Friday, October 9, 2020

TANZANIA,CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA MAHUSIANO YA KIMKAKATI

 Tanzania na China zimekubaliana kuendeleza mahusiano ya kimkakati baina yao ili kuwezesha uwepo wa ulingo sawa miongoni mwa mataifa katika kusimamia maslahi na maendeleo ya nchi husika katika jumuiya za kimataifa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John kabudi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke na kusisitiza umuhimu wa Mataifa kuheshimiana na kutokubali kuingilia uhuru wa mambo ya ndani ya nchi kwa kisingizio cha haki za binadamu,demokrasia ama jambo lolote jingine.  

Ameongeza kuwa mazungumzo hayo ya kimkakati yalilenga pia kutambua kuwa mwaka huu ni mwaka wa 55 tangu Tanzania na China zisaini mkataba wa urafiki ambao uliweka msingi wa mahusiano makubwa na ya dhati  katika nyanja za ulinzi na usalama,afya,kilimo, elimu na miundo mbinu ambapo mpaka sasa China ni Taifa linaloongoza hapa nchini kwa uwekezaji wa moja kwa moja kwa kuwekeza zaidi ya miradi 700 yenye thamani ya dola za Kimarekani (USD) bilioni 7.1 na kutengeneza zaidi ya ajira 87,000 kwa watanzania.

Kwa upande wake Balozi wa China hapa Nchini Mhe. Wang Ke amesema China wakati wote ni Rafiki mwaminifu na wa kudumu wa nyakati zote kwa Tanzania na kwamba kutimiza miaka 55 ya urafiki wa nchi hizo ni kielelezo tosha na siku zote wataendelea kuuheshimu na kuuenzi urafiki huo.

Katika hatua nyingine, Prof. Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Riitta Swan pamoja na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Pamela O'Donnell, ambapo pamoja na mambo mengine, Prof. Kabudi na mabalozi waliadili masuala mbalimbali ikiwemo kuimarisha mahusiano, Uwekezaji na Biashara, Afya, Elimu pamoja na Utalii.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akiongea na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke wakati walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam 

Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati wa mazungumzo yao leo jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akimkaribisha Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Riitta Swan kabla ya kuanza kwa mazungumzo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akimuonesha Balozi wa Canada nchini, Mhe. Pamela O'Donnell sheria ya uchaguzi kabla ya kumkabidhi sheria hiyo pamoja na nyaraka nyingine zinazohusu masuala ya uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba 2020


Thursday, October 8, 2020

RAIS MAGUFULI, RAIS CHAKWERA WAWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA MABASI MBEZI

 RAIS wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.John Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus Chakwera wameweka jiwe la msingi katika kituo kipya cha mabasi Mbezi Luis Jijini Dar es Salaam

Kabla ya kuweka jiwe la msingi, Rais Dkt.Magufuli ametoa maagizo, kwa waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kabla ya tarehe 30 Novemba 2020, vinginevyo mkandarasi atakatwa Pesa kwa kuchelewesha mradi.

Kituo hicho kinatarajiwa kuwa na uwezo wa kubeba mabasi 1,000 na teksi 280 kwa siku, Pia kutakuwa na maeneo ya bodaboda na bajaji na na eneo la mamalishe na babalishe.

Mbali na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha mabasi mbezi Luis, Rais Chakwera pia ametembelea maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), Kampuni ya Huduma za Kontena Bandarini (TICTS), Kituo cha Mizigo cha Malawi (Malawi Cargo Center) pamoja na Bandari ya Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera mara baada ya kumpokea katika eneo la ujenzi wa stendi mpya ya Mbezi Luis Jijini, Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera wakiwa wamesimama huku wakiimba nyimbo za Taifa za mataifa yote mawili kabla ya kuanza rasmi kwa shughuli ya uwekaji wa jiwe la msingi katika maradi wa ujenzi wa stendi mpya ya Mbezi Luis Jijini, Dar es Salaam




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika eneo la maradi wa ujenzi wa stendi mpya ya Mbezi Luis Jijini, Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera kuongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa stendi mpya ya Mbezi Luis Jijini, Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akimuonesha Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera mradi wa ujezi wa Reli ya Kisasa (SGR) wakati alipotembelea mradi huo  Jijini Dar es Salaam 


Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akiongea na wananchi (hawapo pichani) waliojitokeza wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa SGR jijini Dar es Salaam. Kushoto mwa Rais Chakwera ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Bw. Masanja Kadogosa akifuatiwa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isack Kamwele pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi.


Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera pamoja na mkewe Mama Monica Chakwera wakipokea zawadi kutoka kwa uongozi wa Kituo cha Mizigo cha Malawi (Malawi Cargo Center) wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa SGR jijini Dar es Salaam



Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa, Dkt. Lazarus Chakwera pamoja na mkewe Monica Chakwera wakimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa ya kuhudumia Makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Bw. Horace Hui mara baada ya kutembelea kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa, Dkt. Lazarus Chakwera akiongea na wananchi pamoja na waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati alipotembela Bandari ya Dar es Salaam leo jijini Dar es Salaam


 

BALOZI WA TANZANIA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA MFALME WA LUXEMBOURG


 Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji ambaye anawakilisha pia nchini Luxembourg, Mhe. Jestas Abuok Nyamanga amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Mfalme wa Luxembourg, Grand Duke Henri tarehe 2 Oktoba 2020.

