uganda and facilitated by the former President of Tanzania, H.E. Benjamin William Mkapa. Hon. Mahiga also informed the UN Secretary General that the upcoming EAC Summit is expected to receive a progressive report about the process.

With regards to the Democratic Republic of Congo, Minister Mahiga revealed that the Southern African Development Community is intending to include the agenda of political transition in DRC, whereby SADC member states are expecting positive deliberations. Tanzania is the current chair of the SADC organ of political, defense and security with the mandate to support the achievement and maintenance of peace and security as well as the rule of law in the SADC region.

Upon receiving President Magufuli’s message, Mr. Guterres praised Tanzania for its ability to uphold principles of good governance in the country as well as maintaining peace and creating a peaceful environment in the EAC and SADC regions.

Mr. Guterres commended President Magufuli’s efforts in Burundi peace process, and his readiness to host refugees from Burundi, emphasizing the role played by regional communities in Africa in resolving leadership crisis in African countries.

“The United Nations appreciates the work done by President Mkapa in Burundi under the EAC and its leadership. If the region come together the way EAC has done in the case of Burundi, I am sure together they will be able to establish lasting solutions” he remarked.

Minister Mahiga told the reporters that President Magufuli met Mr. Guterres during the AU Summit in Addis Ababa earlier this year, where the two leaders exchanged cordial discussions about various issues concerning the region.

“President Magufuli instructed me to deliver his message to Mr. Guterres, and has also extended an invitation to the Secretary General at an appropriate time to have a working visit in the country” concluded Hon. Mahiga.

Mr. Guterres was met and held talks with Foreign Minister Mahiga at the Julius Nyerere International Airport yesterday night where he was on transit from Somalia and Kenya for a working visit. Also present at the airport was the United Nations Resident Coordinator, Mr. Alvaro Rodriguez and officials from the Ministry of Foreign Affairs including the Director of Multilateral Cooperation Ambassador Celestine Mushy and Ministry’s Spokesperson Ms. Mindi Kasiga. 

Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dar es salaam, Tanzania
March 9, 2017.

Wednesday, March 8, 2017

Waziri Mahiga akutana na Mabalozi wa Tanzania nchini Oman, Korea, Kampala,Uganda, Kenya, Algeria, Qatar na Sudan

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akizungumza  na Mabalozi wanao kwenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali (hawapo pichani), mazungumzo hayo yalifanyika leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. 
Mhe. Mahiga alitumia fursa hiyo kuwasisitiza umuhimu wa kutekeleza majukumu yao kikamilifu, sambamba na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania.
Waheshimiwa Mabalozi wakimsikiliza Waziri Mahiga,  kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima, Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Grace Mgovano na Balozi wa Tanzania nchini Korea, Mhe.  Matilda Masuka.
Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Mabalozi  wakimsikiliza Waziri Mahiga. Kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Sudan, Mhe. Silima  Haji, Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Rajab, Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Chana na Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Omar Mzee.
Mazungumzo yakiendelea.
Picha ya pamoja Mhe. Waziri na Waheshimiwa Mabalozi

Monday, March 6, 2017

Waziri Mahiga azungumza rasmi na Mabalozi kuhusu kuhamia Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiongea na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa yanayowakilisha hapa nchini (hawapo pichani) kwenye kikao kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Aziz P.Mlima. Katika kikao hicho Mhe. Mahiga aliwaeleza rasmi kuhusu mpango wa Serikali kuhamia Dodoma na kuwaomba nao kuwa tayari kuutekeleza.

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia kikao
Sehemu nyingine ya Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wakifuatilia kikao.
Kikao kikiendelea
Mkuu wa Mabalozi  ambaye pia ni Balozi wa Angola nchini, Mhe. Ambrosio Lukoki (kushoto) akizungumza katika kikao hicho. Pamoja na mambo mengine alieleza kuwa Jumuiya ya wanadiplomasia imelipokea agizo la Makao Makuu ya Nchi kuhamia Dodoma na kwamba wapo tayari kushiriki katika hatua zote za maandalizi ya kuhamia Dodoma ili kufanikisha zoezi la kuhama na kuisaidia Serikali katika huduma za ushauri na uzoefu wa namna nzuri ya kuhamisha miji mikuu.
Kulia ni Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin na Balozi Mlima wakifuatilia kikao.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao.
Balozi wa Malawi nchini Mhe. Hawa Ndilowe akichangia hoja katika kikao hicho.
Balozi wa Japan nchini, Mhe. Masaharu Yoshida naye akichangia hoja katika kikao.
Kikao kikiendelea.





