Thursday, December 10, 2020

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE, MHE. OLE NASHA ALIVYOPOKELEWA WIZARANI

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. William Tate Ole Nasha akipokea shada la maua kutoka kwa mmoja wa Watumishi wa Wizara Bi. Amina Abdallah  ikiwa ni ishara ya kukaribishwa mara alipowasili Wizarani baada ya kuapishwa Ikulu tarehe 9 Desemba 2020.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akimkaribisha Wizarani Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. William Tate Ole Nasha mara baada ya kula kiapo Ikulu tarehe 9 Desemba 2020
Mhe. Prof. Kabudi akimtambulisha Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi kwa Naibu Waziri Mhe. Ole Nasha wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Mhe. Prof. Kabudi akimtambulisha Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Alex Mfungo kwa Naibu Waziri Mhe. Ole Nasha wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Mhe. Ole Nasha akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Wizarani

Mhe. Ole Nasha akiwa ofisini kwake baada ya kuwasili Wizarani

Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akimkabidhi  Mhe. Ole Nasha Ilani ya Chama cha Mapinduzi kama moja ya kitendea kazi chake anapoanza majukumu yake mapya Wizarani 


Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi kwa pamoja na Sehemu ya Menejimenti ya Wizara  wakimsikiliza Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha alipozungumza nao mara baada ya kupokelewa rasmi Wizarani
 Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Caesar Waitara wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Agnes Kayola wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Swalehe Chondoma wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ugavi na Ununuzi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Salifius Mligo wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani.

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Japhary Kachenje wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Agnela Nyoni wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Caroline Chipeta wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Masoud Balozi wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Macocha Tembele wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Aman Mwatonoka wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Buhohela wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw.  Gwamaka Lazarous wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani




Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Isaac Kalumuna wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Leonce Bilauri wakati wa mapokezi yake alipowasili Wizarani


Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani

Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akisalimiana na mmoja wa Watumishi wa Wizara waliofika kumpokea  alipowasili Wizarani
aibu Waziri, Mhe. Ole Nasha akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Wizara mara baada ya  Wizarani baada ya kuapishwa

Mhe. Prof. Kabudi akiwa na Mhe. Ole Nasha wakizungumza na Watumishi wa Wizara

Picha ya pamoja  kati Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (wa tatu kushoto mstari wa kwanza)  na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. William Tate Ole Nasha (wa nne kulia mstari wa kwanza) pamoja na Watumishi wa Wizara walioshiriki mapokezi ya Mhe. Ole Nasha alipowasili Wizarani baada ya kuapishwa  
==========================================

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. William Tate Ole Nasha ameahidi ushirikiano kwa Watumishi wa Wizara katika kuhakikisha Wizara inakuwa na matokeo chanya yenye tija kwa jamii na Taifa kwa ujumla katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mhe. Ole Nasha ameyasema hayo aliwapowasili Wizarani mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika hafla iliyofanyika Ikulu, Chamwino jijini Dodoma tarehe 9 Desemba 2020.

Mhe. Ole Nasha ambaye alipokelewa na Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema kuwa yupo tayari kujifunza kutoka kwa Watumishi wote ili kuiwezesha Wizara kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake. Prof. Kabudi alimhakikishia Mhe. Ole Nasha ushirikiano wake binafsi na kutoka kwa Watumishi wote na kwamba uwepo wake utaongeza nguvu za kuifikisha Wizara katika viwango vya juu kiutendaji.



























 

Tuesday, December 8, 2020

HABARI KATIKA PICHA MAHAFALI YA 50 YA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimkabidhi zawadi ya vitabu Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwasilisha salamu za Serikali kwenye mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi moja kati ya zawadi Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah


Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku shahada ya heshima Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Netumbo Ndaitwah


Baadhi ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiwa ukumbini tayari kwa ajili ya kutunukiwa shahada  


Baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa Nchini wakifuatilia sherehe za mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika mahafali ya 50 ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam


FURSA YA AJIRA


 

Monday, December 7, 2020

WAKURUGENZI NA WAKUU WA IDARA WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI WAPIGWA MSASA KUHUSU MANUNUZI YA UMMA

Mkurugenzi wa Rasilimali watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Alex Mfungo akizungumza na Wakurugenzi Idara na wakuu wa Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ( hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya manunuzi ya Umma yanayofanyika Mkoani Morogoro

TANZANIA, NAMIBIA ZAKUBALIANA KUIMARISHA SEKTA ZA UVUVI NA MIFUGO

Katika jitihada za kuendeleza Diplomasia ya Uchumi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekubaliana na Jamhuri ya Namibia kuimarisha sekta za uvuvi na mifugo.

Makubaliano hayo yamefanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) amekubaliana na Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah kuimarisha ushirikiano katika sekta ya Uvuvi pamoja na Sekta ya Mifugo.

"Tumekubalina kuimarisha ushirikiano katika enao la uvuvi wa bahari kuu lakini pia kuwahamasisha wadau wa sekta binafsi kutoka Tanzania na Namibia kuwekeza katika eneo hilo. Kwa upande wa mifugo na uuzaji wa nyama nchi za nje Namibia wamepiga hatua kubwa sana na sasa wanauza nyama Ulaya na Asia," Amesema Prof. Kabudi

Aidha, Prof. Kabudi ameongeza kuwa wamekubaliana pia kuhamasisha sekta binafsi kutoka Namibia kuja kuwekeza katika machinjio na viwanda vya kusindika nyama hapa nchini (Tanzania) kwa ajili ya kuuza nyama hiyo nje ya Tanzania na kuendeleza sekta za uvuvi na mifugo.

Pamoja na mambo mengine, kikao cha leo kimepitia makubaliano ya miaka miwili iliyopita ambapo Tanzania na Namibia zimekubaliana kutumia fursa zilizopo kati yao kuendeleza sekta za uwekezaji, uvuvi, kilimo na mifugo kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah amesema kuwa wamekubaliana kuimarisha sekta mbili ambazo ni Uvuvi na mifugo pamoja na kilimo kwa ujumla kwa kuzingatia mazingira bora ya uwekezaji na biashara ndani ya Umoja wa Afrika (AU).

"Kuna maeneo mbalimbali ambayo kwa pamoja tumekubaliana kuyaimarisha ikiwemo uvuvi, mifugo na kilimo kwa ujumla, kupitia kikao cha leo tunaamini kuwa wawekezaji kutoka Namibia watakuja kuwekeza Tanzania na vilevile wawekezaji kutoka Tanzania watawekeza Namibia," Amesema

Ameeleza kuwa Namibia itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Tanzania katika kuhakikisha kuwa wanakuza uchumi wa nchi zetu zote mbili na Afrika kwa ujumla kwa kuzingatia misingi ya biashara na uwekezaji iliyopo ndani ya Umoja wa Afrika (AU).

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) akimuelezea jambo Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi katika picha ya pamoja. Kushoto mwa Mhe. Ndaitwah ni Balozi wa Namibia hapa nchini, Mhe. Theresia Samaria ambaye amamaliza muda wake wa utumishi, na Kulia mwa Prof. Kabudi ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Bw. Frank Mwega. 


Naibu Waziri Mkuu Wa Jamhuri ya Namibia ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi zawadi za vitabu 



TANZANIA YAUNGA MKONO AZIMIO LA AU KUONGEZA MIAKA 10 YA KUONDOA NA KUTOKOMEZA SILAHA HARAMU

Umoja wa Afrika (AU) umezitaka nchi wanachama wa umoja huo kutilia mkazo azimio la kuondoa na kutokomeza silaha haramu ili kuliondoka na migogoro inayolifanya bara hilo kushindwa kusonga mbele kiuchumi.

Akifungua Mkutano wa 14 wa dharura wa Umoja wa Afrika unaofanyika kwa njia ya mtandao (virtual Conference) Mwenyekiti wa Umoja huo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa amesema ni vigumu Bara la Afrika kupiga hatua za kimaendeleo kiuchumi endapo suala la usalama halitapewa kipaumbele na kuruhusu migogoro kuendelea.

Rais, Ramaphosa ameongeza kuwa wakati umefika kwa nchi za afrika hususani zilizopo katika migogoro na vita kuhakikisha kuwa zinatatua vyanzo vya machafuko hayo na kuboresha hali ya kiuchumi kwa wananchi, utawala wa sheria, na kuzingatia misingi ya haki na utawala bora.

Akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Meh. John Pombe Joseph Magufuli katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi amesema mkutano huo ulikuwa unajadili mpango na mkakati wa miaka 10 iliyopita wa kuondoa na kutokomeza silaha haramu na kujenga amani katika bara la Afrika.

"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeunga mkono azimio la nchi za AU kuongeza miaka mingine 10 ya kutokomeza silaha haramu na kusisitiza tena ushiriki wake kikamilifu katika kuhakikisha kuwa Afrika inatatua migogoro yake yote yenyewe bila kuingiliwa na nchi za nje, lakini pia kuzitaka nchi za Afrika kuzuia mitafaruku na migogoro yote ambayo kwa miaka mingi imeigharimu sana bara la Afrika," Amesema Prof. Kabudi

Prof. Kabudi ameongeza kuwa, toka hatua ya kuondoa na kutokomeza silaha haramu ilipoanza mwaka 2017 hadi 2019, silaha zaidi ya 1,233 zimerejeshwa na Serikali itaendelea na jitihada ya kuhakikisha kuwa inazitambua silaha zote.

Aidha, Prof. Kabudi ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi zote ili kuwa na amani endelevu na utulivu endelevu katika eneo lote la Maziwa Makuu, pia Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa mchango wake katika nchi mbalimbali zenye mapigano ikiwemo DRC halikadhalika katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na sehemu nyingine ambapo vikosi vyake vya kijeshi vitatumwa kulinda amani.     

Nae Rais wa Ghana, Mhe. Nana Akufo-Addo amesema kuwa Ghana inaungana na Umoja wa Afrika (AU) na itaendelea kuhakikisha inaondoa na kutokomeza silaha haramu kwa lengo la kuimarisha masuala ya Amani, umoja na ushirikiano wa nchi za AU.

"Ghana tangu mwaka 2014 tulishaanza mkakati wa kuzuia na kutokomeza matumizi holela silaha haramu kwa kuzihakiki na kuandikisha wamiliki wote wanaomiliki silaha,….….pia mwaka jana 2019 kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) tumeweza kuendelea kudhibiti silaha matumizi ya silaha holela," Amesema Rais Akufo-Addo

Nae Rais wa Somalia, Mhe. Mohamed Farmajo amesema kuwa suala la Amani na usalama ni suala muhimu sana kwenye jamii hivyo Somalia inaungana na Umoja wa Afrika katika kuhakikisha kuwa wanaondoa na kutokomeza silaha haramu na kujenga amani katika bara la Afrika.

Rais Mohammed ameongeza kuwa amani na usalama vitakumbukwa kuwa ni msingi wa maendeleo kwenye katika jamii. Aidha, Rais huyo ameuomba umoja wa Afrika kushirikiana kwa karibu na Somalia katika kuhakikisha kuwa wanatokomeza vikundi vya kigaidi (Alshabab) kwa maendeleo ya ukanda wa Afrika.

Pamoja na mambo mengine, Umoja wa Afrika umekubaliana kuongeza muda wa kuondoa na kutokomeza silaha haramu na kujenga amani katika bara la Afrika kwa kipindi cha miaka 10 ijayo kuanzia mwaka 2021 hadi 2030.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi akichangia moja ya agenda katika mkutano wa 14 wa dharua Umoja wa Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao (virtual Conference) jijini Dar es Salaam 



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi akiwa pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe pamoja na washiriki wengine wakifuatilia mkutano wa 14 wa dharua Umoja wa Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao (virtual Conference) 



Sunday, December 6, 2020

MAWAZIRI SADC - TROIKA WAJADILI UPIGAJI KURA KWA WAGOMBEA WA KAMISHENI YA AU

Mawaziri wa SADC Double Troika wamejadili na kutolea maamuzi mapendekezo ya namna ya kupigia kura kwa wagombea kutoka Kundi la Kusini wanaowania nafasi mbalimbali kwenye Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika katika Mkutano Mkuu wa 34 mwezi Februari, 2021.

Majadiliano hayo yamefanyika katika mkutano wa Mawaziri ulifanyika mwishoni mwa wiki (Ijumaa) kwa njia ya mtandao (Video Conference) chini ya Uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano kutoka Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Verónica Nataniel Macamo Dlhovo.

Aidha, Mkutano wa Mawaziri ulitanguliwa na Kikao cha Makatibu Wakuu siku hiyo hiyo ambapo kikako hicho kilichoratibiwa chini ya Uenyekiti wa Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda na Kibara na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa SADC kutoka Jamhuri ya Msumbiji, Balozi Alfredo Fabiao Nuvunga.

Katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) aliwakilishwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.

Itakumbukwa kuwa, mnamo mwezi Juni, 2020 Umoja wa Afrika (UA) ulitangaza nafasi za kazi za ngazi za juu ikiwa ni pamoja na nafasi ya Mwenyekiti wa Kamisheni (1), Naibu Mwenyekiti wa Kamisheni (1) na Makamishna (6). Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika zilialikwa kushiriki katika mchakato huo kwa kutangaza na kuhamasisha umma kuomba nafasi hizo.  

Tanzania pia ni nchi mojawapo inayogombea nafasi mbalimbali kwenye Kamisheni ya Umoja wa Afrika. Nchi zilozoshiriki katika mkutano huo ni pamoja Msumbiji, Malawi, Tanzania, Botswana Afrika Kusini na Zimbabwe. 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika Mkutano wa Mawaziri wa SADC Double Troika kwa njia ya mtandao (Video Conference) jijini Dar es Salaam  

 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika Mkutano wa Mawaziri wa SADC Double Troika kwa njia ya mtandao (Video Conference) jijini Dar es Salaam 

 




MKUTANO WA DHARURA WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA UMOJA WA AFRIKA WAFANYIKA KWA NJIA YA MTANDAO (VIRTUAL MEETING)

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika Mkutano wa dharura wa 13 wa Umoja wa Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandano            (Virtual Meeting) mkutano uliohusu umuhimu wa mkataba wa eneo huru la biashara la Bara la Afrika. Prof. Palamagamba amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mabilionea kutoka nchini Japan wavutiwa na fursa za uwekezaji nchini


Mabilionea kutoka nchini Japan wavutiwa na fursa za uwekezaji nchini 

Tarehe 3 Disemba 2020 kundi la Watalii 37 kutoka nchini Japan liliwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya kutalii sambamba na kufanya mikutano 

ya mafunzo. Watalii hawa wanaofahamika kama Klabu ya Mabilionea (Billionaires Club) watakuwepo nchini kuanzia tarehe 3 hadi 10 Disemba 2020. Watalii hawa ambao watatembelea vituo mbalimbali vya utalii nchini ni viongozi na wamiliki wa makampuni kutoka katika sekta mbalimbali nchini Japan. 

Watalii hao mara baada ya kuwasili nchini walipata fursa ya kusikiliza mawasilisho (presentation) kutoka taasisi mbalimbali kama vile Mamlaka ya Hifadhi Tanzania, Kituo cha Uwekezaji Tanzani na Bodi ya Utalii ya Tanzania ambapo, sambamba kufahamishwa zaidi kuhusu Tanzania, vilevile walielezwa kuhusu fursa na taratibu za kuwekeza katika sekta mbalimbali nchini.

Watalii hao wengi walionesha kuvutiwa na fursa za uwekezaji zilizopo nchini na kuridhishwa na namna Serikali ilivyoandaa mazingira rafiki kwa wawekezaji. Akizungumza baada ya kusikiliza mawasilisho Bi. Nanako Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kutengeneza viungo bandia vya binadamu, alisema amevutiwa na fursa zilizopo katika sekta ya afya na namna Serikali ilivyojiandaa kutoa motisha kwa wawekezaji wa eneo hilo hapa nchini. Maeneo mengine ya uwekezaji yaliyowavutia watalii hao ni sekta ya utalii, usafirishaji, kilimo na viwanda. 

Watalii hawa wametembelea hapa nchini kwa juhudi kubwa za utangazaji na uhamasishaji utalii zinazoendelea kufanywa na Bodi ya Utalii Tanzania kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Japan ambao unafanya juhudi kubwa ya kufungua soko la utalii la Japan kwa vivutio vya utalii vinavyopatikana hapa nchini hasa baada ya mlipuko wa ugonjwa wa Corona. 

Vilevile watalii hao wametaja mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika kupambana na mlipiko wa ugonjwa wa CORONA, amani iliyopo nchini, ukarimu wa watanzania na uwepo wa vivutio hadhimu vya utalii nchini ni miongoni mwa sababu nyingi zilizowafanya kuja kutalii Tanzania.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya Watali hao Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania Haji Thomas Mihayo  alisema Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020-2025 inazungumzia kukuza utalii wa mikutano ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hapa nchini Pamoja na kuongeza mapato kufikia Dola Billioni 9. "Sisi Bodi ya Utalii Tanzania Pamoja na Balozi zetu utekelezaji wa ilani umeshaanza mara moja, kwani katika kipindi hiki cha miaka mitano ya pili ya awamu hii ya tano ya muheshimiwa Rais Dr. John Pombe Magufuli tunalengo la kufikia watalii million 5 na utalii wa mikutano ni moja ya aina za utalii zitakazosaidia kufikia lengo hilo.

Baadhi ya Watalii kutoka nchini Japan wakijanza taarifa kwenye fomu maalumu mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA) 

Watalii kutoka nchini Japan  wakiwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA)
Watalii kutoka nchini Japan  wakisikiliza mwasilisho (presentation) kutoka kwa Wataalamu wa Taasisi za Serikali zilizolenga kuwaelezea kuhusu fursa na taratibu za kuwekeza nchini Tanzani. Mawasilisho hayo yalifanyika katika eneo la Hoteli ya Serena iliyopo mbugani Serengeti.
Watalii kutoka nchini Japan  wakiendelea kufutalia mwasilisho (presentation) kutoka kwa Wataalamu wa Taasisi za Serikali zilizolenga kuwaelezea kuhusu fursa na taratibu za kuwekeza nchini Tanzani.