Wakati wa hafla hiyo, Balozi Nyamanga na Mfalme Henri walifanya mazungumzo kuhusu umuhimu wa kuongeza wigo wa ushirikiano baina ya nchi mbili hizi na kutumia ipasavyo fursa mbalimbali zilizopo kwa ajili ya manufaa ya pande mbili. Miongoni mwa maeneo ya ushirikano yaliyojadiliwa ni pamoja na ushirikiano wa anga hususan ndege za mizigo, ushirikiano katika sekta za kifedha na kibenki na sekta ya madini hususan madini ya chuma kama yale ya Mchuchuma na Liganga, eneo ambalo Luxembourg ina uzoefu mkubwa.

Matukio katika Ubalozi wa Tanzania, Abu Dhabi

KUTAFUTA SOLO LA KOROSHO

Mhe. Balozi Mohamed Mtonga alifanya mazungumzo na wafanyabiashara, Bw. Abdo Shamakh Al-Shibani wa kampuni ya SHAFA iliyopo Dubai na Bw. Dzhuraev Khairullo ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya FoodArt LLC yenye Makao Makuu yake mjini Moscow nchini Urusi. Kampuni ya FoodArt LLC imekuwa ikinunua korosho sehemu mbalimbali duniani na kuziuza katika nchi mbalimbali za Ulaya ikiwamo Urusi.

Mhe. Balozi Mtonga aliwaonesha fursa ya kuweza kununua zao la korosho kutoka Tanzania na kuwapa mwongozo wa ununuzi kama ulivyotolewa na Wizara ya Kilimo na Ushirika na Bodi ya Korosho Tanzania.

Kwa ujumla wafanyabiashara hao walionesha dhamira ya kununua zao la korosho kutoka Tanzania katika msimu huu wa mwaka 2020/2021.

KUKABIDHI UENYEKITI WA SADC

Mhe. Balozi Mohamed Mtonga alikabidhi Uwenyekiti wa SADC Group of Ambassadors hapa Abu Dhabi kwa Balozi wa Nchi ya Msumbiji. Mhe. Balozi Tiago Recibo Castigo. Balozi Tiago, alimshukuru Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa Mwenyekiti wa SADC aliyemaliza muda wake kwa mafanikio makubwa katika kipindi chake cha uenyekiti licha ya changamoto ya ugonjwa wa COVID-19.


KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

Mhe. Mohamed Abdallah Mtonga, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu alifanya mazungumzo na Wakurugenzi wa Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Abu Dhabi (ADNOC), Bw. Khaled Salmeen, Bw. Iman Al Hosani, Bw. Mohamed Al Suwaidi na Bw. Abdulla Al Qubaisi kwa njia ya mtandao (Virtual Meeting).

Balozi alitumia fursa hiyo kuwajulisha fursa kadhaa zilizopo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia katika eneo hili la Mafuta na Gesi. Maeneo aliyowajulisha kwa uwekezaji ni yale yaliyohusu uwekaji wa miundombinu katika biashara ya Gesi na Mafuta. Aidha, Balozi aliwajulisha fursa za kibiashara katika biashara ya mbolea aina ya Urea kwa utaratibu wa Bulk Procurement System unaoratibiwa na Tanzania Fertilizers Regulatory Authority na uletaji wa Mafuta kwa pamoja unaoratibiwa na Bulk Procurement System for Petroleum Products. Bidhaa zote hizi huzalishwa na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Abu Dhabi (Abu Dhabi National Oil Company (ADNOC).

Vilevile, Balozi aliwasilisha kwa ADNOC miradi ambayo ipo tayari kwa uwekezaji iliyopo katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (Tanzania Investment Centre) ambayo inatafuta wawekezaji au wabia.

Miradi hiyo ni kama ifuatavyo:

·       Establishment of Strategic Petroleum Reserve Infrastructures (Farm Tanks).

Kwa mujibu wa andiko Mradi utajikita katika ujenzi wa Matanki ya kuhifadhia mafuta katika miji ya Dar Es Salaam, Morogoro, Isaka(Kahama),Makambako, Mbeya, Songwe na Tanga. Watekelezaji wa Mradi huu ni Mwekezaji Mshirika (Strategic Partner) na Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (Tanzania Petroleum Development Corporation). 

·       LPG Bulk Distribution Project

Kwa mujibu wa andiko Mradi huu ni kuweka miundombinu ya Kupokea,kuhifadhi na kuweka miundombinu ya kujaza Gesi aina ya LPG. Mradi huu utatekelezwa kwa awamu katika miji ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara. Watekelezaji wa Mradi huu ni Mwekezaji Mshirika (Strategic Partner) na Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (Tanzania Petroleum Development Corporation).

Kwa upande wao, Wakurugenzi wa ADNOC wamehitaji taarifa mbalimbali ambazo Mhe. Balozi Mohamed Mtonga ameziwasilisha katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania kwa kufanyiwa kazi.







 

Wednesday, October 7, 2020

RAIS MHE.DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMPOKEA MGENI WAKE RAIS WA MALAWI DKT. LAZARUS CHAKWERA JIJINI DAR ES SALAAM

 


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi akiongea jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi wakati walipokuwa wakimsubiri Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam. Kushoto mwa Balozi Kijazi ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akikagua Gwaride la Heshma lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal 1 Jijini Dar es Salaam 



Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani) kutoka Tanzania na Malawi mara baada ya mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari kutoka Tanzania na Malawi (hawapo pichani) katika mkutano na Waandishi wa Habari mara baada ya mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera


Waziri wa Mabo ya Ndani Mhe. George Simbachawene mwenye (suti ya blue) pamoja na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge (kushoto) wakiwa pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali wakifuatilia mkutano wa pamoja wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Chakwera wakati walipokuwa wakiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) Ikulu Jijini Dar es Salaam.








Tuesday, October 6, 2020

ZIARA RASMI YA KITAIFA YA SIKU TATU YA RAIS WA MALAWI DKT. LAZARUS MCCARTHY CHAKWERA

 






RAIS DKT MAGUFULI AMUANDIKIA BARUA YA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIONGOZI MPYA WA KUWAIT

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemwandikia barua ya salamu za rambirambi Kiongozi mpya (Amir) wa Kuwait, Mtukufu Sheikh Nawaf Al-Ahmad Al-Sabah kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait hapa nchini amemkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait.

Prof. Kabudi amesema Tanzania na Kuwait zina mahusiano mazuri sana na muda mrefu katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo akitolea mfano wa mfuko wa Kuwait ambao umekuwa wa msaada mkubwa katika kwa Tanzania ambao umekuwa ukisaidia katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali hapa nchini ikiwemo barabara.

Ameongeza kuwa msiba wa Kiongozi huyo wa Kuwait ni msiba wa Watanzania wote kwa kuwa kwa muda wote ambao Hayati Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah amekuwa Kiongozi wa Taifa hilo amekuwa karibu sana na Tanzania.


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Kuwait nchini, kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Taifa hilo Mtukufu Sheikh Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-sabah.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John akimkabidhi Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan barua iliyoandikwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kwa Kiongozi mpya wa Kuwait


 


Balozi wa Kuwait Mhe.Mubarak Mohammed Alsehaijan akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John mara baada ya kumaliza kusaini kitabu cha maombolezo 





Friday, October 2, 2020

Mradi wa Umeme wa Pamoja wa Tanzania, Burundi, Rwanda Wafikia Pazuri


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akipokelewa na Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Mutukula, alipowasili kwenye kituo hicho kujionea shughuli zinavyoendelea.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge akikagua ubora wa mashine ya kukagulia mizigo iliyofungwa katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha Mutukula.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiongea na mmoja wa wafanyakazi wa Kituo cha Hudum kw Pamoja Mpakani cha Mutukula.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akisaini kitabu cha kabla ya kuanza kikao na watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Mutukula.


Mkurugenzi wa Miundombinu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Kamugisha Kazaura akitoa maelezo namna EAC inavyoratibu upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kikanda. 




Ujenzi wa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge  akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye eneo unapojengwa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera.


Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Dkt. Jilly Maleko akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye eneo unapojengwa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera.

 Mhandisi wa Kampuni inayojenga Mtambo wa kuzalisha umeme katika Mto Kagera akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mtambo huo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiuliza maswali kwa wahandisi wanaojenga mradi wa kuzalisha umeme katika Mto Kagera.

Sehemu ya Eneo unapojengwa Mtambo wa Kuzalisha Umeme katika Mto Kagera.

OSBP ya Rusumo

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akisalimiana na watumishi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo, mara baada ya kuwasili kituoni hapo kwa ziara ya kikazi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiongea na Mtalaam wa Afya katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.

Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo, Bw. Jackson Mushi akitoa taarifa ya utekelezaji wa kituo hicho kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  IbugeA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge akiongea na watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo

Watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo wakiwa katika kikao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge.

Mkurugenzi wa Miundombinu kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Kamugisha Kazaura na Msaidizi wa Katibu Mkuu, Bw. Hangi Mgaka wakitabasamu akati wa kikao cha briefing kwenye Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dkt. Jilly Maleko, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhandisi Steven Mlote pamoja na ujumbe wao akitemb kwa miguu kuelekea katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.

Malori yakiwa katika foleni ya ukaguzi katika Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.

Bango la kutoa elimu kuhusu wafanyabiashara wadogo wanavyoweza kufanya shughuli zao katika nchi a EAC bila usumbufu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert  Ibuge na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani cha Rusumo.