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Balozi Mahiga aongea na Mabalozi kuhusu kuhamia Dodoma

Mabalozi na wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wa hapa nchini wametakiwa kuyahimiza makampuni ya nchi yao kutumia fursa za uwekezaji zinazotokana na zoezi la Serikali la kuhamia Dodoma. 
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) katika kikao maalum cha kuwafahamisha wanadiplomasia hao uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Tano wa kuhamia Dodoma.
“Uamuzi wa kuhamishia Makao Makuu ya Serikali mjini Dodoma umetengeneza fursa nyingi za uwekezaji katika maeneo mbalimbali kama vile utengenezaji wa vifaa vya ujenzi; ujenzi wa majengo ya ofisi, biashara na makazi; huduma za kijamii kama hospitali, shule, miundombinu ya maji safi na maji taka; TEHAMA; bustani za mapunziko; shughuli za kilimo na utalii. Hivyo, nachukua fursa hii kuwaomba muwahimize wawekezaji kutoka nchi zenu kuchangamkia fursa hizo”, Balozi Mahiga aliwambia wanadiplomasia wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.
Balozi Mahiga alieleza kuwa uamuzi wa kuhamisha Makao Makuu ya Serikali kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma ulifanywa mwaka 1973 lakini tokea kipindi hicho haukuweza kutekelezwa kutokana na sababu mbalimbali hadi Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ilipoingia madarakani.
Mhe. Waziri alieleza kuwa zoezi la Serikali kuhamia Dodoma limepangwa kutekelezwa kwa awamu nne ambapo awamu ya kwanza tayari imeshakamilika. Katika awamu hiyo, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imehamisha watumishi 47 kati ya 152 waliopo Makao Makuu akiwemo yeye mwenyewe, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu. 
Waziri Mahiga aliendelea kueleza kuwa kufuatia kuanza utekelezwaji wa uamuzi huo ambao ulitangazwa rasmi na Mhe. Magufuli alipochaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM tarehe 23 Julai 2016, hakuna budi kwa Ofisi za Balozi na Mashirika ya Kimataifa nazo zianze kujiandaa kwa ajili ya kuhamia mji huo Mkuu wa Serikali.  
Aliongeza kuwa, katika kipindi hiki cha mpito, baadhi ya Watumishi wa Wizara watakuwepo Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine watasaidia mawasiliano na ofisi hizo. Aidha, katika kipindi hicho, Wizara katika ofisi zake mpya zilizopo kwenye Jengo la LAPF mjini Dodoma itaimarisha mawasiliano kwa njia ya simu, mtandao wa internet na kufunga kifaa cha kufanyia mikutano kwa njia ya video ili kurahisisha mawasiliano na ofisi za Balozi.
Mhe. Mahiga aliwafahamisha Mabalozi hao kuwa Serikali itatenga eneo maalum ambalo litakuwepo kwenye mji wa Serikali utakaojengwa Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za balozi na mashirika ya kimataifa.  Alisema pindi Serikali itakapokamilisha zoezi la kupitia upya Mpango Mkuu wa Mji wa Dodoma, itawasiliana na Balozi hizo ili ziweze kuwasilisha maombi ya mahitaji ya ardhi wanayohitaji.
Balozi Mahiga alihitimisha kikao hicho kwa kuwashauri wanadiplomasia wanaomiliki majengo jijini Dar es Salaam kuingia makubaliano maalum na kampuni zinazohitaji ofisi hapa jijini ili kampuni hizo ziwajengee majengo ya ofisi mjini Dodoma. 
Kwa ujumla wanadiplomasia walipokea uamuzi huo na kuiomba Wizara iwasilishe taarifa hiyo kwa maandishi ili nao waiwasilishe kwenye Serikali zao kwa ajili ya utekelezaji.
                                                                                                                                                                         
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 06 Machi 2017.


                                                                                                                                                                         

Friday, March 3, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Palestina nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.Susan Kolimba amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Palestina hapa nchini Mhe.Hazem Shabat. Mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha mahusiano baina ya Tanzania na Palestina katika sekta mbalimbali.
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo kati ya Dkt. Kolimba na Balozi wa Palestina (hawapo pichani).Kutoka kushoto ni Bw. Hangi Mgaka, Bw. Charles Faini na  Bi. KisaDoris Mwaseba.
Mazungumzo yakiendelea.

Thursday, March 2, 2017

Waziri Mahiga akutana na Rais wa Mahakama ya Afrika ya haki za Binadamu na Watu

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo alipokutana na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jaji Sylvain Ore yenye Makao Makuu Jijini Arusha,Tanzania. Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Mhe. Wiziri Mahiga mjini Dodoma, wamejadili masuala mbalimbali ya kuboresha miundombinu ya mahakama hiyo ikiwemo majengo ya ofisi ili kuiongezea ufanisi zaidi.


Mazungumzo yakiendelea; Kushoto ni Wafanyakazi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu na kulia kwa Rais wa Mahakama, ni Mtumishi wa Wizara Bw. Beatus Kalumuna

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha na Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jaji Sylvain Ore mara baada ya mazungumzo

Picha ya Pamoja

Waziri Mhe. Mahiga akiongea na wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya mazungumzo

Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jaji Sylvain Ore akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo